Sunday, December 21, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 7




Bwana alizungumza waziwazi. Wakati huu, shughuli za kiroho za makanisa zinapingana na kile ambazo niliwakusudia. Viongozi na waumini wananiabudu kimazoea tu na wananijua kwa nadharia tu za vitabuni. Iweni na shauku kubwa kisha mnijie Mimi.


Bwana wetu ana shauku ya kutuonyesha uhalisia wa kuingia kwenye mapambano ya kiroho dhidi ya mapepo wabaya na kufungua macho yetu ya kiroho ili kwamba tuweze kuona moja kwa moja Mbinguni, kuzimu, malaika na shetani. 

Saturday, December 13, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 6







====  SIKU YA 13  ==== 

Kim, Joo-Eun 

Leo yalikuwapo mashambulizi makubwa kutoka kwa mapepo. Wakati ninaomba, nilipelekwa hadi kwenye sehemu yenye giza, ambayo nilijua kuwa ni kuzimu. Niliona mapepo mengi ambayo yalikuwa yamezunguka kiumbe kikubwa kiovu. Kiumbe hiki kikubwa kilionekana kina hamaki pamoja na hofu. Kilipiga kelele na kuhaha huku na huku, na kuonekana kimechanganyikiwa na kisichokuwa na utulivu.


Wednesday, December 10, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 5






====  SIKU YA 11  ====

Kim, Joo-Eun

Kadiri nilivyoomba kwa bidii, nuru kali ilitokea mbele yangu, na mbele ya hiyo nuru alisimama Yesu. "Joo-Eun, nakupenda. Omba bila kukoma; omba kwa bidii; omba kwa moyo wako wote. Usiache kuomba." Nilihisi ujotojoto na niliweza kumwona Yesu kwa wazi zaidi. Ndipo nikatambua ni kwa nini Yesu aliniambia niinue mikono yangu juu zaidi. Niliweza kumwona wazi zaidi nilipofanya hivyo. Nikamwambia, "Haa! Nakuona waziwazi, Bwana. Ni vizuri sana, Yesu. Nakushukuru." Kutokana na kule kujisikia vizuri sana, nilijikuta ninaacha kuomba kwa muda kidogo. Mara lilitokea pepo chafu. Lilikuwa jeusi tii kuliko giza. Nikalifukuza kwa Jina la Yesu, na nikaendelea kuomba kwa kunena kwa lugha. 

Sunday, July 27, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 4




====  SIKU YA 10  ====

Kim, Joo-Eun: 
Wakati nikiwa nimezama katika kuomba kwa lugha, joka jekundu lilinitokea. Lilikuja kwangu kwa kasi na kunirukia. Lilikuwa na macho kama ya mamba na makucha makubwa makali, na likajaribu kunitisha kwa makucha yake. Moshi unaotia kinyaa ulitoka kwenye pua zake. "Ewe shetani mbaya, ondoka kwangu kwa Jina la Yesu." Nilikuwa napaza sauti kama mwanamke mwenye wazimu. Ndipo joka hilo likaelekea upande wa kaka  Haak-Sung.  Haak-Sung akashtuka. Kuomba

Saturday, July 19, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 3


Huu ni ushuhuda unaotokana na kitabu kinachojulikana kama Baptized by Blazing Fire, Devine Expose of Heaven and Hell kilichoandikwa na Mchungaji Yong-Doo Kim wa Korea. Ni ushuhuda mrefu ambao utakupa mafundisho, maonyo, utakutia moyo na kukuimarisha katika safari yetu ya kuelekea kwa Baba, Mbinguni.

Wednesday, July 16, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 2





Huu ni ushuhuda unaotokana na kitabu kinachojulikana kama Baptized by Blazing Fire, Devine Expose of Heaven and Hell kilichoandikwa na Mchungaji Yong-Doo Kim wa Korea. Ni ushuhuda mrefu ambao utakupa mafundisho, maonyo, utakutia moyo na kukuimarisha katika safari yetu ya kuelekea kwa Baba, Mbinguni.

Monday, July 14, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 1




Huu ni ushuhuda unaotokana na kitabu kinachojulikana kama Baptized by Blazing Fire, Devine Expose of Heaven and Hell kilichoandikwa na Mchungaji Yong-Doo Kim wa Korea. Ni ushuhuda mrefu ambao utakupa mafundisho, maonyo, utakutia moyo na kukuimarisha katika safari yetu ya kuelekea kwa Baba, Mbinguni.

Tuesday, June 24, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 10




Sura ya 8: Silaha za Mwamini


- Jina la Yesu
- Damu ya Yesu
- Neno la Mungu
- Sifa za Mkristo


Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.” (Efe 6:10-11). 

“Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.” (Ufu 12:11).

Sunday, June 22, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 9




Sura ya 7: Kazi za Maajenti wa Shetani

Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” (Eph 6:11-12). 

Kitabu hiki hakitakuwa kimekamilika iwapo hakitaweka wazi mbinu mbalimbali za utendaji kazi za hizi nguvu za giza. Pia ni muhimu kwamba namna mbalimbali za kujidhihirisha kwao nazo ziwekwe wazi.

Tuesday, June 17, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 8




Sura ya 6: Majaribu na Ushindi

Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata. Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.” (Yohana 10:27-28) 

Baada ya kumpokea Kristo, jambo la kwanza lililotokea lilikuwa ni kutoweka kwa zawadi zote ambazo nilipewa kule baharini, yaani teleskopu, TV, mashati, picha nilizopiga kwenye maabara za ndani ya bahari na picha za malkia wa pwani ambazo zilikuwa nyumbani kwangu.

Saturday, June 7, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 7



Sura ya 5: Kukutana kwangu na Yesu Kristo

Mwezi wa February 1985, tulikuwa na mkutano wetu wa kawaida baharini. Baada ya hapo niliamua kusafiri hadi Port Harcourt kwenye Jimbo la Rivers, kumtembelea mke wa marehemu mjomba wangu. Nilikutana na mtu aliyeitwa Anthony. Alikuwa na karakana yake kule Nwaja Junction, kwenye barabara ya Trans-Amadi, Port Harcourt, Jimbo la Rivers. Alituma ujumbe niende kwake na kwa kuwa kwenye kundi letu tuna sheria kwamba usikatae wito, niliamua kwenda. Nilienda kwake mchana siku ya Alhamisi. Alianza kwa kusema, “Mungu amenipa ujumbe kwa ajili yako.” Alitoa Biblia yake na kuanza kuhubiri. Kulikuwa na Wakristo wengine watatu wamekaa (mwanamume na wanawake wawili). Aliendelea na mahubiri yake kwa muda mrefu na sina uhakika kama niliyasikia yote. Hatimaye aliniambia nipige magoti kwa ajili ya kuombewa. Nilitii na nikapiga magoti kimyakimya.

Monday, June 2, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 6



Sura ya 4: Jinsi shetani anavyopambana na Wakristo


“Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” (Efe 6:12) 

Kupambana na Wakristo
Baada ya amri kutoka kwa Lusifa ya kupambana na Wakristo, tulikaa na kupanga njia zetu za kupambana nao kama ifuatavyo:

Sunday, April 27, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 5



Kufanywa kuwa ajenti wa shetani

Sikuwa na hisia za kibinadamu wala huruma ndani ya moyo wangu tena. Niliingia kazini mara moja na kuharibu nyumba tano kwa wakati mmoja. Nyumba hizo zilizama ardhini pamoja na wakazi wake wote. Tukio hili lilitokea Lagos  Agosti 1982. Kontrakta aliyejenga nyumba hizo alishikiliwa kwa kosa la kutoweka msingi imara na alilipa faini kubwa sana. Uharibifu mwingi unaotokea duniani hivi leo hausababishwi na wanadamu. Kazi ya ibilisi ni kuiba, kuchinja na kuharibu. Nasema tena,  shetani hana zawadi za bure!”

Thursday, April 17, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 4



Sura ya 3: Utawala mwovu


Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. (Yohana 10:10) 


Baada ya kurudi Lagos, niliendelea na biashara; na baada ya wiki mbili nilirudi tena baharini. Malkia wa Pwani alinipatia kile aambacho alikiita ni “kazi ya kwanza”. Nilitakiwa kwenda kwenye kijiji changu na kumwua mjomba wangu, ambaye alikuwa ni mganga maarufu wa kienyeji, na ambaye huyu malkia  aliniambia kuwa ndiye aliyehusika kuwaua wazazi wangu.

Saturday, April 12, 2014

Mbinguni, peponi, kuzimu na jehanamu




Mpendwa mmoja aliniuliza maswali yafuatayo ambayo nimeona ni muhimu niyajibu kama Makala fupi kwa ajili hata ya faida ya watu wengine wenye maswali kama haya:


Swali la 1: Hivi watu wakifa, roho zao zinakuwa wapi hasa?
Swali la 2: Roho hizo zinakuwa katika hali gani hasa?

Sunday, April 6, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ay 3




Agano Langu na Alice
Mapema asubuhi moja, Alice aliniambia kuwa kulikuwa na sherehe ya muhimu iliyotakiwa kufanywa kwenye nyumba yake. Saa 8 usiku alileta mtoto mchanga wa kike anayetambaa, akiwa hai. Mbele ya macho yangu, Alice alitumia vidole vyake kunyofoa macho ya mtoto yule! Kilio cha mtoto huyo kiliniumiza sana! Kisha alimkatakata vipande na kumimina damu pamoja na nyama kwenye sinia na kuniambia nile. Nilikataa! Alinitazama moja kwa moja usoni na kile kilichotokea machoni mwake siwezi kukielezea kwa kuandika. Kabla sijajua nini kinaendela, nilijikuta si tu natafuna zile nyama, bali pia nilikuwa nalamba damu. Wakati haya yakiendelea alisema, “Hili ni agano kati yetu. Hautasema chochote kamwe utakachoona nikifanya au chochote kuhusiana na mimi kwa mwanadamu yeyote duniani. Siku utakayovunja agano hili, lako litatoweka.” Alimaanisha kuwa siku nitakayovunja agano hilo, nitauawa!

Monday, March 31, 2014

Niliokolewa Toka kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 2

Sura ya 2: Kuingizwa Kundini

Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, lakini mwisho wake ni njia za mauti.” (Mithali 14:12).


Bali wabaya wanafanana na bahari iliyochafuka; maana haiwezi kutulia, na maji yake hutoa tope na takataka. Hapana amani kwa wabaya; asema Mungu wangu.” (Isaya 57:20-21).

Tuesday, March 25, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza – Sehemu ya 1

Emmanuel Eni alizaliwa nchini Naijeria. Alipitia mateso na dhiki nyingi chini ya vifungo vizito vya ibilisi. Katika ushuhuda huu, anatusimulia kile kilichotokea maishani mwake, mateso aliyopata na hatiamaye jinsi Bwana alivyompa ushindi.

Sunday, March 16, 2014

Mwanafunzi wa Mchawi - Sehemu ya 5


(Waebrania 11:35-40)


Hii ni sehemu ya mwisho ya ushuhuda wa Jim McCoy aliyekuwa mwanafunzi wa mwanamke mchawi kule Marekani, lakini akaokolewa na Bwana Yesu na kutolewa ndani ya vifungo vya mauti.

Monday, March 10, 2014

Mwanafunzi wa Mchawi - Sehemu ya 4


Kuhubiri Injili kwa kila kiumbe na kila mahali


Matibabu ya kisaikolojia (psychotherapy) ni aina nyingine ya mazoezi ambayo yanaonekana ni ya kisayansi kabisa, kama njia ya kuwasaidia watu. Watalamu wengi wa  ‘psychotherapy’ hutumia taaluma hii kuwasaidia watu sababu hasa ya majonzi yao (depression) au kubadili namna ya tabia au mazoea mabaya waliyo nayo. Lakini ni nini hasa kinachoendelea humo? Wanafungua milango ya ndani na kwa kufanya hivyo, wanafungua njia kwa kazi za mapepo. Hii ni pamoja na aina zote za mapumziko ya kisaikolojia (psychological relaxations).

Wednesday, February 26, 2014

Mwanafunzi wa mchawi - Sehemu ya 3




Katika Sehemu ya 1 na ya 2 tuliona jinsi ambavyo Jim McCoy aliingizwa kwenye vifungo vya kipepo na mwanamke mchawi (lakini kwa ridhaa ya McCoy mwenyewe); lakini akajikuta kwenye mateso mengi. Hatimaye Bwana Yesu alimhurumia na kumtoa kwenye vifungo hivyo.

Katika sehemu hii, McCoy anaendelea kueleza mbinu na hila zinazotumika leo duniani; ambazo shetani na maajenti wake wanafanya juhudi za kuzieneza kote duniani ili, sit u watu wanaomkataa Yesu, bali hata Wakristo waweze kunaswa katika mtego na kuishia jehanamu.

Friday, February 21, 2014

Mwanafunzi wa mchawi - Sehemu ya 2


Yale makucha yalijaribu kunizuia tena lakini yakashindwa. Kwa hiyo, niliikamata ile Biblia na kuiweka kifuani pangu. Biblia ilijifunua yenyewe! Nilitaka kuinyanyua hadi kwenye mwanga wa mshumaa ambao nilikuwa tayari nimeshauwasha. Lakini shetani aliuzima ule mshumaa. Kwa hiyo, sasa kulikuwa na giza kabisa kwenye chumba kile. Na hivyo, sikuweza kusoma chochote kutoka kwenye kitabu hicho na sikuona kilichokuwa kimeandikwa kwenye ukurasa ule ambako Biblia ilijifunua yenyewe kimiujiza. Kulikuwa na giza totoro.

Sunday, February 2, 2014

Mwanafunzi wa mchawi - Sehemu ya 1



Jim McCoy alikuwa ni mwanafunzi wa mchawi mkubwa wa Kimarekani. Ufuatao ni ushuhuda wake ambao aliutoa kwenye mkutano kuhusiana na  
New Age, kule Jamhuri ya Cheki kwenye mwaka 1995, miaka michache baada ya kuanguka kwa ukomunisti.
  
Bwana alimwambia, “Nenda kawaambie na wengine kile ambacho nimekutendea wewe, ili kwamba waweze kuamini kuwa ninakuja tena hivi karibuni.”