Je, umewahi kusikia juu ya ile inayoitwa Injili ya
Barnaba? Hii ni injili ya namna gani?
Injili ya Barnaba ni kitabu kikubwa karibu sawa na Injili zote za kwenye Biblia zikichanganywa pamoja. Injili hii inapendwa na kusambazwa sana kwenye ulimwengu wa Kiislamu, wakidai kwamba ndiyo injili sahihi kabisa.
Sababu za injili hii kuwa maarufu kwenye ulimwengu wa Kiislamu ni kwamba injili hii:
- inasema kuwa Yesu si Mungu.
- inasema kuwa Yesu si Masihi.
- inasema kuwa Muhammad ndiye mtume ambaye angekuja siku za mwisho; na kwamba Yesu alisema kuwa hastahili kumlegezea kamba za viatu vyake!
Lakini pamoja na kwamba kwa Mkristo ni suala lililo wazi kabisa kuwa injili hii ni ya uongo, kwa mamilioni ya Waislamu ni kitabu cha muhimu sana kwa kuwa wanadhani kinathibitisha ujio, uhalali na utume wa Muhammad.
Kwa nini basi injili hii ni ya uongo? Tafadhali bofya HAPA ili kupata majibu ya swali hili.
Nimeyapenda masomo yako nimejalibu kutafuta namba yako nimekosa sijui nitaipataje mtumishi
ReplyDeleteHhhhhhh mbona hamujiamini na injili yenu wenyewe
ReplyDeleteHiyo si injili yetu. Ni kanyaboya la muislamu mmoja ambaye hakuwa anajua anachokiandika. Lakini ndio imewateka kwelikweli wa aina yake. Wanaendelea kulishwa matango mwitu.
DeleteMuambiwe nini ninyi ili mumuamini Mtume Muhammad rehma na amani ziwe juu yake na muiamini Quran? Hakika Hapana mola isipokuwa Mungu Mmoja Pekee hajazaa wala hajazaliwa, hana mshirika. Na hakika Muhammad ni mtumwa na mjumbe wa Mungu.
ReplyDeleteNi kweli Abdul, muhammad ni mtume sahihi kabisa wa mungu aitwaye allah mwenye makao yake makuu kwenye kaabah. Hilo hakuna mtu mzima anayeweza kubisha. Suala tu ni kwamba muhammad KAMWE si mtume wa Mungu wa Israeli, mwenye makao yake makuu Yerusalemu.
DeleteMungu akai Kaaba wala Misri kaka angu
DeleteMungu Allah wa Makkah asie jua kiswahili 😂😂
DeleteTusome uislam na ukristo, tuviangalie vitabu hivi na tuwe MAKINI tunayosema. Mfano baadhi wanasema kuwa muislamu ndiye aliyeandika injili ya barnaba na BADO pia inaonyesha kuwa injili ya barnaba iliandikwa hata kabla ya Muhammad, Sasa sisi Kama watu wa kutafuta elimu tuendelee kufanya udadisi juu ya hili kwa maana barnaba alikuwa Ni mmoja ya watu waliokuwa karibu na Yesu, Elimu Ni Jambo la msingi kabla ya Kusema ulichonacho kile ulichosikia kabla ya kukifanyia utafiti.
ReplyDeleteUnajitahidi kuuficha ukweli lakini kweli inadhihiri upende usipende
ReplyDeleteUislamu ni dini ya kweli na haki
ReplyDelete