Monday, July 30, 2012

Bikira Maria wa Fatima



 Picha ya kubuni kuonyesha jinsi Bikira Maria
alivyowatokea watoto watatu kule Fatima

Duniani humu yako mambo yanayoendelea chini kwa chini bila wengi wetu kujua. Wengi tuko kwenye harakati za kuishi na labda hata kustarehe tu bila kujali nini kiko mbele yetu.

Kuna mahali katika ratiba ya nyakati ambako tunaelekea hakika. Ni jambo lililo wazi kabisa kwamba tulikotoka kulikuwa na unafuu mkubwa kuliko tuliko na tunakoelekea. Misingi mikuu ya kijamii kama vile uaminifu, upendo, kuvumiliana, kushirikiana na kusaidiana ilikuwa na nguvu sana huko nyuma kuliko sasa, na kuliko huko mbele tuendako.

Tuesday, July 17, 2012

Je, ni kweli hatutakiwi kuhukumu?


Naamini umeshasikia mara nyingi watu wakisema, “Usinihukumu bwana. Wewe si Mungu.”

Lakini swali ni kuwa, je, dhana hii hutumiwa na watu kwa jinsi ilivyo sawa? Kabla hatujajibu swali hili, hebu tuchunguze maandiko yafuatayo: