Friday, July 12, 2013

Ushuhuda wa Rodolfo Acevedo Juu ya Mbinguni, Kuzimu na Hali ya Kanisa la Leo

Ufuatao ni ushuhuda wa Mwinjilisti Rodolfo kutoka Jamuhuri ya Domonika, ambao Bwana alimwonyesha kuhusiana na kuzimu, mbinguni pamoja na mambo yanayoendelea katika Kanisa la siku za leo.


Utangulizi
Mimi ni Mwinjilisti Rodolfo Acevedo Hernandez kutoka Jamuhuri ya Dominika. Koo langu limeathirika kutokana na usimuliaji wa ushuhuda huu lakini bado nitafanya hivyo tena leo hata kama kuna upinzani. Utukufu ni kwa Mungu! Tupo hapa kuhubiri Neno la Bwana Yesu Kristo na ninaenda kutoa ushuhuda ambao ulibadili maisha yangu na maisha ya maelfu kwa maelfu ya watu wengine!!