Sunday, October 9, 2022

Uumbaji wa kutoka chini

Mungu Baba aliye JUU YA YOTE aliumba kila kitu.

Neno lake linasema: Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, NI CHEMA SANA. (Mwanzo 1:31)

Iwe ni wanyama, ndege, mazao na binadamu – KILA KITU kikawa ni chema sana.

Kuna watu duniani humu wanaomchukia Mungu kuliko unavyoweza kufikiri.
Wamebadilisha mazao karibu yote unayoyajua.
Iwe ni pilipili, tangawizi, mahindi, matikiti, maparachichi, nk.
Yale yanayozalishwa sasa, ukiyatazama kwa macho ni makubwa, na yanazaa sana. Siku hizi utaona maparachichi makubwa kama boga dogo.
Kibiashara utawaza ni faida sana.
Lakini ukweli utabaki palepale – HAKUNA MWANADAMU ALIWAHI AU ATAWAHI KUTENGENEZA KITU KIKAMILIFU KAMA MUNGU BABA – HAKUNA!
Iwe ni zao, mnyama, dawa, au chochote.

Ukitembea popote utaona maua madogomadogo, mengine hayana hata mvuto wa maana – yapoyapo tu. LAKINI Bwana Yesu akasema: … nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo. (Mat 6:29)

Kale kaua kabayakabaya unakokakanyaga kila siku bila kukatilia maanani kameundwa na Mungu Baba kwa ufundi wa hali ya juu (extremely sophisticated) kuliko vazi au pambo lolote lililotengenezwa na mwanadamu duniani!

Neno linasema:
Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, AMBAO MBEGU ZAKE ZIMO NDANI YAKE, juu ya nchi; ikawa hivyo. (Mwanzo 1:11)

Siku hizi kuna matunda na mazao ambayo hayana mbegu ndani yake. Yameshachezewa na mwanadamu. Hata yakiwa na mbegu, ni mbegu tasa. Huwezi kuipanda ikaota. Ukishavuna, inabidi ukanunue mbegu za kileo ili upande tena.

Wameshabadlisha pia wanyama.
Ndiyo maana kuku aitwaye “wa kisasa” anaotaga mayai lakini hayawezi kuangua vifaranga, nk.

Lakini kwa nje utavutiwa kwa sababu unataka pesa – miezi mitatu, umeshavuna na kuuza.

Swali ni kuwa, unadhani wataishia kubadili mimea na wanyama tu? Je, hawana mpango wa kumbadili hata mwanadamu?

Dunia inaongozwa na uongo mkubwamkubwa MWINGI.
Yesu ni KWELI na UZIMA.
Ibilisi – ambaye anaabudiwa na dunia – ni UONGO mtupu na MAUTI.
Yeye ndiye audanganyaye ulimwengu WOTE.
Anatumia umoja wa mataifa kutimiza malengo maovu ya kuharibu uumbaji wa Mungu Baba.
Heri ungeelewa ninasema nini!
Mpokee Yesu uwe salama.

Kama una maswali, uliza ujue zaidi.

1 comment:

  1. Ushuhuda Wangu wa Kutoka Moyoni 💖

    Baada ya baba yangu mdogo kuniacha kwa miezi saba mirefu, nilikuwa nimevunjika moyo kabisa. Alinizuia kwenye mitandao yote ya kijamii, akaondoka, na hakukuwa na njia ya kumfikia. Karibu nikate tamaa, lakini ndani kabisa nilijua singeweza kupata mtu yeyote ambaye angenipenda na kunitendea jinsi alivyonitendea.

    Siku moja, bosi wangu kazini aligundua jinsi nilivyokuwa na huzuni na akanitambulisha kwa Dkt. Dawn. Dkt. Dawn alisikiliza hadithi yangu na akaahidi kwamba mpenzi wangu angerudi kwangu ndani ya siku tatu. Kwa kweli, sikuamini mwanzoni—lakini kwa mshangao wangu mkubwa, siku ya tatu simu yangu iliita. Ilikuwa yeye! Alikuwa akilia na kuomba msamaha, akisema hataniacha tena.

    Tangu siku hiyo, uhusiano wetu umekuwa na nguvu na uzuri zaidi kuliko hapo awali. Amekuwa akipenda na kunijali mimi na mtoto wetu, na sasa tunafunga ndoa katika miezi miwili tu! ❤️

    Shukrani zote kwa Dkt. Dawn, ambaye kwa kweli alifanya jambo lisilowezekana liwezekane. Ninampendekeza kwa moyo wote kwa yeyote anayekabiliwa na changamoto katika:

    Masuala ya uhusiano au ndoa

    Ugonjwa au magonjwa

    Matatizo ya utasa au bahati nasibu

    Kesi za mahakamani au urejeshaji wa mali

    Dkt. Dawn kweli hutatua matatizo kwa ufanisi na hurudisha furaha katika maisha ya watu.

    Wasiliana na Dr. Dawn kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete