Monday, December 11, 2017

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 11


 
==== SIKU YA 20 ==== (Matendo 1:8)
* Kim, Joo-Eun ayashambulia mapepo!
Mchungaji alituambia tusiyaogope mapepo, bali tuyashambulie moja kwa moja. Alisema kwa ujasiri, “Yakanyageni na yapeni uchungu! Ng’oeni macho yao na myapondeponde. Yakamateni na kuyatikisa mahali pote.” Ilikuwa inafurahisha na ilitupa nguvu sana. Kwa kuwa huwa ninaogopa kirahisi, mchungaji aliniambia nisionyeshe kabisa woga vinginevyo mapepo yatashambulia zaidi. Niliamua kuwa imara.