Sunday, May 27, 2018

Kubatizwa kwa moto uwakao - 15





==== SIKU YA 24 ====

Kim Joseph: (2 Timotheo 3:1-5)
Wakati nikiomba kwa kunena kwa lugha, ghafla nilianza kulia machozi ya toba. Nilikuwa nimeshangoja kwa muda mrefu ili kuihisi hasa kwa machozi toba yangu. Mwili wangu ulishakuwa moto. Kwa hiyo, pepo mchafu mwenye umbo la nyoka alipotokea, nilimkamata na kumzungusha hewani.


Lee Yoo Kyung:
Nilipokuwa naomba kwa bidii, pepo ovu baya sana lilitokea huku likipaa juu yangu. Liliruka mbele yangu kwa mbawa zake kama za popo. Lilikuwa na macho kama ya chura, pua nyekundu na ulimi mrefu. Nilikerwa na jinsi lilivyokuwa likinitolea sauti kama ya nyoka. Kwa hiyo, nililikamata na kuchana mabawa yake na nikalitupa hewani. Damu nyekundu ilivuja kutoka kwenye sehemu zake zilizojeruhiwa.

Wakati huohuo, joka baya jeusi lilinijia. Mimi naogopa sana nyoka. Ni viumbe ambao ni wa kuchukiza mno. Aliponikaribia, sikuwa na uwezo wa kufanya chochote zaidi ya kupiga kele, “Bwana! Naogopa! Kuna joka hapa!” Mara moja Yesu alitokea, akalikamata na kulitupa mbali.

Bwana akauliza, “Yoo Kyung, uko vizuri? Usiogope! Hebu twende tukatembelee Mbinguni.” Nilimshika mkono na tukaondoka kwenda Mbinguni. Yesu aliniambia niimbe wimbo wa sifa wakati tukipaa kupita galaksi. Tuliimba, ‘Sifu ee! Moyo wangu!’ mara kadhaa. Baada ya kutembelea mbinguni, tulirudi kwenye Kanisa la Bwana na nikaendelea kuomba.

Yesu akaenda karibu na Mchungaji Kim na akasikiliza kwa makini akiomba. Yesu alisikiliza kwa muda mrefu na akamgusa eneo ambalo mchungaji alikuwa na maumivu. Maumivu yalikuwa kwenye mgongo wake ambako pepo ovu lilimng’ata. Yesu akamkaribia Joseph na kusema kwa sauti, “Tubu zaidi! Zaidi, zaidi, zaidi! Omboleza! Ni pale tu utakapolia ndipo mlango wa Mbinguni utafunguka!” Joseph aliomboleza sana leo. Alikuwa anabubujika machozi ya toba.

Yesu alirudi kwangu na baadhi ya malaika walitokea. Bwana akasema kwa ujasiri, “Yoo Kyung, usiugue; kila wakati uwe na afya. Changamka!” Malaika nao hata wakapiga kelele, “Mtakatifu Yoo Kyung! Usiugue!” Bwana akasema, “Changamka!” Kisha tukaagana.

Lee Haak Sung: *Tabaka la ulinzi lililofanywa na malaika

Wakati ninaomba, malaika wengi walikuja kupitia mlangoni. Malaika wale walinizunguka, huku wakifanyika tabaka la ulinzi. Niliwauliza malaika kile walichokuwa wakikifanya. Wakaniambia kuwa walikuwa wakinizunguka kwa tabaka la ulinzi. Malaika waliponizunguka kwa tabaka la ulinzi, moto mtakatifu uwakao ulinichemsha. Nikaona pepo ovu likiwa limesimama nje ya tabaka la ulinzi. Pepo lile ovu lilikuwa limeshikilia kisu na likanikumbusha kuhusu Chucky toka kwenye sinema za kutisha. Lilimkaribia mmoja wa malaika na kumchoma, lakini mara moja kisu kiliyeyuka na mkono wake ukawaka moto. Niliona pepo jingine ovu lilija. Lilionekana kama mti uliozeeka sana. Wakati lilipokuwa likinijia taratibu, lilitoa mikono yake na kugusa tabaka la ulinzi. Liliwaka moto na mti wote ukawa unateketea. Mti ule ulipiga kelele huku ukikimbia.

Malaika walikuwa wakiweka pia tabaka la ulinzi kumzunguka shemasi Shin, ambaye alikuwa anaomba. Malaika walikuwa takribani 200. Wote walikuwa wanafanya kazi kuweka tabaka la ulinzi kwa washirika wa kanisa. Niliona pepo ovu lililofanana na ‘buff man’ nje tu ya tabaka la ulinzi. Lilikuwa linanijia mimi. Pepo hilo ovu lilijaribu kupenya tabaka la ulinzi, lakini tabaka likawa la moto mno kama moto uwakao. Likakata tamaa ya kuingia. Kisha pepo hilo likamwendea shemasi Shin. Bahati nzuri, alikuwa amefunikwa kwa tabaka la ulinzi na moto. Lilishindwa kupenya kwenye matabaka yake. Pepo hilo likaruka kuelekea kwa mama yangu. Lilipomkaribia mama yangu, liliwaka moto na kutoweka.

Ghafla, mwanga mkubwa unaong’aa ulimulika kutokea Mbinguni. Niliona malaika mkubwa mrefu akija kuelekea kanisani huku amepanda farasi mweupe. Ilikuwa ni hali ya kustaajabisha sana.   Moyo wangu ulikuwa unadunda kwa kasi.  Malaika alikuja kwangu na kujitambulisha, “Habari, Mimi ni Malaika Mkuu Mikaeli.” Malaika mwingine anayeng’aa alikuwa anafuata nyuma ya Mikaeli, aliyeitwa Malaika Mkuu Gabrieli. Gabrieli alishikilia bendera kubwa iliyofungwa kwenye mti wake.  Walinieleza kuwa Malaika mkuu Mikaeli anapoyashinda mapepo, Malaika Mkuu Gabrieli anaiyumbisha bendera ya ushindi upande hadi upande nyuma ya Mikaeli.

Malaika wakuu Mikaeli na Gabrieli walikuwa na urefu karibu sawa. Walisimama kimya wakimwangalia mchungaji akiomba. Nilipotazama jambo hili la kushangaza, niliduwaa kabisa. Ilikuwa vigumu kwangu kutofautisha kama nilikuwa naota au nilikuwa naona jambo halisi.


Kim Joo Eun: * Mapepo mengi yalikuwa yanakuja mbio kwa makundi lakini imani yetu iliongezeka
 Mara ya mwisho nilipoomba, pepo ovu lenye jicho moja na umbo la nusu mwezi lilitokea, likiwa linabiringika kuja kwangu. Pepo lile liliponikaribia, nililichoma jichoni na kuling’oa jicho hilo. Nilizungusha kidole changu ndani ya shimo la jicho. Pepo lililipuka huku damu ikisambaa kote nilipolishambulia. Baada ya muda mfupi, pepo ovu lililojifanya msichana mdogo lilitokea huku likijizungusha kwa kichwa chake kama pia. Nilikamata baadhi ya nywele zake, nikalitikisa, nikalizungusha mara kadhaa, na kulitupa mbali. Yesu alinijia na kunipongeza kwa kitendo changu, akisema, “Madoa (Freckles), kazi nzuri!”
Yesu akaendelea kusema, “Madoa, unaonekana mrembo sana leo! Nani amekusuka nywele zako?” Nikajibu, “Ni shemasi Shin!” Bwana akapongeza, “Kweli eh? Amefanya kazi nzuri sana!” Kwa kuwa shemasi Shin alikuwa bado hajaamshwa kiroho, hakujua kuwa Yesu alikuja karibu yake. Malaika wengi walimsindikiza Yesu. Mara nyingi huwa nawaona malaika wakimsindikiza Yesu lakini safari hii walikuwa wengi zaidi. Miongoni mwa malaika, baadhi yao walikaa wawiliwawili na kukaa karibu na washirika wa kanisa waliokuwa wakiomba. Malaika wale walitumia mikono yao kufunga vyombo vya dhahabu vilivyokuwa na midomo mipana juu na kwa bidii walivijaza kwa maombi ya watakatifu.
Kwa mara nyingine tena, kundi la mapepo wachafu lilitokea kwenye kona ya chumba na kuja kuelekea kwangu. Waliponikaribia, Dada Yoo Kyung aliyakamata, akayazungusha juu, na kuyatupa mbali.  Kaka Haak Sung na Kaka Joseph nao pia walikuwa wakipambana na mapepo wachafu. Waliyakamata mapepo machafu, wakayazungusha juu na kuyatupa kule. Sote tulirudiarudia mbinu hii mara nyingi.

Niliweza kusikia sauti za mapepo wachafu yakijibamiza yanapoanguka ukutani au chini. Kulikuwa na kelele sana. Karibu na mwisho wa kipindi chetu cha maombi, tuligundua kuwa kulikuwa na mashambulizi mengi mbalimbali kwetu. Hata hivyo, kila shambulizi lilisababisha imani yetu kuwa na nguvu zaidi na zaidi.


Dada Baek Bong Nyu: * Mchungaji Kim alisababisha Yesu acheke
Nimeshashuhudia na kuona mambo mengi ya rohoni. Kwa upendeleo huu, pia nimevumilia maumivu mengi. Yesu alinishangaza kwa kunipeleka kwenye bustani ya maua Mbinguni. Aliniruhusu kuwa na muda wa kurejezwa upya kwa kujiburudisha kwenye bustani ile. Niliweza kutumia muda mwingi kwenye bustani ile kadiri nilivyopenda. Kwenye bustani, nilijibiringisha, niliruka na kucheza na malaika kama mtoto. Bustani ya maua ya mbinguni ni kubwa na nzuri kwa namna ambavyo ni vigumu hata kufikiria. Harufu nzuri ya maua ilikuwa ya thamani sana. Nisingekubali hata kupewa dunia yote. Kwa kuwa mwili wangu ulikuwa dhaifu na umechoka, nilipumzika na kujilaza baada ya kuwa nimesharudi kwenye Kanisa la Bwana. Wakati wa ibada ya asubuhi, mchungaji alipokuwa akihubiri, alitembea toka upande mmoja hadi mwingine, huku akifuatwa kwa karibu na Yesu.

Mchungaji wetu ana vichekesho sana kiasi kwamba ninapomfikiria, natabasamu na kucheka papo hapo. Kwa udadisi tu, nilimwuliza mchungaji swali, “Mchungaji, hivi wewe ulikuwa na vichekesho hivi hata kabla sijajiunga na kanisa hili?” Mchungaji akajibu, “Kanisa letu si la zamani sana. Hakuna jambo ambalo naweza kukumbuka ambalo linaweza kuwa la kuchekesha. Sikumbuki jambo lolote ambalo limekuwa la kuchekesha wakati wa kusanyiko letu hili la maombi. Mara zote nilikuwa nimevunjika moyo. Nilijisikia mzito na wa kutia huruma.” Nikauliza, “Kwa nini basi umebadilika kiasi hicho?” Mchungaji akasema, “Hata sijui kwa kweli. Nimebadilika wakati wa maombi haya! Sijui hasa ni nini kinaendelea. Ukiniuliza kwa vipi nimekuwa hivi na ni nani au nini kimenikuta, itanibidi niseme tu ni Bwana ndio ameumba mazingira ya furaha.”

Mchungaji wetu ana kipaji cha kuigiza aina zote za watu. Kimsingi, si watu tu; anaweza kuigiza vitu vya aina zote, ikiwa ni pamoja na wanyama na vitu visivyo na uhai. Yesu alikuwa anamuigiza mchungaji huku akicheka kwa nguvu. Wakati wa ibada, malaika wawili walikuwa wakirekodi kila neno ambalo mchungaji alikuwa akisema. Hata hivyo, mara kadhaa walikuwa wakichungulia kuona mchungaji anavyotumia ishara mbalimbali. Malaika walikuwa wakicheka kwa nguvu kiasi kwamba walikuwa wanapitwa na maneno ya mchungaji. Malaika walipopitwa na maneno ya mchungaji, Yesu aliwakemea. “Msimwangalie mchungaji; nyie andikeni tu kwa bidii!”
Yesu anapotabasamu au kucheka, malaika wote huungana naye katika wakati huo wa furaha. Hata hivyo, Yesu akihuzunika, malaika wanabaki kimya. Katikati ya ibada, mchungaji aliniuliza swali, “Dada, Yesu yuko wapi hivi sasa?” Nikasema, “Amesimama hapohapo nyuma yako.” Mchungaji akakenua na kusema, “Oh, nifanyeje sasa? Nilijamba na kulinuka vibaya sana. Ingekuwa vigumu kwa mtu yeyote kuvumilia. Namhurumia Bwana kama yuko nyuma yangu, ambako atanusa gesi yangu. Nifanyeje sasa?”

Bwana akaongea huku akicheka, “Haina uhusiano wowote kwa kuw amimi ni roho. Ni sawa tu.” Akashikashika kichwa na mgongo wa mchungaji.

Mchungaji Kim Yong Doo: 
Washirika wa kanisa walishamaliza nguvu zao za kimwili karibu zote wakati wakati wa maombi. Badala ya kuacha, waliendelea kwa bidii kuomba kwa kujitoa kabisa huku wameuma meno yao. Bwana alipoona tunaomba kwa kujitoa kiasi hicho, alifurahi. Mimi nilikuwa katika maumivu yasiyovumilika. Maumivu yalisababishwa na mashambulizi ya mara kadhaa ya mapepo wachafu. Aina hii ya majeraha inapona polepole sana. Maumivu yasiyokoma yalinitesa sana. Ikawa vigumu mimi kuomba kwa muda mrefu nikiwa nimeinua mikono yangu. Hata hivyo, katikati ya hayo maumivu, Roho Mtakatifu alisogeza mikono yangu kwa namna mbalimbali. Mijongeo ya mikono yangu iliendeshwa vizuri sana.
Mikono yangu yote ilisogea kwa uthabiti. Iliachiana zamu. Ghafla, mikono yangu ilianza kutetemeka kwa fujo. Nilikuwa na joto kali sana vilevile. Nilimwona Yesu akiwa amevaa joho jeupe akitembea toka upande hadi upande mbele yangu. Uso wangu ulihisi upepo wa vuguvugu wa kipindi cha joto. Nilihisi uwepo wake kwa nguvu. Cha kusikitisha ni kuwa, macho yangu ya rohoni yalikuwa bado hayajafunguka. Inaonekana kana kwamba Bwana anaangalia hali zetu na mwitikio wetu. Alikuwa akitutathmini.

6 comments:

  1. Shalom ndugu,
    Umekaa kimya sana, tafadhali update kubatizwa kwa moto uwakao sehemu zinazofuata,Bwana akutie nguvu.

    ReplyDelete
  2. Ni kweli ndugu nimekaa kimya muda mrefu sana. Mungu mwingi nimekuwa facebook. Amina Bwana anisaidie niendeleze.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Facebook unatumia jina gani, je unajua usipomuamini nabii kacou philippe utaenda jehanamu baada ya kifo chako kama hujui najulisha hapa download app ya nabii Kacou kwa masomo zaidi kwa kiswahili nabiikacouphilippe.blogspot.com

      Delete
  3. Kazi nzuri ndugu ninafrahia sana

    ReplyDelete
  4. Kiongozi mbona umeitelekeza blog?

    ReplyDelete