Monday, July 30, 2012

Bikira Maria wa Fatima



 Picha ya kubuni kuonyesha jinsi Bikira Maria
alivyowatokea watoto watatu kule Fatima

Duniani humu yako mambo yanayoendelea chini kwa chini bila wengi wetu kujua. Wengi tuko kwenye harakati za kuishi na labda hata kustarehe tu bila kujali nini kiko mbele yetu.

Kuna mahali katika ratiba ya nyakati ambako tunaelekea hakika. Ni jambo lililo wazi kabisa kwamba tulikotoka kulikuwa na unafuu mkubwa kuliko tuliko na tunakoelekea. Misingi mikuu ya kijamii kama vile uaminifu, upendo, kuvumiliana, kushirikiana na kusaidiana ilikuwa na nguvu sana huko nyuma kuliko sasa, na kuliko huko mbele tuendako.


Ni rahisi tu kusema kwamba hiyo inatokana na ugumu wa maisha katika nyakati hizi. Lakini nikwambia kweli, kuna zaidi ya hapo. Mambo haya yanapangwa katika ulimwengu wa roho na kusimamiwa kikamilifu na viumbe wa rohoni ambao hawamtakii mema mwanadamu.

Na kama huna uwezo wa kustahimili hali ya sasa, nakuhakikishia kabisa huko mbele tuendako ndio kabisa usahau. Hutaweza katu kusimama. Maandiko yanasema:Kwa kuwa wakati huo kutakuwako dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu yeyote; lakini kwa ajili ya wateule, zitafupizwa siku hizo. (Mt. 24:21-22).

Mambo haya, kama nilivyosema, hayazuki tu. Ni mipango iliyoanza miaka na miaka. Inapangwa taratibu kiasi kwamba inazoeleka na kuonekana kama sehemu tu ya kawaida ya maisha. Lakini inakuwa inapanda kiwango kadiri muda unavyoendelea.

Leo ninapenda tuongelee kuhusu maono au jambo ambalo lilitokea mwaka 1916 na 1917 kule Ureno. Haya yalikuwa ni maono ambayo yanaaminika na wengi kuwa yalikuwa yanamhusu Mariamu mama wa Yesu.

Mnamo mwaka 1916 watoto watatu wa kijiji cha Fatima kule Ureno, yaani Lucia dos Santos (miaka 10), Francisco Marto (8) na Jacinta Marto (7) waliokuwa wachunga kondoo, walitokewa na kile ambacho kinaaminika kwa wengine kwamba ni malaika ambaye aliwaambia kuwa yeye ni Malaika wa Amani. Aliwaambia waungane naye kuombea amani; maana hiki kilikuwa ni kipindi cha vita kuu vya kwanza vya dunia. Ilikuwa ni kama maandalizi ya kukutana na Bikira Maria.

 
Watoto Jacinta, Francisco na Lucia 

Tarehe 13 Mei 1917

Tarehe 13 Mei 1917 wakiwa machungani tena, waliona kama mtu akiwa anatoa nuru kali kuliko jua ambaye alikuwa ni mwanamke. Lucia alimwuliza anatoka wapi na anataka nini. Aliwaambia anatoka mbinguni na anataka wawe wanaenda pale  (ilikuwa ni eneo liitwalo Cova da Iria) kwa muda wa miezi sita lakini iwe ni kila tarehe ya 13 ya mwezi katika muda uleule. Kisha alisema kuwa baada ya hapo ndipo atawaambia kusudi lake. Akawaambia wawe wanasali rozari kila siku ili kuleta amani duniani na kumaliza vita.  

Tarehe 13 Juni 1917

Tarehe 13 Juni 1917 walienda tena kwenye eneo lile, na wakati huo kulikuwa na watu takribani 50 hivi pamoja nao. Watoto wale walimwona tena huyo Maria (lakini si wale watu wengine) na akawaambia, “Nataka mje tarehe 13 mwezi ujao na kusali rozari kila siku. Kisha baadaye nitawaambia nitakacho.
Lucia alimwomba awapeleke mbinguni. Maria akasema kuwa angewachukua Jacinta na Francisco baada ya muda mfupi, lakini Lucia angebaki. Ni kweli Jacinta na Francisco walikufa wakiwa watoto lakini Lucia aliendelea kuwapo hadi katika umri mkubwa.

Yule Maria alimwambia Lucia:  Jesus wants to use you to make Me known and loved. He wishes to establish the devotion to My Immaculate Heart throughout the world. I promise salvation to whoever embraces it; these souls will be dear to God, like flowers put by Me to adorn his throne." 

Yaani: “Yesu anataka kukutumia wewe kunifanya mimi nijulikane na kupendwa. Anataka kuanzisha ibada ya moyo wangu safi duniani kote. Naahidi wokovu kwa yeyote atakayekubali; roho hizi zitapendwa na Mungu. Kama maua yaliyowekwa name kupamba kiti chake cha enzi.” 

Tarehe 13 Julai 1917

Tarehe 13 Julai watoto hao walifika tena Cova na kumwona Maria. Lucia akamwuliza anachokitaka. Akawajibu tena: "Nataka mje hapa tarehe 13 mwezi ujao ili kuendelea kusali rozari kila siku kwa heshima ya Mama yetu wa Rozari; ili kuleta amani na mwisho wa vita duniani, maana ni yeye tu ndiye anayeweza kuwasaidia."

Baadaye Maria aliwaonyesha maono ya kuzimu ambako roho nyingi zinateseka. Baada ya hapo, akawaambia kwamba: 

"You have seen hell where the souls of poor sinners go. To save them, God wishes to establish in the world devotion to my Immaculate Heart. If what I say to you is done, many souls will be saved and there will be peace ...”

Yaani: “Mmeona kuzimu zinakoteseka roho za wenye dhambi. Ili kuwaokoa, Mungu anataka kuanzisha duniani ibada kwa moyo wangu safi. Kama mkifanya kile nitakachowaambia, roho nyingi zitaokolewa na kutakuwa na amani ...” 

Tarehe 13 Agosti 1917

Tarehe 13 Agosti ilipokaribia, habari hizi zilishafikia vyombo vya habari ambavyo haviungi mkono mambo ya kidini. Hiyo ilifanya habari hizi zisambae kwa watu wengi sehemu mbalimbali. Asubuhi ya tarehe 13, watoto wale walitekwa na meya wa Vila Nova de Ourem, Arturo Santos. Walihojiwa juu ya siri walizokuwa wanazijua lakini waligoma kabisa kusema. Watekaji walijaribu kiuwahonga fedha na hata kuwatishia kifo, lakini hawakusema kabisa. 

Agosti 19, Lucia, Francisco na Jacinta walikuwa pamoja kwenye eneo linaloitwa Valinhos, karibu na Fatima wakati wa mchana. Walimwona tena Maria ambaye aliwaambia: "Nendeni tena Cova da Iria tarehe 13 na kuendelea kusali rozari kila siku." Maria akasema kuwa angefanya muujiza ili watu waamini, na kama watoto wale wasingekuwa wametekwa, basi huo muujiza ungekuwa mkubwa zaidi. 

Tarehe 13 Septemba 1917

Tarehe 13 Septemba kundi kubwa la watu lilikusanyika Fatima. Mchana hao watoto walifika na waliweza kumwona huyo Maria (lakini si watu wengine).  Alimwambia Lucia: "Endeleeni kusali rozari ili kukomesha vita. Mwezi wa Oktoba Bwana wetu atakuja pamoja na Mama yetu wa huzuni na Mama yetu wa Karmeli (Our Lady of Dolours and Our Lady of Carmel). Mtakatifu Yohana atatokea pamoja na mtoto Yesu ili kuibariki dunia ....” 

Tarehe 13 Oktoba 1917

Tarehe 13 Oktoba 1917 watu wengi sana walikusanyika Cova. Wengi walienda wakiwa hawajavaa viatu huku wakisali rozari kama namna ya kuonyesha unyenyekevu kwa Maria. Mchana watoto wale walimwona Maria. 

Kwa mara nyingine tena Lucia alimwuliza swali lilelile la siku zote: Unataka nini? Akasema: Nataka kukuambia kwamba kanisa lijengwe hapa kwa heshima yangu. Mimi ndimi Mama wa Rozari. Endeleeni kila wakati kusali rozari kila siku. Vita vitakwisha, na askari watarudi hivi karibuni nyumbani kwao.” Baadaye alianza kupaa kwenda juu kuelekea kwenye jua. 

Wakati huo ndipo umati mkubwa wa watu uliweza kuona kile kinachotajwa kama mwujiza. Kwa vile kulikuwa na mawingi, mawingu yale yaliachana na jua likaonekana kama duara jeusi ambalo mtu aliweza kulitazama bila kuumia macho. Mashuhuda wanasema kuwa waliona jua likitetemeka na kuchezacheza na kugeukageuka rangi. Wengine wakasema waliona uso wa Maria, nk. 


Sehemu ya umati wa watu uliojitokeza kuja 
kumshuhudia Bikira Maria  

Kanisa lilikaa kimya kuhusu maono ya Fatima hadi ilipofika Mei 1922 ndipo Askofu Correia alitoa barua ya kichungaji juu ya jambo hili; akisema kwamba angeunda tume ya kuchunguza suala hili. Mwaka 1930 alitoa barua nyingine ambayo, pamoja na mambo mengine, ilisema: 

"In virtue of considerations made known, and others which for reasons of brevity we omit; humbly invoking the Divine Spirit and placing ourselves under the protection of the most Holy Virgin, and after hearing the opinions of our Rev. Advisors in this diocese, we hereby: 
  1. Declare worthy of belief, the visions of the shepherd children in the Cova da Iria, parish of Fatima, in this diocese, from the 13th May to 13th October, 1917. 
  1. Permit officially the cult of Our Lady of Fatima."

Yaani: “Kulingana na masuala ambayo yamewekwa wazi, pamoja na mengine ambayo hatutayataja kwa lengo la kufupisha taarifa hii; huku tukimsihi Roho wa Kiungu na kujiweka chini ya ulinzi wa Bikira Mtakatifu sana, na baada ya kusikiliza maoni ya mapadri Washauri katika jimbo hili: 
  1. Tunatangaza kuwa maono ya watoto wachunga kondoo kule Cova de Iria, parokia ya Fatima, katika jimbo hili, yaliyoanza tarehe 13 Mei hadi tarehe 13 Oktoba 1917 yanastahili kuaminiwa.  
  2. Tunaruhusu rasmi imani ya Mama Yetu wa Fatima.

...............................


Hadi hapa tumeshaona kile hasa kilichotokea kule Fatima. Sasa, yafuatayo ni mambo matano tunayoweza kujiuliza kutokana na hicho tulichokiona:

Moja: Biblia inasema kwamba: Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. (1 Yohana 4:1).

Unawezaje kuijaribu roho? Ona jinsi Paulo anavyosema: Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. (Gal. 1:8).

Maana yake ni kwamba, injili au neno la kweli ni lile linaloendana na kile kilicho kwenye Biblia tu! Hata kama malaika atakuja na jambo ambalo liko kinyume na maandiko, hapaswi kuaminiwa hata kidogo ingawaje yeye ni malaika.

Sasa, Petro anamwongelea Bwana Yesu na jina lake akisema: Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. (Mdo. 4:12).

Lakini hebu angalia huyu ‘bikira Maria’ alivyosema tarehe 13 Julai: "Nataka mje hapa tarehe 13 mwezi ujao ili kuendelea kusali rozari kila siku kwa heshima ya Mama yetu wa Rozari, ili kuleta amani na mwisho wa vita duniani, maana ni yeye tu ndiye anayeweza kuwasaidia."

Je, Mungu anaweza kutoa maagizo yanayojipinga? Je, maneno ya Mungu kupitia Paulo na Petro hapo juu yanamhusu nani? Je, hayamhusu hata huyu ambaye alijiita ni ‘bikira Maria’?

Yanapotokea maneno yanayopingana juu ya jambo lilelile, ni wakati wetu wa kuchambua lipi la kweli na lipi sio; na sio kuyachukua yote mawili kuwa ni kweli. Na ukweli hautokani na maoni na mapenzi yetu, bali unatokana na Neno la Mungu lililo katika Biblia.

Mbili: Vilevile ‘Maria’ anawaambia hao watoto: “Mmeona kuzimu zinakoteseka roho za wenye dhambi. Ili kuwaokoa, Mungu anataka kuanzisha duniani ibada kwa moyo wangu safi. Kama mkifanya kile nitakachowaambia, roho nyingi zitaokolewa na kutakuwa na amani ...” 

Tumeona hapo juu kwamba Maandiko yanasema:  Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. (Mdo. 4:12).

Tangu zamani katika Agano la Kale, inajulikana wazi kwamba msamaha wa dhambi ulifanyika tu baada ya kumwagika damu. Hebu angalia jinsi Mungu anavyowaambia Israeli: 

Kisha mtu awaye yote ... atakayekula damu, ya aina yoyote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu, nami nitamkatilia mabali na watu wake. Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho juu ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa ajili ya nafsi. (Mambo ya Walawi 17:10-11).

Utoaji sadaka ya wanyama ili kumwaga damu kwa ajili ya ondoleo la dhambi yalikuwa ni maandalizi ya ujio wa sadaka kuu na ya mwisho ya Mwanakondoo wa Mungu, Yesu Kristo.

Na maandiko yako wazi kabisa: Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu HAKUNA ondoleo. (Ebr. 9:22).

Wenye dhambi wote sehemu yao ni katika jehanamu ya moto. Dhambi inaondoka kwa njia MOJA TU, nayo ni kwa kusafishwa kwa damu ya Yesu!

Sasa hebu niambie ndugu msomaji, huyu Maria anasema: Mungu anataka kuanzisha duniani ibada kwa moyo wangu safi. Kama mkifanya kile nitakachowaambia, roho nyingi zitaokolewa na kutakuwa na amani ...” Je, roho hii inakubaliana na Maandiko? Kama anachokisema ni kweli, je, Yesu alikufa kwa mateso kiasi hicho ili iwe nini? Je, kifo chake ni batili?

Tatu: Huyu mama Maria akasema: Nataka kukuambia kwamba kanisa lijengwe hapa kwa heshima yangu. 

Bwana Yesu alipofukuza wafanyabiashara katika hekalu alisema maneno haya: Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi. (Mt. 21:13).

Pia akamwambia Petro:  Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. (Mt. 16:18).

Ndugu, kanisa ni kanisa la Kristo Yesu mwenyewe. Hakuna mtu mwingine mwenye mamlaka ya kumiliki kanisa aliloanzisha Kristo. Sasa, ni kwa vipi maneno ya ‘Maria’ hapo juu hayapingani na maneno ya Yesu? Tunawezaje kutekeleza maneno yake bila kupingana na Maandiko?

Nne: Jambo jingine kubwa linalotakiwa kumshtua kabisa mtu ni tarehe ya matukio haya. Ni jambo lililo wazi kwa wasomaji wa Biblia kwamba Mungu hutumia sana namba kwenye maandiko katika kufikisha ujumbe wake mbalimbali. Namba za Mungu zinafahamika, kwa mfano 3, 7 na 12.

Mathalani, tunasoma kuhusu Utatu Mtakatifu wa Mungu, Kristo alifufuka siku ya 3, katika Ufunuo kuna baragumu 7, mapigo 7, mihuri 7, malaika 7, makanisa 7; kabila 12 za Israeli, mitume 12, nk.

Lakini katika namba za Mungu, 13 haipo kabisa! Hebu angalia andiko hili ambalo linaongelea wafalme fulani katika agano la kale: Hawa wote wakakutana panapo bonde la Sidimu, kwenye Bahari ya Chumvi. Miaka kumi na miwili walimtumikia Kedorlaoma, hata mwaka wa kumi na tatu wakaasi. (Mwa. 14:3-4).

Kumi na tatu ni namba ya uasi. Ni namba ya kishetani, sio ya kiungu. Hata hivyo, mstari huu hauwezi kuonyesha kwa wazi sana kuwa hii ni namba ya uasi.

Lakini tunapokuja kwenye maisha ya kawaida, hapo ndipo tunapoona mambo haya kwa uwazi kabisa.

Namba 11, 13 na 33, ni namba zinazoheshimika na kutumika sana na waabudu shetani, kwa mfano freemason na illuminati. Kwa mfano, namba hii inaonekana wazi kwenye muhuri mkuu wa Marekani (the Great Seal of America). Tazama picha hapa chini:


  Muhuri Mkuu wa Marekani

Huu ni muhuri mkuu wa Marekani kwa mbele na nyuma. Ukiangalia upande wa mbele utaona yafuatayo: kuna majani 13, matunda 13, mistari myeupe na myekundu 13 kwenye ngao,  mishale 13, maneno "E Pluribus Unum" yenye herufi 13, nyota 13!

Kwa upande wa nyuma, utaona ngazi za matofali ziko 13,  maneno “Annuit Coeptis” yenye herufi 13.

Lakini swali la haraka atakalojiuliza mtu ni kuwa, je, iweje jambo hili liwe la kiserikali? Ndugu, kuna nchi moja tu hapa duniani iliyoanza na msingi wa kweli wa Mungu aliye hai, yaani Israeli.

Marekani nayo ni nchi ambayo waasisi wake wa mwanzo walianza vema kabisa, lakini baadaye mambo yaliharibika. Nchi nyingi zimeanza na mazindiko na mikataba ya kishetani. Zimewekwa wakfu kwa shetani. Viongozi wake wameingia madarakani kwa msaada wa joka wa zamani, yaani Lusifa.

Wachunguzi mbalimbali walishagundua kuwa muhuri huu ulitengenezwa na watu ambao walikuwa ni freemason, hivyo ukaingizwa serikalini bila wengi kujua. Haya ni maagano ya kishetani ambayo Marekani na watu wake waliingizwa bila wao kujua. Unaweza kusoma zaidi juu ya hili kwa kubofya hapa.

Sasa, tukirudi kwa bikira Maria wa Fatima, bila shaka utaona wazi sasa kwamba kuna jambo ambalo limejificha hapa. Kwa nini asisitize kuwa watoto hao ni lazima waje tarehe 13 na katika muda uleule? Tangu lini Mungu wa mbinguni alitumia namba 13 kwa mambo yake? Ulimwengu Na kwa lugha nyepesi ni kuwa, swala la Fatima halina Mungu aliye hai ndani yake.

Tano: Mwisho nimalizie kwa kuuliza swali kuhusu uamuzi wa kanisa kupitia uamuzi uliofanywa na tume ya Askofu Correia. Kanisa liliamua kuwa ni sahihi kufanya ibada zinazomhusu huyu ‘Maria’ na kwamba jambo hili linastahili kuaminiwa.

Wasomaji wa Biblia wanafahamu kuwa Mungu anasema kuwa tusiongeze wala kupunguza katika Neno lake (Ufunuo 22:19). Sasa je, wewe msomaji, unadhani katika haya kanisa liliongeza au halikuongeza. Kama unadhani halikuongeza, je, unafikiri ni hadi mtu afanye nini ndipo ionekane kuwa ameongeza katika Neno la Mungu?

Rafiki, Yesu anakuita uingie ndani ya safina kabla gharika haijamwagwa. Saa ya wokovu ni sasa. Kama ninavyosema kila mara, usiendekeze dini bila Yesu. Dini zimemwacha Yesu nje na kufundisha mambo yao ya kibinadamu ambayo Bwana anasema: Watu hawa huiheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. (Mt. 15:8-9).

Hatuendi mbinguni kwa sababu tuna dini. Tunaenda mbinguni kwa sababu tuna Yesu kila siku; kila saa; kila wakati. Maana unaweza kujua hata Biblia yote na mbinguni usiende kwa sababu unaweza kujaza maandiko moyoni kichwani lakini usiwe na Yesu. 

Imeandikwa: Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani  kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. (John 5:39).

Karibi kwa Yesu sasa. Acha kuahirisha kuokoka. Acha kuendelea kutumainia dini. Mpate Yesu ndipo na dini itakuwa na maana. Maana ya kusema hivi kuwa, haitoshi tu kusema kwa mdomo kuwa mimi ni Mkristo. Mfanye Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Ni kwa njia hiyo tu ndipo hata utaweza kuogopa kutenda dhambi kwa sababu yake. Lakini kama mtu huwa anatenda dhambi watu wengine wanapokuwa hawamwoni, ina maana kuwa kwake Yesu hana nafasi. Kama akiwa na nafasi kwako, utamwogopa Yeye na si wanadamu. Mungu akubariki.

33 comments:

  1. Hi, i think that i saw you visited my weblog thus i came to
    “return the favor”.I am attempting to find things to enhance my site!
    I suppose its ok to use a few of your ideas!!

    Here is my page; http://www.het-vakantiehuis-frankrijk.nl/duitsland.htm

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hi, thanks for visiting my little blog. Mine is a gospel spreading blog, so the ideas in here can be used completely freely. Be blessed.

      Delete
  2. hata wewe usipotoshe watu, kupanga tarehe ni mipango ya mtu inamana hata hizo tarehe zifutwe kwenye kalenda?? tusiziishi kwa mawazo yako??kanisa linamueshimu Maria kama mama wa mkombozi, ungeijua rozari usingeongea mana ndani yake ni Yesu mwenyewe. mambo yamchukizayo Mungu twayatambua na hatuoni dosari ktk hilo. Tafuta sadaka za watu kwa njia nyingine si kwakupotosha.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Asante ndugu kwa kutembelea blog hii na kuandika kile kilichomo moyoni mwako. Ni kweli tarehe haina shida; na tarehe kama tarehe kusema kweli haifanyi suala la Bikira Maria kuwa dhambi. Vilevile, ni kweli kabisa Mariamu ni mama wa Mkombozi wetu, Yesu Kristo na anastahili kuheshimiwa kabisa.

      Tatizo linapokuja ni pale tunapounganisha kila kitu ndani ya mafundisho yanayomzunguka mama Maria.

      Hivi ni kweli kwa mfano kuwa huyu mama anaweza kutuombea sisi?
      Hivi ni kweli watu sasa hawasamehewi dhambi kwa damu na kifo cha Yesu badala yake wanasamehewa kutokana na kumwomba Maria? Huko si kubatilisha msalaba wa Kristo?

      Kutoona dosari juu ya jambo hakulihalalishi. Haujasikia hata msemo tu wa kawaida kwamba: The path to hell is paved with good intentions?

      Hatuwezi kusimamia mambo kutokana na hisia zetu. Kanisa limejengwa juu ya Neno la Kristo; si vinginevyo. Uthabiti wetu katika imani unatokana na kusimama kwenye kile kilichoandikwa kwenye Biblia?

      Mbona kuna 'makanisa'ambayo yanadai kuwa Yesu si Mungu, na kwamba hakuna mahali panapoitwa jehanamu ya moto. Hakika kabisa na hawa nao hawaoni dosari katika mafundisho haya! Je, kutokuona kwao dosari kunahalalisha imani hii waliyo nayo?

      Kwani ukitaka kuamini utamuuliza yule anayetuhubiria: "Hivi unaona dosari yoyote katika haya unayonihubiria?"

      Au utauliza: "Ni wapi ambako Biblia inasema hayo unayonihubiria?"

      Mimi nitauliza hili swali la pili.

      Mpendwa, mimi sina tatizo na wewe kuwa na msimamo huo kulingana na haya unayoyasema, ila sikukubalii hadi uthibitishe kimaandiko.

      Bwana akubariki.

      Delete
    2. Ulichokiongea ndicho kilichopo, watu hawajui lipi ni neno la Mungu na yepi ni maagizo ya shetani ila kwakuwa dini wamezaliwa wamezikuta hata kama mtu angeambiwa vipi, haweziamini maana kazaliwa kakuta imni ndiyo ipo hivyo na anaona anayemwelekeza jambo tofauti na alivyokaririshwa. Nin.Mungu pekee ndiye atakayewezambadilisha mtu huyu kutokana na fikra potofu alizopewa

      Delete
  3. Sema msemayo,watu wa kizazi hiki mlishaambiwa kuwa hamtaona muujiza isipokuwa wa Yona,mnajidai kuijua kweli ya Mungu wakati dunia ndiyo inazidi kuangamia,Mungu anahitaji wanyenyekevu wapeleke sala kwake dunia ipate kuokolewa, je wako wapi? sana tunaona ushuhuda wa mapepo na watu wa kuzimu,ivyo tunarudi kwa mwanadamu mwenzetu ambaye yeye Mungu mwenyewe alituhakikishia kuwa ni msafi,mbarikiwa na myenyekevu,mama wa Kristu apeleke sala zutu kwa mwanawe ili tupate kuokolewa Mungu anasema "SALA ZA WATAKATIFU NI MANUKATO KWAKE" Nakushauri tuma sala zako kwa mama naye atazifikisha kwa mwanawe wewe na mimi sala zetu hazifiki tunayo MAWAA, Lakini yawezekana wewe mwenzetu ni mkingiwa pia soms Warumi 8:28-30 na pia biblia inasema yeye anayejiona hana dhambi anajidanganya na kweli haipo ndani yake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ndugu mpendwa, muujiza wa Yona unaozungumzwa unahusianaje na bikira Maria kuwa mwmbezi? Nadhani unahusiana zaidi na kufa kwa Yesu na kufufuka kwake - Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo NDIVYO MWANA WA ADAMU ATAKAVYOKUWA SIKU TATU MCHANA NA USIKU KATIKA MOYO WA NCHI. (Mat 12:40)


      Watu walio wasafi si bikira Maria peke yake. Mungu anasema: WATAKATIFU WALIOPO DUNIANI NDIO WALIO BORA, HAO NDIO NILIOPENDEZWA NAO. (Zab 16:3)


      Yako mambo mengi ambayo kanisa Katoliki linafundisha ambayo hayana ukweli wa kibiblia ndugu yangu. Mungu anasema watakatifu wako duniani hapahapa; tena hawa ndio BORA ZAIDI YA WALE WALIOKO MBINGUNI.


      Sasa utasemaje kuwa bikira Maria anasikiwa kwa sababu yeye ni msafi.

      Kwanza NI UONGO MTUPU kusema kwamba: [yeye Mungu mwenyewe alituhakikishia kuwa ni msafi].

      Huu ni uongo wa kanisa Katoliki. Hakuna POPOTE kwenye Biblia Mungu analosema kuwa bikira Maria hakuwa na dhambi; badala yake Biblia inasema:


      “Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, HAKUNA MWENYE HAKI HATA MMOJA. Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. WOTE WAMEPOTOKA, WAMEOZA WOTE PIA; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja. Koo lao ni kaburi wazi, Kwa ndimi zao wametumia hila. Sumu ya fira i chini ya midomo yao. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu. Miguu yao ina mbio kumwaga damu. Uharibifu na mashaka yamo njiani mwao. Wala njia ya amani hawakuijua. (Romans 3:10-17).

      Asiye na dhambi ni MMOJA TU:
      (2Kor 5:21) YEYE ASIYEJUA DHAMBI alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.

      Huyu ni Yesu Kristo.

      Naomba unionyeshe KOKOTE kwenye Biblia ambako kumeandikwa kuwa bikira Maria hakuwa na dhambi ya asili (kama kanisa Katoliki) linavyofundisha – NI UONGO!


      Umeongelea kuhusu Waumi 8:28-30


      Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. (Rm 8:28-30).


      Wala hakuna uhusiano hapa na bikira Maria. Hapa inaongelea kuhusu wote walio katika Kristo Yesu – akiwamo na bikira Maria mwenyewe; ambao wamehesabiwa haki na Mungu KATIKA KRISTO.


      JE, SI KWELI KWAMBA JAPO TUKO DUNIANI SASA, LAKINI PIA TUKO MBINGUNI KAMA TU NDANI YA KRISTO?

      Bwana anasema:


      hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu; ili katika zamani zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa wema wake kwetu sisi katika Kristo Yesu. (Efe 2:5-7).


      Mpendwa wangu, hatuko hapa kushindana na dini yoyote. Bwana Yesu hakuja kuleta dini duniani bali wokovu. Yeyote anayekubali wokovu wake na – awe ni Mkatoliki, Mlutheri, au mwingine – anakubaliwa na Baba wa mbinguni. Lakini kung’ang’ania mafundisho ambayo ni wazi kabisa kwamba NI UONGO na kuona kwamba wale wanaoyapinga kuwa ama WANAJIDAI, WANAJIKWEZA, WANAHUKUMU, WANAJIHESABIA HAKI, n.k. hakumsaidii yeyote.


      Hatutaogopa kusema iliyo kweli kwa kuogopa kwamba tutaitwa majina. Ni lazima INJILI SAHIHI YA YESU ihubiriwe ili watu WAOKOLEWE.


      Mungu akubariki sana.

      Delete
    2. Asante sana nimekuelewa vizuri sana na huko sahihi 100%

      Yesu mwenyewe alisema hakuna jina lingine litupasalo/tulilopewa wanadamu kuokolewa kwalo bali ni jina moja tu ''YESU'' ambalo kila goti litapigwa kuanzia wanadamu mpaka lusifer achilia mbali mapepo yanatetemeka mara wasikiapo jina tu YESU.

      na pia alisema huwezi kufika/kuingia mbinguni bila kupitia kwake. akiwa na maana umkiri umjue na umfuate maana yeye ndiye njia na lango la kukufikisha mbinguni, bila yeye hufiki mbinguni. (kama ni hivyo hapa angekupa na option number 2 kama alijua na mama yake ni njia ya kutufikisha kwake. lazima angesema tu.)

      Maria yeye alikufa kama watu/wanaadamu wengine na aliweka alipopaswa kuwekwa mara baada ya kufa. yeye asikii wala hajui kinachoendela duniani bali ni Yesu. na msaidizi ambaye tumeachiwa atusaidie na kutuongoza kufikia/kufuata ile kweri yaani Roho Mtakatifu.

      Delete
    3. kumbe kwa vile wewe si mkatoliki ndio unaamua kupotosha watu....hivi wewe hapo unamuheshimu mama yako humuheshimu? kwa nini na sisi wenye Adabu tusimuheshimu mama aliyemzaa Mungu?

      kama unamuheshimu mama yako definitely utamuheshimu mama wa Yesu....
      Najua vijana siku hizi mnaona dili kujifunza bible na kuomba watu michango fanya kazi kijana.....Bila bikira Maria usingemjua Emmanuel

      Delete
  4. Acha kupotosha watu. nashangaa watu kung'ang'ana na kanisa katoliki. kuna wapagani wangapi na waislamu ambao hawamjui Yesu Kristo. Watafute hao uongeze sadaka. maana siku hizi dini mmeifanya mtaji eti mmekuwa wajasiriamali kwa kudanganya watu kwa mgongo wa kuokoka wakati matendo yenu ni ya aibu.

    ReplyDelete
  5. Imani bila matendo ni bure. Mmekaa kusengenyana na kusema uongo. kutapanya siri za watu wanaowaamini na kuwaeleza matatizo yao. kutumia vifungu vya biblia kudai sadaka. ni aibu tupu. tuacheni sisi wakatoliki tusali rozali, tuombe kupitia Mama Maria. Yawauma nini nyie? Kwamba nyie mliookoka mtaenda mbinguni? jidanganyeni sana. Imani bila matendo ni bure.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Yesu ndo njia ya kweli, wala sio bikira maria

      Delete
  6. Inaonyesha ulivyo na ufinyu wa mawazo

    ReplyDelete
  7. wele wote unaowaona katika madhehebu mengine hpo mwanzo walikuwa wakatoliki, baada ya kuijua kweli ukatoliki hauna nafasi kwao tena, kuhesabu rozali, kuombewa na wafu,kutubu kwa padre,kukariri sala ndefu zilizotungwa na wazungu, kufuata liturgia,misa,sacramenti saba, upapa badala ya roho mt. wanaoweza kuijua vizuri ukatoliki na katoliki ni waliokuwemo wakatoka si wewe uliyemo ndani.

    ReplyDelete
    Replies
    1. amen. mimi pia mmojawapo wa waliokuwa wakatoliki. ubatizo, komunio na kipaimara vyote nilipata.

      Delete
    2. kwa akili za kushikiwa ukatoka....umepotea sana
      haya unapa shilingi ngapi kwa siku kwa kujifanya na wewe unakanisa,,,,,,eti mama Maria aruhusiwi kuwa na kanis alke mbona gwajima analo na kila siku unaenda kuhesabu nae sadaka

      Delete
    3. Inaoneka wazi wewe ni Muislamu usipotoshe Jamii hasa wakristu....Je yesu aliposema yeyote mtakao waondolea dhambi wameondolewa na mtakao wafungia wamefungiwa hata mbinguni aliwaambia akina nani? alimaanisha nini? somo hilo linawahusu nani? "wewe ni mtumwa wa shetani"

      Delete
  8. Duh!!!!!!!!!!!!!!!!! Barikiwa Mtumishi James

    ReplyDelete
  9. hicho usemacho ni kweli kabisa mungu alinifanyia muujiza kwa namba 12 akutie nguvu sana Ndugu kwa huduma yako inasaidia wengi

    ReplyDelete
  10. KWELI KABISA NDUGU ZANGU WAKATOLIKI HIKI KINACHOELEZWA NI KWELI KABISA KUMBUKENI MTUME PAUL ALISEMA HATA MALAIKA WA GIZA WATAJIGEUZA KUWA MALAIKA WA NURU ILI KUPOTOSHA UKWELI 2WAKORINTHO 11:14 BIKIRA MARIA HANA SEHEMU YOYOTE KUHUSU WOKOVU WA MWANADAMU YESU ANASEMA MIMI NDIYO NJIA KWELI NA UZIMA MTU HAJI KWA BA ILA KWA NJIA YA MIMI Yoh. 14:6

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe na James ambae ni msadukayo ni mmoja wa wasiojua dini unafata mkumbo..unajua maandiko matakatifu ? Ufunuo 12:1 unaijua? Muujiza wa kwanza wa Yesu alifanya kwa kuambia na nani?....Yesu wakati anakufa msalabani unajua alimwambia nini Mama yake...na alimwambia nini Yohane? Jifunze biblia utaishia kuwa body guard wa wachungaji wenu feki

      Delete
  11. Katika ulimwengu wa leo kuna njia nyingi za kutumaini. Furaha ya milele na Mbinguni vina hubiriwa kila mahali. Hata hivyo kuna dini nyingi tofauti, filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo (furaha ya milele) vinatofautiana. Na kila mmoja katika tofauti hizo za dini na filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo; anaamini ya kuwa amesimama katika ukweli.
    Na maisha ya mwanadamu yamefikia mawazo ya hali ya juu. Wengi wetu wanapenda kuishi katika dunia hii kwa muda mrefu iwezekanavyo. Baadhi yao wanategemeo la kuishi milele katika dunia hii.
    Lakini kuna njia moja tu ya kumuingiza mtu katika furaha ya kweli ya milele. Kuna ukweli mmoja tu, umfanyao mtu kuwa huru. Kuna namna moja ya maisha itakayomfikisha mtu katika uzima wa milele. Yesu Kristo Mwana wa Mungu, ndiyo “Njia, na Kweli na Uzima.” Kumbuka Yesu mwenyewe alisema, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima; mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya Mimi,” Yoh. 14:6.
    Na Yesu Kristo ni “Njia na Kweli na Uzima.” Kwa sababu Yeye alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. Wote wametenda dhambi kwa kuiasi Sheria ya Mungu (Rum 3:23; 1 Yoh 3:4). “Na mshahara wa dhambi ni mauti,” Rum 6:23. Hii ndiyo mauti ya pili au Jehanamu (Ufu. 21:8; Mat. 10:28). Kwa sababu ya dhambi zetu tulistahili adhabu ya milele katika Jehanamu, lakini kwa sababu ya upendo mkuu wa Mungu na rehema zake alimtoa mwanawe Yesu Kristo akafa msalabani akalipa deni letu la dhambi zetu (Yoh. 3:16-17; Rum. 5:5-10; 6:17-23). Yesu ni “Njia na Kweli na Uzima.” Kwa sababu Yeye alifufuka kutoka kaburini. Kabla hajaja Yesu Kristo, kaburi la giza la mauti lilikuwa likitungojea mwisho wa safari yetu pasipo tumaini. Lakini Yesu alishinda kifo akafufuka toka kaburini. Yesu alishinda mauti. Yeye atatupa ushindi juu ya mauti wale tunaompokea na kumtii (1 Kor 15:2023; Ufu. 1:17-18). Yesu alisema, “Mimi ndimi huo ufufuo na uzima: yeye aniaminie mimi, ajapokufa atakuwa anaishi,” Yoh 11:25.
    Yesu ni “Njia, Ukweli na Uzima,” kwa sababu Yeye atawahukumu watu wote siku ya mwisho (Mdo. 17:30-31). Kila mtu atasimama mbele ya Yesu Kristo na atatoa hesabu ya matendo yake aliyoyafanya wakati wa maisha ya hapa duniani. Mtume Paulo kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu aliandika hivi: “Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda kwamba ni mema au mabaya,” 2 Kor. 5:10.
    Yesu ndiye njia pekee ya kwenda mbinguni. Yesu peke yake ndiye kweli. Hakuna atakayepata uzima wa milele isipokuwa kwa njia ya Yesu Kristo. Ili mtu apokee baraka zitolewazo na yesu mwenyewe, ni sharti awe amuamini Yesu kuwa ni Mwana wa Mungu
    aliye hai. Kumbuka Yesu alisema “....Msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu,” Yoh. 8:24. Pia inampasa kutubia dhambi zake, Yesu alisema nawaambia; “Sivyo msipotubu ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo,” Lk. 13:3. Mtu hawezi kupokea baraka zitolewazo na Yesu Kristo iwapo atamuonea haya. Maana Yesu alisema,
    “Yeye atakayenikiri mbele za watu nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye Mbinguni, bali mtu yeyote atakayenikana mbele ya watu nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye Mbinguni,” Mat. 10:32-33. Pia inampasa mtu abatizwe katika kristo ili apokee msamaha wa dhambi na baraka. Kumbuka Yesu alisema, “Aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiye amini atahukumiwa,” Marko 16:16.
    Yesu Kristo Mwana wa Mungu hakika ndiye, “Njia na Kweli na Uzima.” Hakuna atakaye okoka isipokuwa kwa njia ya Yesu Kristo. Kama ukimwamini Yesu leo na kumtii ujue ya kuwa furaha na amani na uzima vita kuwa vyako; sio katika ulimwengu huu tu, bali na katika ulimwengu ule ujao.
    SIYO MALAIKA WATAKATIFU WALA BIKIRA MARIA!!!

    ReplyDelete
  12. Nilitaka kukwambia kuwa ukisemacho kinauzito sababu sisi ni wanadamu na hatujakamilika sababu biblia ni ngoa na upanga una waza ni ambia maana ya neno hilo katika biblia ukitaka kuonana na baba yangu pitia kwanza kwangu na ukitaka kuniona pitia kwa baba yangu

    ReplyDelete
  13. Nilitaka kukwambia kuwa ukisemacho kinauzito sababu sisi ni wanadamu na hatujakamilika sababu biblia ni ngoa na upanga una waza ni ambia maana ya neno hilo katika biblia ukitaka kuonana na baba yangu pitia kwanza kwangu na ukitaka kuniona pitia kwa baba yangu

    ReplyDelete
  14. YESU NI ALFA NA OMEGA [Ufunuo1:8,Ufunuo1:17 ISAYA 41:4]

    ReplyDelete
  15. YESU NI ALFA NA OMEGA [Ufunuo1:8,Ufunuo1:17 ISAYA 41:4]

    ReplyDelete
  16. usipotubu utahangamia na hapa hapa Duniani utapata bakora zako kwa kumzarau mama wa Mungu....rubbish

    ReplyDelete
  17. wewe ni mmoja wa wapinga kriso.chuki za kidini zimekufanya utumie akiri nyingi na vifungu vya biblia kumpinga mama wa Mungu.kumbuka shetani pia alitumia biblia kumshawishi Yesu amsikilize.Dunia nzima inajua kuwa Bikira Maria aliwatokea hao watoto.shahidi wa kwanza ni sista lucia mwenyewe aliyekufa waka 97.tafiti zimefanywa kwa miaka zaidi ya 100 na utabiri wa kupigwa risasi papa mwaka 81 aliutoa mama,na mama mwenyewe ndiye alimwinua papa.angalieni nyie wapinga kristo shetani anajitukuza ndani mwenu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Unaweza kujadili kwa kutumia maandiko? Kama ni kutokewa tu na viumbe, wapo waliotokewa na viumbe mapangoni na leo wana wafuasi mamilioni. Ongea kwa kutumia maandiko.

      Delete