Tuesday, December 25, 2012

Maisha ya Maonyesho na Ubatili




Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua? 
(Yeremia 17:9).


Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. (Wagalatia 6:4).


Katika somo lililopita nililoliita Nia ya Ndani ya Moyo niligusia kuhusu umuhimu wa kuwa makini na nia zetu pale tunapomwendea Mungu, maana Mungu anajali sana hizo nia ambazo ndizo zinazoamua endapo atayakubali maombi yetu au tutaishia kupata hasara.


Katika somo hili namwomba Mungu anisaidie kufafanua kwa uwazi zaidi kile ambacho hasa kinaweza kuwa kinaendelea ndani ya mioyo yetu, ambacho ndicho anachokiona Mungu wetu pale anapotutazama.

Monday, December 24, 2012

Ushuhuda wa Adelaida Juu ya Mbingu na Kuzimu



Mwanamke mmoja kutoka Bolivia aitwaye Adelaida De Carrillo alipelekwa Mbinguni na Kuzimu na Yesu Kristo. Kule alionyeshwa ni Utakatifu gani anaotakiwa mtu kuwa nao ili aweze kuingia kwenye UFALME WA MUNGU, na pia ni dhambi gani (ambazo wengi wetu tunadhani kuwa ni ndogo), zinaweza kumfanya mtu aingie Jehanamu.

Friday, December 21, 2012

Maswali kwa Maalim Moses na Ndugu Hamudi




Nawashukuru ndugu Hamudi na Maalim Moses kwa majibu na maswali yenu kuhusu makala yangu ya Ndugu Waislamu Nisaidieni. Mimi naamini lengo letu sote ni kumtafuta na kumtii Mungu wetu aliyetuumba, huku tukiwa na imani kuwa, mwisho wa safari ya maisha haya tutafika kwake mbinguni. Hata hivyo, leo ninayo maswali mengine kwao na kwa Waislamu wengine.

Nia ya Ndani ya Moyo




Tunapofanya jambo lolote, mara nyingi huwa tunasukumwa na nia fulani iliyomo ndani yetu. Kwa mfano, mtu anaweza kumpatia mtu mwingine fedha ili:
  •  Kumsaidia katika mahitaji yake,
  • Kujionyesha mbele za watu kwamba yeye ni mwema,
  • Aweze kuja kumwomba jambo fulani, n.k.

Kwa mfano, katika biashara nyingi utakuta makampuni yakitangaza kwamba: Mteja kwetu ni mfalme; Tuko hapa kwa ajili yako; Tunakuthamini na kukujali; Tumekuandalia bidhaa kabambe kwa ajili yako na familia yako, n.k.

Wednesday, December 12, 2012

Majibu ya Maalim Moses - Sehemu ya II







5. Maalim Moses anasema: Quran ni kitabu pekee duniani ambacho muumini anaweza kukihifadhi kwa moyo. Hamlioni hilo?

Jibu langu:
Ndugu yangu Mzizimkavu, hivi kweli unaweza ukaona fahari na ukajisifia suala la KUKARIRI? Hebu nenda katika taasisi yoyote ya elimu duniani (of course, ukiacha elimu ya Uislamu) – kukariri ni jambo linalopigwa vita. Kukariri hakuna faida yoyote! Kukariri kunamfanya mtu asiwe na tofauti yoyote na roboti au kaseti ambazo ukifungulia zinaanza kutoa tu kile kilichoko ndani ingawa zenyewe hata hazielewi kitu.

Sunday, December 9, 2012

Majibu ya Maalim Moses – Sehemu ya I




Katika makala niliyotoa ambayo yana kichwa Ndugu Waislamu Nisaidieni, wapo ndugu zangu Waislamu ambao wamejibu. Mmojawapo ni Maalim Moses – Mzizimkavu. Nakushukuru Maalim Moses kwa yale uliyosema. Basi na mimi nimeona niseme kuhusiana na kile ambacho amekisema Maalim Moses huku nikiamini kuwa huu utakuwa ni mwanzo na mwendelezo wa mjadala wenye manufaa kwetu sote.


Niwie radhi kwa kuwa sikuweza kukujibu mara moja. Hii ni kwa sababu niliibiwa laptop yangu, hivyo nikawa sina uwezo wa kufanya kazi hii. Hata hivyo, namshukuru Bwana wangu Yesu kwa kuwa amenipatia laptop nyingine na sasa naweza kuendelea tena.

Saturday, December 8, 2012

Je, Walikuwa Binadamu Kama Sisi?




Tunasoma katika maandiko juu ya mambo makubwa yaliyofanywa na watu wa nyakati za Biblia. Mambo hayo yalimfurahisha Mungu kiasi kwamba walioyatenda ilibidi Roho Mtakatifu ayaandike kwenye Biblia. Tunapoyasoma mambo hayo tunatiwa changamoto kiasi kwamba wakati mwingine tunajiona labda sisi ni wa hali ya chini sana na huenda Mungu hatufurahii. Mambo hayo ni pamoja na yafuatayo:

Majibu ya Hamudi – Sehemu ya IV



Adamu na Hawa walifukuzwa Edeni


Ndugu Hamudi, nilikuwa nimeahidi kuwa ningetoa jibu la jumla ili kuweza kuweka maisha ya mwanadamu katika picha yake sahihi; na ili tuweze kuona tulikotokea, tuliko na kwa nini tuko hapa; na ni wapi tunaelekea.


Tunaweza kujadiliana na kubishana sana kuhusu suala la Yesu kuwa Mungu au mwanadamu hadi mwisho wa dunia. Lakini jambo moja ni dhahiri – hatuwezi sote tukawa sahihi. Lakini hebu tuangalie uhusiano wa mwanadamu na Mungu kwa ujumla.