Friday, November 17, 2017

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 10



==== SIKU YA 19 ====    (Waebrania 10:35-39)
Shin Sung-Kyung: * Shemasi Shin Sung-Kyung alicheza uchezaji wa kiroho
Nilikuwa naomba kwa kunena kwa lugha na mwili wangu ukajisikia kama moto unaowaka. Nje baridi ilikuwa kali sana na ilifikia hadi nyuzi hasi 10 na tulizima mitambo yote ya kupasha joto. Ndani ya kanisa kulikuwa baridi. Lakini Roho Mtakatifu alikuwa juu yetu kiasi kwamba baridi ile kali hata haikutusumbua kwa kuwa Bwana aligeuza miili yetu kuwa kama moto unaowaka. Ilitubidi kuvua makoti yetu mazito ambayo huwa ni kwa ajili ya kipindi cha baridi kali na tukabaki tu nguo za mikono mifupi.

Sunday, November 12, 2017

Kubatizwa kwa moto - 9

 ==== SIKU YA 18 ====      (Petro 5:6-10)
Lee, Haak-Sung: * Kushambulia Mapepo moja kwa moja!
Wakati wa mahubiri ya jioni, mchungaji alituambia, “Mapepo yakija, msiogope bali piganeni nayo uso kwa uso! Mapepo hayo machafu si lolote, kwa hiyo msiyaogope. Ukizama ndani kabisa ya ulimwengu wa roho na kuomba kwa ujasiri, utakutana na upinzani [toka kwa mapepo]. Ikitokea hivyo, likamate na kulichana vipandevipande; liharibu kabisa!” Nikawaza moyoni mwangu, “Tunawezaje kufanya mambo kama hayo kwa mapepo haya yanayotisha kiasi hiki? Mchungaji naye atakuwa anazidisha chumvi mno bwana.”