Friday, September 28, 2012

Ushuhuda wa Victoria Juu ya Kuzimu




Muda Unaisha Haraka!

Huu ni ufupisho wa ushuhuda wa Victoria Nehale
Nilizaliwa na kuishi Namibia maisha yangu yote; na niliyatoa maisha yangu kwa Yesu tarehe 06 Februari 2005. Bwana Yesu Kristo ameshanifunulia mambo mengi katika ulimwengu wa roho ikiwa ni pamoja na safari za kuzimu. Bwana alinipa maelekezo kwamba niwashirikishe watu uzoefu wangu; pia alinionya kuwa nisiongeze wala kupunguza chochote katika vile alivyonionyesha na kuniambia. Wakati nikiandika kitabu hiki, mwishoni mwa 2006, nilishatembelewa mara 33 na Bwana Yesu Kristo. Kila aliponitembelea, Bwana alikuwa akiniambia kabla ya kuondoka: MUDA UNAISHA HARAKA!

Friday, September 21, 2012

Muujiza wa Bwana Yesu Ndani ya Msikiti




Huu ni ushuhuda wa dada mmoja wa kutoka Indonesia ambaye, japokuwa zamani alikuwa Mwislamu (na sasa ni Mkristo), Bwana Yesu alimwokoa kimiujiza yeye pamoja na watu wengine kutoka kwenye janga na mauti ya sunami na tetemeko ambavyo vilisababisha vifo vya mamia kwa mamia ya watu.[Japokuwa video si jambo lenyewe halisi kabisa, lakini imeigizwa kuakisi kile ambacho ndicho kilitokea kabisa].


Je, ni nini kilisababisha hadi Bwana Yesu akaingilia kati wakati ule ambapo kifo kilikuwa hakikwepeki?

Friday, September 14, 2012

Kutoka Kwenye Kundi la Kigaidi Hadi Kwa Yesu





Huu ni ushuhuda wa kweli kabisa kutoka kwa kijana wa Kimisri ambaye Bwana Yesu mwenyewe alimtoa kutoka kwenye uasi na kumfanya kuwa mtu mpya kabisa anayempenda Bwana Yesu pamoja na wanadamu wenzake wote.

Monday, September 3, 2012

Je, Umechoka?



Bwana wetu Yesu alisema wazi: Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. (Mt. 16:24).
Maisha tunayoishi hayaishi mitihani na majaribu mbalimbali. Mitihani hiyo inaweza kuwa inahusu maeneo ya kiafya, kimahusiano, kiuchumi, kiroho, nk.

Kila mwanadamu katika wakati wowote ule, ni lazima anapambana na uhitaji wa namna moja au zaidi. Mtume Petro anatuambia kwamba tumpinge shetani kila wakati kwa imani thabiti: ... mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. (1 Pt 5:9).