Sunday, April 21, 2013

Yesu ni Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni





Yohana 19:1  Basi ndipo Pilato alipomtwaa Yesu, akampiga mijeledi.

Yohana 19:2  Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika vazi la zambarau.

Yohana 19:3  Wakawa wakimwendea, wakisema, Salamu! Mfalme wa Wayahudi! Wakampiga makofi.

Yohana 19:4  Kisha Pilato akatokea tena nje, akawaambia, Mtu huyu namleta nje kwenu, mpate kufahamu ya kuwa mimi sioni hatia yo yote kwake.

Mwanamke wa Kiislamu Aokoka Baada ya Yesu Kumjia Ndotoni





Katika kukua kwangu, mara zote nilimwona Mungu kama yuko mbali sana. Nilikuwa nikimuogopa sana. Na nilikuwa nikijaribu kumpendeza kwa matendo yangu yote, huku nikijitahidi kubakia safi kulingana na mafundisho niliyopokea, nikiwa kama mwislamu wa kishia.

Nilikuwa nikijitahidi kufanya zile swala 5 kwa siku, huku nikigeukia kwenye Ka’aba, Makka. Pamoja na matendo yangu haya mazuri, nilikuwa sina uhakika ni wapi nitakwenda baada ya maisha haya.

Na tena, kwa sababu ya vita na hali ilivyokuwa nchini, nikiwa nimezaliwa wakati wa mapinduzi na kuona vijana hawa wote waliouawa, nilianza kumhoji Mungu. “Hivi wewe kweli upo ilhali haya yote yanatokea?” Na mara zote mama yangu alikuwa akiniambia, “Nyamaza. Utakwenda motoni. Hutakiwi kumhoji Mungu!”

Je, Mtume Muhammad Yuko Wapi Hivi Leo?




Mungu hutufunulia mambo mbalimbali kupitia watumishi wake mbalimbali anaowachagua ili kutujulisha yale yaliyopo na hata yajayo; yaliyo katika ulimwengu huu na pia ule ujao. Wapo watu wengi ambao Mungu amewatumia kutufahamisha juu ya mbingu na hata juu ya kuzimu.


Bo Ra Choi ni mchungaji kutoka Korea ya Kusini. Mchungaji huyu amekuwa akionyeshwa maono mbalimbali na Mungu kuhusu mambo ya ulimwengu wa roho. Mojawapo ya maono aliyoonyeshwa yanamhusu Muhammad, mtume wa Uislamu.


Je, Muhammad yuko wapi hivi leo? Tafadhali bofya HAPA ili kupata jibu.

Tuesday, April 9, 2013

Kuna Nguvu Katika Mawazo Yetu – Sehemu ya 3




MPANGO WA MUNGU KUHUSU MAWAZO YETU

Bila mimi hamuwezi

Mawazo yetu ni muhimu sana kwa maisha yetu ya sasa na yale yajayo. Kwa hiyo, Mungu anayo mengi ya kusema kuyahusu. Ametuwekea utaratibu na mwongozo wa kuweza kuvuna baraka zake kwa kupitia kwenye mawazo yetu. Hata hivyo ni muhimu kukumbuka wakati wote kuwa msaada wetu unatoka kwa Bwana. (Zaburi 124:8). Pia Yeye anasema: “Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamuwezi kufanya neno lolote.” (Yohana 15:5).

Friday, April 5, 2013

Kuna Nguvu Katika Mawazo Yetu – Sehemu ya 2



Mawazo ni kama sumaku

Sumaku ina nguvu za aina mbili - nguvu ya kuvuta vitu vije kwake na nguvu ya kusukuma vitu viende mbali nayo. Sumaku huvuta au kusukuma vitu vinavyofanana nayo, kwa mfano vipande vya chuma. Haiwezi kuvuta au kusukuma kipande cha mti, maana hakifanani nayo. Mawazo, hali kadhalika, huvuta au kusukuma mambo yanayofanana nayo. Hili ni jambo la kweli kabisa! Kwa mfano, kuna watu wengi ambao utawasikia wakisema, “Najisikia kama nataka kuumwa. Nadhani nitakuwa na malaria.”


Ukiwa na mawazo ya kuumwaumwa, mawazo hayo yatavuta magonjwa na udhaifu vije kwako. Iwapo una mawazo ya kuweza na kufanikiwa, vivyo hivyo, mawazo hayo ni lazima yatavuta mafanikio yaje kwako.

Injili ya Barnaba



Je, umewahi kusikia juu ya ile inayoitwa Injili ya Barnaba? Hii ni injili ya namna gani?

Injili ya Barnaba ni kitabu kikubwa karibu sawa na Injili zote za kwenye Biblia zikichanganywa pamoja. Injili hii inapendwa na kusambazwa sana kwenye ulimwengu wa Kiislamu, wakidai kwamba ndiyo injili sahihi kabisa.

Injili hii inadai kwamba iliandikwa na mmojawapo wa mitume wa Yesu Kristo aliyeitwa Barnaba.

Thursday, April 4, 2013

Kuna Nguvu Katika Mawazo Yetu – Sehemu ya 1



Je, mawazo yana athari au mchango katika uhusiano wetu na Mungu? Je, yanaweza kutumika kuboresha uhusiano huo?

Kila mmoja wetu huwa anawaza mambo mbalimbali kila wakati, maadamu tuko macho. Wakati mwingine huwa tunawaza kwa kuamua na wakati mwingine huonekana kana kwamba mawazo fulani yanavamia tu akili zetu; na kila tukijitahidi kuyaondoa inakuwa ni vigumu.