Sunday, September 29, 2013

Siri Inayohusu Moyo wa Mwanadamu - Sehemu ya 3




Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu,
kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini,
na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia,
na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
(Mwanzo 1:26).


Tazama nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge,
na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu
kitakachowadhuru. (Luka 10:19).

‘Kutawala’ ni kuwa na mamlaka, amri au usemi wa mwisho juu ya jambo au hali. Hii ina maana kwamba chochote kilicho chini ya mamlaka hayo hakiwezi kufanya kilicho juu ya mamlaka hayo iwapo mamlaka yenyewe yamesimama sawasawa.