Wednesday, February 26, 2014

Mwanafunzi wa mchawi - Sehemu ya 3




Katika Sehemu ya 1 na ya 2 tuliona jinsi ambavyo Jim McCoy aliingizwa kwenye vifungo vya kipepo na mwanamke mchawi (lakini kwa ridhaa ya McCoy mwenyewe); lakini akajikuta kwenye mateso mengi. Hatimaye Bwana Yesu alimhurumia na kumtoa kwenye vifungo hivyo.

Katika sehemu hii, McCoy anaendelea kueleza mbinu na hila zinazotumika leo duniani; ambazo shetani na maajenti wake wanafanya juhudi za kuzieneza kote duniani ili, sit u watu wanaomkataa Yesu, bali hata Wakristo waweze kunaswa katika mtego na kuishia jehanamu.

Friday, February 21, 2014

Mwanafunzi wa mchawi - Sehemu ya 2


Yale makucha yalijaribu kunizuia tena lakini yakashindwa. Kwa hiyo, niliikamata ile Biblia na kuiweka kifuani pangu. Biblia ilijifunua yenyewe! Nilitaka kuinyanyua hadi kwenye mwanga wa mshumaa ambao nilikuwa tayari nimeshauwasha. Lakini shetani aliuzima ule mshumaa. Kwa hiyo, sasa kulikuwa na giza kabisa kwenye chumba kile. Na hivyo, sikuweza kusoma chochote kutoka kwenye kitabu hicho na sikuona kilichokuwa kimeandikwa kwenye ukurasa ule ambako Biblia ilijifunua yenyewe kimiujiza. Kulikuwa na giza totoro.

Sunday, February 2, 2014

Mwanafunzi wa mchawi - Sehemu ya 1



Jim McCoy alikuwa ni mwanafunzi wa mchawi mkubwa wa Kimarekani. Ufuatao ni ushuhuda wake ambao aliutoa kwenye mkutano kuhusiana na  
New Age, kule Jamhuri ya Cheki kwenye mwaka 1995, miaka michache baada ya kuanguka kwa ukomunisti.
  
Bwana alimwambia, “Nenda kawaambie na wengine kile ambacho nimekutendea wewe, ili kwamba waweze kuamini kuwa ninakuja tena hivi karibuni.”