Friday, November 29, 2013

Jiandae kwa Kurudi kwa Bwana! - Sehemu ya 1




Dada Barnarda Fernandez alichukuliwa katika Safari ya Mbinguni mara 2 na Bwana Yesu. Alionyeshwa thawabu za mbinguni zilizoandaliwa kwa ajili ya watakatifu wa Bwana, unyakuo, Karamu Kuu na taji za uzima. Pia aliona hali ya Kanisa, hukumu ijayo na roho zilizopotea zilizoko kuzimu. Ufuatao ndio ushuhuda wake:

Saturday, November 23, 2013

Wakristo walio kwenye giza la nje




Dada Liyan ni mwenyeji wa China. Bwana alisema naye kwa njia ya maono na hata kumpeleka mbinguni na kuzimu. Anayo mafunuo mengi ya muhimu sana ambayo tunayahitaji mno, hasa katika nyakati hizi za mwisho. Tafadhali fuatana naye katika ushuhuda huu muhimu na Bwana atasema na moyo wako kwa namna ya ajabu sana.

Sunday, November 17, 2013

Yesu - nitoe humu kuzimu!



(Hii ni picha tu ya mtandaoni - si ya Linda)


Ndugu msomaji, wako watu wengi sana wanaopita kwenye lindi la huzuni ambazo zimesababishwa na aina ya maisha au familia walimojikuta kiasi kwamba inaonekana kama kila kitu kimekwama. Haijalishi tunapita kwenye hali ngumu kiasi gani. Wito wa Bwana wa mabwana, Yesu Kristo bado uko palepale: Njoni kwangu ninyi nyote wenye kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha (Mt 11:28). Bwana Yesu yuko kazini saa ishirini na nne. Karibu utiwe moyo na ushuhuda huu wa dada ambaye alishakata tamaa kabisa na kuamini kabisa kuwa tayari alikuwa kuzimu. Lakini Yesu anapoingia, kila kitu kinabadilika.