Sunday, October 9, 2022

NYAKATI HIZI NI MBAYA SANA

Japo injili ya mafanikio haijawahi kuwa na umuhimu wakati wowote, lakini huu HASA si wakati kabisa wa kuhubiri injili za mafanikio.

Dunia tayari inatekwa na waabudu shetani.

Ufunuo 9:15 inasema:
Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu.

Theluthi ya wanadamu kwa leo duniani ni watu wangapi?
Tukiwa tunakaribia watu bilioni 8, theluthi ni watu karibu BILIONI TATU NA NUSU!
Hivi inawezekana watu bilioni 3.5 wakaondoshwa duniani?
Jibu ni NDIO, NDIO, NDIO!
Na tayari mchakato uko kazini hivi sasa usomapo maneno haya.

Tunaishi kwenye kurasa za mwisho za kitabu cha Ufunuo.

Nirudie kusema tena, dunia inatekwa na waabudu shetani.

Ibilisi anaitwa “audanganyaye ulimwengu wote” (Ufu 12:9).

Dunia inazidi kudanganywa kuwa inapewa kinga dhidi ya magonjwa. Wengi wameingia kwenye mtego wa yeye audanganyaye ulimwengu wote.

Wanadai kuwa eti tumekuwa wengi sana kiasi kwamba tunahatarisha dunia!
Yaani kwao ni bora kulinda mazingira kuliko kulinda uhai wa watu. Ni bora kwao wanadamu wapungue ili samaki, miti, fisi na nguruwe waongezeke kuliko kinyume chake.

Dunia inaenda kulazimishwa kumwabudu mungu wake kwa nguvu sana.

Dunia – sasa hivi inapelekwa kuwa kama ifuatavyo:
- serikali moja duniani kote
- kiongozi mkuu mmoja duniani kote
- jeshi moja duniani kote
- dini moja duniani kote
- sarafu moja duniani kote
…………
Heri watumishi wa Mungu wangeachana na kuhubiri mafanikio, wahubiri utakatifu na kutafuta Ufalme wa Mungu KWANZA na sio mafanikio kwanza.

Wakati umeshasonga sana.
Muda wowote Bwana Harusi ataondoa bibi harusi wake. Maneno haya tumeyasikia miaka mingi – lakini hakika, huu ndio muda wenyewe.
……….
Kama una maswali – na hasa kama wewe ni mtumishi unayechunga kanisa – karibu tujadiliane mambo haya kwa undani maana hapa naongea kwa juujuu tu.

Mambo yanayoendelea ni makubwa kuliko nilivyoandika hapa.

Lakini kwa wale wanaompenda Bwana Yesu – tuendelee kuchochea moto mioyoni mwetu. Hata hali iwe mbaya kiasi gani:

Danieli 11:23 inasema wazi:
Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza; lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.
………….
Giza linaifunika dunia lakini Yesu, aliye Jua la Haki, kwake hakuna giza.

No comments:

Post a Comment