Sunday, October 9, 2022

Uumbaji wa kutoka chini

Mungu Baba aliye JUU YA YOTE aliumba kila kitu.

Neno lake linasema: Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, NI CHEMA SANA. (Mwanzo 1:31)

Iwe ni wanyama, ndege, mazao na binadamu – KILA KITU kikawa ni chema sana.

Kuna watu duniani humu wanaomchukia Mungu kuliko unavyoweza kufikiri.
Wamebadilisha mazao karibu yote unayoyajua.
Iwe ni pilipili, tangawizi, mahindi, matikiti, maparachichi, nk.
Yale yanayozalishwa sasa, ukiyatazama kwa macho ni makubwa, na yanazaa sana. Siku hizi utaona maparachichi makubwa kama boga dogo.
Kibiashara utawaza ni faida sana.
Lakini ukweli utabaki palepale – HAKUNA MWANADAMU ALIWAHI AU ATAWAHI KUTENGENEZA KITU KIKAMILIFU KAMA MUNGU BABA – HAKUNA!
Iwe ni zao, mnyama, dawa, au chochote.

Ukitembea popote utaona maua madogomadogo, mengine hayana hata mvuto wa maana – yapoyapo tu. LAKINI Bwana Yesu akasema: … nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo. (Mat 6:29)

Kale kaua kabayakabaya unakokakanyaga kila siku bila kukatilia maanani kameundwa na Mungu Baba kwa ufundi wa hali ya juu (extremely sophisticated) kuliko vazi au pambo lolote lililotengenezwa na mwanadamu duniani!

Neno linasema:
Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, AMBAO MBEGU ZAKE ZIMO NDANI YAKE, juu ya nchi; ikawa hivyo. (Mwanzo 1:11)

Siku hizi kuna matunda na mazao ambayo hayana mbegu ndani yake. Yameshachezewa na mwanadamu. Hata yakiwa na mbegu, ni mbegu tasa. Huwezi kuipanda ikaota. Ukishavuna, inabidi ukanunue mbegu za kileo ili upande tena.

Wameshabadlisha pia wanyama.
Ndiyo maana kuku aitwaye “wa kisasa” anaotaga mayai lakini hayawezi kuangua vifaranga, nk.

Lakini kwa nje utavutiwa kwa sababu unataka pesa – miezi mitatu, umeshavuna na kuuza.

Swali ni kuwa, unadhani wataishia kubadili mimea na wanyama tu? Je, hawana mpango wa kumbadili hata mwanadamu?

Dunia inaongozwa na uongo mkubwamkubwa MWINGI.
Yesu ni KWELI na UZIMA.
Ibilisi – ambaye anaabudiwa na dunia – ni UONGO mtupu na MAUTI.
Yeye ndiye audanganyaye ulimwengu WOTE.
Anatumia umoja wa mataifa kutimiza malengo maovu ya kuharibu uumbaji wa Mungu Baba.
Heri ungeelewa ninasema nini!
Mpokee Yesu uwe salama.

Kama una maswali, uliza ujue zaidi.

No comments:

Post a Comment