Thursday, March 28, 2013

Msamaha! Msamaha!




Kibinadamu ni vigumu na haiwezekani kufanya mambo ya kimungu. Upendo na msamaha ni jambo la kimungu. Lakini mwanadamu yumo ndani ya anguko; ndani ya dhambi. Je, anawezaje kutenda jambo la kimungu?


Bila shaka inahitajika nguvu tofauti na uwezo wetu wa kibinadamu. Sisi ni kama magari ambayo yanahitaji kupitia kituo cha mafuta ili kupewa nguvu ya kufanya safari ndefu. Kwa uwezo wake lenyewe gari haliwezi kufanya hivyo bila nguvu hiyo.

Wednesday, March 27, 2013

Dhambi Isikupeleke Kwenye Hatia Bali Kwenye Msamaha


Karen

Kama ilivyo kwa wanadamu wote, Karen naye alikuwa na dhambi yake imzingayo kwa upesi. Dhambi hiyo ilimfanya ajisikie hatia (ambalo si jambo baya), lakini sasa alijikuta akikwamia humohumo. Matokeo yake akawa na matatizo mawili, kwanza ni hiyo dhambi yenyewe; na pili ni hatia kutokana na dhambi hiyo.

Alijua kuwa Bwana Yesu ni lazima atakuwa ana hasira sana naye. Lakini kwa neema ya Bwana, Karen aliweza kumwona Bwana Yesu. Matarajio yake yote yalibadilika pale alipogundua kuwa, kumbe Bwana hakuja kuuhukumu ulimwengu bali kuuokoa. 

Si tu kwamba dhambi yake iliisha, bali na hatia nayo. Hivi sasa Karen anasema, "Siwezi kuacha kumpenda Yesu!"

Ufuatao ni ushuhuda wake alioupa jina: Nilimwona Yesu.

Thursday, March 21, 2013

Aliyekuwa Ustaadhi na Hakimu wa Mahakama ya Kadhi Akutana na Injili ya Yesu Kristo na Kuokoka – Sehemu ya 1



Ahmed alikuwa ni injinia. Baadaye alishawishiwa na Ulama mmoja na kupandikiziwa chuki dhidi ya Wakristo na Wayahudi kiasi kwamba aliamua kuacha kazi yake na kwenda kusomea masomo ya dini ya Kiislamu (licha ya mama yake kupinga sana).

Masomo hayo yalimwezesha kuwa hakimu wa mahakama ya sharia. Kutokana na ukandamizaji mkubwa aliouona kwenye mahakama hizo na kukosekana kwa haki na pia kukosekana kwa msimamo juu ya tafsiri sahihi ya sheria za kiislamu, moyo wake ulikosa kabisa amani.

Kwa neema za Yesu Kristo, Ahmed alifunguliwa macho yake na sasa anajiuliza ilikuwaje akaamini Uislamu?

Ufuatao ni ushuhuda wake kwa maneno yake mwenyewe ambao ameupa kichwa cha habari: “Njia ya Allah Kuelekea Jehanamu au Njia ya Yesu Kuelekea Mbinguni.”

Tuesday, March 19, 2013

Je, Tuache Kula Nyama Zilizochinjwa na Waislamu?



Kumekuwapo na migogoro hivi karibuni inayohusiana na suala la uchinjaji wa wanyama.

Baadhi ya watu wanaamini kuwa Wakristo tunatakiwa tuache kulala, badala yake tudai serikali itupe uhuru au ‘haki’ ya kuwa na bucha zetu wenyewe. Baadhi ya viongozi wa dini hata walifikia kuwaambia waumini wao (Wakristo) wasinunue nyama kutoka kwenye bucha za Waislamu. Tazama hapa

Sababu mojawapo inayotolewa ni kuwa tunalishwa nyama zilizoombewa dua zisizohusiana na Mungu wetu. Je, tuache sasa kununua nyama kutoka kwenye bucha za Waislamu? Je, tuwe na bucha zetu?

Tuesday, March 5, 2013

Mpiganaji wa Hezbollah Akutana na Yesu na Kuokoka – Sehemu ya I




Afshin Javid alikuwa ni askari wa Hezbollah ambaye aliyatoa maisha yake kikamilifu kwa ajili ya Allah. Katika maisha yake yote, alijifunza kumtii Allah na alikuwa tayari kufanya lolote, ikiwa ni pamoja na kufa kwa ajili ya Allah.


Lakini baada ya kukutana uso kwa uso na Bwana Yesu, kila kitu kilibadilika. Sikiliza ushuhuda wake huu wenye nguvu sana, ambao si  tu kwamba utakutoa machozi, kama yeye mwenyewe anavyoeleza kwa machozi mengi, bali pia utajua jinsi Bwana Yesu alivyo Mungu Mkuu na wa kweli ambaye, kila anayemtafuta kwa moyo wa kweli, anamwona.


Ufuatao ndio ushuhuda wenyewe: