Saturday, May 11, 2013

Siri Inayohusu Moyo wa Mwanadamu - Sehemu ya 2




Mwanadamu alivyoumbwa

Tukisoma Biblia kuhusiana na uumbaji wa mwanadamu, imeandikwa hivi:

Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo 2:7).

Kulingana na andiko hili, tunajifunza yafuatayo:
(a) Mwanadamu ana sehemu kuu mbili.
(b) Sehemu ya kwanza ni mavumbi, yaani mwili unaoonekana 
     kwa  nje na tunaweza kuugusa.
(c) Sehemu ya pili ni pumzi ya uhai ambayo iko ndani na hatuwezi
     kuiona wala kuigusa.
(d) Mavumbi pamoja na pumzi ya uhai yanaunda nafsi hai.

Thursday, May 9, 2013

Siri Inayohusu Moyo wa Mwanadamu – Sehemu ya 1




Mungu anasema mengi sana kuhusiana na moyo. Lakini moyo ni nini? Na umuhimu wa moyo ni nini katika maisha yetu ya kiroho na ya kimwili?

Hebu angalia maandiko machache yafuatayo na uone kile ambacho Bwana anasema kuhusiana na moyo.