Monday, August 26, 2013

Kanisa Litanyakuliwa Wakati Wowote!




Yapo mambo mengi sana ambayo Wakristo tunapishana na kutofautiana katika mitazamo na tafsiri zake kuhusiana na Maandiko. Jambo mojawapo ni kuhusu unyakuo wa Kanisa. Baadhi ya watu husema kuwa  unyakuo utatokea kabla ya dhiki kuu; na wengine wanasema kuwa unyakuo utatokea baada ya dhiki kuu.

Saturday, August 17, 2013

Wachawi Wapigwa Kisha Waumbuliwa Waziwazi na Bwana Yesu!



 
[Picha kutoka mtandaoni. Walioumbuliwa si hawa]

Mungu anatenda kazi. Kazi ya kueneza Injili ya Yesu Kristo si kazi nyepesi kwa sababu ushindani wake hautoki kwa wanadamu bali ni kutoka kwenye falme za giza zinazoongozwa na mapindikizi ya mapepo yanayoongoza majeshi kwa majeshi ya pepo wachafu.

Imeandikwa:
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. (Waefeso 6:12).

Sunday, August 4, 2013

Nilipokuwa Nje ya Mwili Wangu Nilimwona Mungu, na Wafu Walio Hai!





Huu ni ushuhuda wa mtumishi wa Mungu, Dr. Roger Mills, ambaye anaishi North Carolina kule Marekani. Hii ni sehemu tu ya ushuhuda huo ambao ameuandika kwenye kitabu. Lakini nimeona niulete viyo hivyo katika ufupi wake, maana naamini kuwa kuna mambo ya muhimu mengi ya kujifunza katika sehemu hii kwa ajili ya uzima wetu wa milele katika Kristo Yesu.

Tafadhali karibu uendelee kupokea kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo kile ambacho alimfunulia mtumishi wake kwa ajili yangu na yako.