Wednesday, February 20, 2013

Manyanyaso na Ukandamizaji Mkubwa wa Wanawake Katika Nchi za Kiislamu




Kati ya mambo ya kusikitisha sana ni jinsi wanawake katika nchi za Kiislamu wanavyonyanyaswa na kukandamizwa. Ni wanadamu ambao Bwana Yesu amewaumba na kuwapa heshima kubwa lakini maskini wamejikuta katika nchi ambazo Mungu anayeabudiwa huko amewapokonya ile heshima na kuwatwika mateso makali ambayo hata ni vigumu kueleza. Mungu huyo amewapa wanaume mamlaka ya kuwafanyia chochote watakacho, lakini bahati mbaya sana, kile wanaume hawa wanachofanya ni masikitiko matupu.

Tuesday, February 19, 2013

Bahasha za Zaka Makanisani Zinatoka Wapi?



Je, ni huduma kwanza au ni roho kwanza?
Wapendwa nawasalimu katika jina la Bwana wetu, Yesu Kristo.

Katika safari yetu ya kiroho tunakutana na mitihani na changamoto mbalimbali ambazo, ama zinatujenga au, kwa bahati mbaya, wakati mwingine zinatubomoa.

Lakini tunapokutana na changamoto kutoka kwa watu wasiomjua Mungu, hilo halitusumbui sana, maana tunajua kuwa kwa hao hilo ni jambo la kawaida. Mtihani mkubwa unakuja pale tunapopambana nazo kutokea kwa wale wanaomjua Mungu, na hasa kama ni vongozi wetu wa kiroho.

Nimekuwa nikijiuliza juu ya suala moja ambalo, nafikiri, limekuwa likifanyika kimazoea zaidi kuliko kimaandiko. Hili ni suala la ulipaji wa zaka.