Sunday, April 27, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 5



Kufanywa kuwa ajenti wa shetani

Sikuwa na hisia za kibinadamu wala huruma ndani ya moyo wangu tena. Niliingia kazini mara moja na kuharibu nyumba tano kwa wakati mmoja. Nyumba hizo zilizama ardhini pamoja na wakazi wake wote. Tukio hili lilitokea Lagos  Agosti 1982. Kontrakta aliyejenga nyumba hizo alishikiliwa kwa kosa la kutoweka msingi imara na alilipa faini kubwa sana. Uharibifu mwingi unaotokea duniani hivi leo hausababishwi na wanadamu. Kazi ya ibilisi ni kuiba, kuchinja na kuharibu. Nasema tena,  shetani hana zawadi za bure!”

Thursday, April 17, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 4



Sura ya 3: Utawala mwovu


Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. (Yohana 10:10) 


Baada ya kurudi Lagos, niliendelea na biashara; na baada ya wiki mbili nilirudi tena baharini. Malkia wa Pwani alinipatia kile aambacho alikiita ni “kazi ya kwanza”. Nilitakiwa kwenda kwenye kijiji changu na kumwua mjomba wangu, ambaye alikuwa ni mganga maarufu wa kienyeji, na ambaye huyu malkia  aliniambia kuwa ndiye aliyehusika kuwaua wazazi wangu.

Saturday, April 12, 2014

Mbinguni, peponi, kuzimu na jehanamu




Mpendwa mmoja aliniuliza maswali yafuatayo ambayo nimeona ni muhimu niyajibu kama Makala fupi kwa ajili hata ya faida ya watu wengine wenye maswali kama haya:


Swali la 1: Hivi watu wakifa, roho zao zinakuwa wapi hasa?
Swali la 2: Roho hizo zinakuwa katika hali gani hasa?

Sunday, April 6, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ay 3




Agano Langu na Alice
Mapema asubuhi moja, Alice aliniambia kuwa kulikuwa na sherehe ya muhimu iliyotakiwa kufanywa kwenye nyumba yake. Saa 8 usiku alileta mtoto mchanga wa kike anayetambaa, akiwa hai. Mbele ya macho yangu, Alice alitumia vidole vyake kunyofoa macho ya mtoto yule! Kilio cha mtoto huyo kiliniumiza sana! Kisha alimkatakata vipande na kumimina damu pamoja na nyama kwenye sinia na kuniambia nile. Nilikataa! Alinitazama moja kwa moja usoni na kile kilichotokea machoni mwake siwezi kukielezea kwa kuandika. Kabla sijajua nini kinaendela, nilijikuta si tu natafuna zile nyama, bali pia nilikuwa nalamba damu. Wakati haya yakiendelea alisema, “Hili ni agano kati yetu. Hautasema chochote kamwe utakachoona nikifanya au chochote kuhusiana na mimi kwa mwanadamu yeyote duniani. Siku utakayovunja agano hili, lako litatoweka.” Alimaanisha kuwa siku nitakayovunja agano hilo, nitauawa!