Sunday, June 22, 2014

Niliokolewa Toka Kwenye Nguvu za Giza - Sehemu ya 9




Sura ya 7: Kazi za Maajenti wa Shetani

Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” (Eph 6:11-12). 

Kitabu hiki hakitakuwa kimekamilika iwapo hakitaweka wazi mbinu mbalimbali za utendaji kazi za hizi nguvu za giza. Pia ni muhimu kwamba namna mbalimbali za kujidhihirisha kwao nazo ziwekwe wazi.


Jambo moja ni dhahiri nalo ni, ibilisi ama atakufanya uamini kuwa yeye hayupo au kwamba shetani ni mawazo tu mabaya; au atakufanya uone zaidi nguvu zake kuliko nguvu za Mungu. Wakati Biblia inasema: kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho,” Biblia hiyohiyo pia inasema kuwa silaha za Mkristo dhidi ya ibilisi na maajenti wake si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo (2 Kor 10:4-5). Vilevile Maandiko yanasema wazi: “Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za ibilisi.” (1Yoh 3:8) 


Na Yesu alizivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo. (Kol 2:15). 


Maandiko yanasema,Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako.” Kwa hiyo, mwana wa Mungu ni lazima uwe mwangalifu kukiri Neno la Mungu, ambalo Mungu alishaahidi kuwa atalitimiza haraka. Kuna ukiri wa aina tatu uliotajwa kwenye Neno la Mungu:

1. kukiri kuwa Kristo Yesu ni Bwana.
2. Kukiri imani katika Neno, katika Kristo na katika Mungu Baba.
3. Kukiri dhambi.


Tunaposikia neno “kukiri,” ni rahisi kuwazia dhambi. Maana ya kukiri kwenye kamusi ni:
1. Kukiri kile tunachoamini.
2. Kushuhudia kile tunachokijua.
3. Kuwa shahidi wa kile tulichokipokea.


Kwa hiyo, inasikitisha kwamba kila tunapotumia neno ‘kukiri’ mawazo mengine hukimbilia kwenye dhambi. Hapa mwandishi anamtia moyo mwana wa Mungu kuanza kukiri kile ambacho Mungu amesema. Wewe ambaye ulikuwa umekufa kutokana na dhambi zako Mungu alikufufua pamoja na Kristo na kukuketisha juu sana kuliko ufalme uwao wote katika Kristo Yesu. Kwa hiyo, Wakristo wanatakiwa watambue mahali kule walikoketishwa. Ni lazima wajue kuwa wanatenda kazi kutokea kule juu sana; juu ya shetani na maajenti wake. Bwana Yesu amewapa nguvu na mamlaka yote kama ambavyo amewapa kila kitu kinachohusiana na uzima na ucha Mungu. (2Petro 1:3). Mungu hakupanga kwamba mazingira yawatawale watoto wake, bali Neno la Mungu kwenye kinywa cha Mkristo ndilo liyatawale mazingira na matukio. Mungu ameongea kwenye Yer 23:29 akisema:Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?


Wakristo, yaani waliookoka, ni lazima watambue kuwa, Jina la Yesu linapotamkwa, kinachotoka kwenye vinywa vyao ni moto. Mkristo anaposimama kwenye mamlaka aliyopewa na Kristo na akatoa amri kwa Jina la Yesu, moto unabubujika toka kinywani mwake na pepo yeyote anayetawala matukio na mazingira ni lazima atii! Yesu yuko hai leo ili kuhakikisha kuwa kila Neno lake linatimia. Napenda pia kusisitiza jambo ambalo Wakristo wengi hawalizingatii, lakini ambalo shetani analitumia. Pale Petro alipomwonyesha Yesu mtini ulionyauka kwa kuwa aliulaani, Bwana alisema:


(Kulingana na Mathayo) Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka. Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea. (Mat 21:21-22). 


(Kulingana na Marko) Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. (Mark 11:22-23).

Bwana anatuonyesha nguvu ya maneno na pia anamtia moyo Mkristo kusema kitu maalum wakati akiwa anaomba na katika kutumia mamlaka yake. Baadhi ya Wakristo huuambia mlima ung’oke lakini hawauambii uende wapi. Yesu alisema kuwa ukiuambia mlima, “Ng'oka ukatupwe baharini …” Hebu tuchukue mfano wa kutoa mapepo. Baadhi ya Wakristo huyafunga na kuyafukuza mapepo bila ya kuyaambia yaende wapi. Hii ni hatari. Unapolifunga pepo, linafungika. Kama ukilitoa bila kulipeleka mahali maalum litabakia hapo karibukaribu. Kama pepo likikemewa tu litoke kwa mtu, linaweza baadaye kurudi na kumwingia yeyote asiye Mkristo. Kwa hiyo, Wakristo wanatakiwa kuwa waangalifu wanaposhughulika na mapepo. Hakikisha kuwa pepo limefungwa, limetolewa na limepelekwa sehemu maalum (na limepigwa marufuku kurudi kumwingia mtu tena).  

Baadhi ya Wakristo wanapoomba husema, “Nakuteka ewe pepo kwa Jina la Yesu.” Kwenye ulimwengu wa roho, hapo unaliona kabisa pepo likiwa limesimama likisubiri amri inayofuata. Lakini kama Mkristo akiishia tu hapo, anakuwa hajamsaidia yule mwenye shida. Usichezecheze na ibilisi. Hauwezi kuchezacheza mbele za adui yako. Mungu amekutuma kwenye huduma ya kuwafungua watu na ya upatanisho (kuwapatanisha watu na Mungu). Kwa hiyo, ni lazima uwe mwangalifu kutenda kazi iliyokamilika. Narudia tena: unapomfunga pepo, anafungwa.  Unapomtoa na kuamuru aende mahali fulani, anatoka na kwenda huko. Maadamu tu kama huchezi na dhambi bali unaishi ndani ya mapenzi ya Mungu, amri yoyote utakayotoa kwa ibilisi au maajenti wake kwa Jina la Yesu, ni lazima waitii! Mungu ameahidi kulitimiza kila Neno lake.


Tunapokuwa sasa tunaelekea kwenye hatua ya pili, yaani udhihirisho wa shetani na maajenti wake, napenda uweke aya zifuatazo moyoni mwako:

1. “Na ninyi mmetimilika katika yeye aliye kichwa cha enzi yote na mamlaka.” (Kol 2:10). 

2.
Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.” (Luk 10:19).
 
3.
Tazama, yamkini watakusanyana; lakini si kwa shauri langu. Watu wo wote watakaokusanyana juu yako wataanguka kwa ajili yako…. Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana.” (Isa 54:15, 17). 

Napenda nikuonyeshe kwenye kitabu hiki kwamba nguvu hizi za giza zinafanya kazi zaidi makanisani, masokoni, makaburini, mahotelini, maporini, baharini na angani.

Makanisani

Sisi ni mashahidi leo kwamba kuna watu wengi waliopagawa na mapepo makanisani. Wengine hata hunena kwa lugha au kutoa unabii. Ni wale tu walio na Roho wa Mungu wanaweza kuwatambua watu hawa. Lakini tuko hapa kuwajadili maajenti wa shetani walioko makanisani. Hatuko hapa kujadili wanachama wa vyama vya siri vya kishetani walioko makanisani (ambao baadhi yao hata ni viongozi wa Kanisa) – hao tunajua wapo. Ninaoongelea ni wale wanaokuja kama maajenti wa shetani:

1. Kusababisha ugomvi na mivurugano makanisani.
2. Kutawanya makanisa.
3. Kuwafanya watu wasinzie wakati ibada inaendelea.
4. Kusababisha mambo mbalimbali yanayoondoa usikivu wakati wa ibada.
5. Kuwaleta watu kwa shetani.


Kwa kuwa nilishasema mambo kadhaa kuhusiana na mambo haya kwenye sura ya tatu, nitawapa tu ushuhuda wa kile ambacho kilitokea si muda mrefu uliopita. Wakristo wanatakiwa kutii kila Neno la Bwana Yesu Kristo kwa sababu, wasipotii wanakuwa kwenye hatari ya kuanguka pale shetani au maajenti wake wanapoweka kikwazo kidogo tu mbele yao. Wakristo wameitwa watoke gizani ili waje kwenye nuru ya ajabu ya Mungu mwenyewe. Wakristo wameitwa ili kujitenga kabisa na dunia na yale yaliyo ya dunia. Maandiko yanasema,Tokeni kati yao, Mkatengwe nao,” (2 Kor. 6:17).

Alikuwapo huyu dada mmoja, dada J (sitataja jina lake). Alikuwa ameokoka na akawa mshirika kamili wa Kanisa moja lililo hai. Baadaye alihamishia ushiriki wake kwenye dhehebu langu. Alishiriki katika kazi zote za Kanisa na alikuwa na bidii sana. Lakini tabia yake ilianza kutia mashaka wakati fulani. Kwa hiyo, wachache wetu tuliamua kwenda kumtembelea nyumbani kwake ili kujua kilichokuwa kinamsumbua. Wakati tukimhoji, mapepo yalilipuka ndani yake na kuanza kutuambia kuwa alikuwa ni ajenti wao kwenye Kanisa letu. Mapepo haya yalitolewa ndani yake na akafanyiwa huduma ya kufunguliwa.

Tulimwuliza, “Dada, inakuwaje wewe ni mshirika wa Kanisa la kiroho na bado ukawa ajenti wa shetani?” Alituambia yafuatayo: Haya yalianza siku moja baada ya ibada ya Jumapili. Dada mmoja (ambaye alidhani alikuwa akimwamini Kristo), alimwendea na kuomba kuwa karibu naye kwa sababu, alidai kuwa alivutiwa na maisha ya Kikristo ya dada J. Dada J alikubali kuwa rafiki yake bila kuwa wasiwasi. Wote walienda nyumbani kwa dada J na huyo aliyeomba urafiki alileta ndizi na karanga, ambazo wote wawili walizila. Alikaa na dada J kwa muda kisha akaondoka.


Akawa akija mara kwa mara kumtembelea dada J huku akimletea zawadi mbalimbali. Zawadi hizo ni pamoja na magauni, viatu, fedha, n.k. Wakati mwingine huyo rafiki wa dada J alikuwa akija na wasichana wengine wengi. Haya yaliendelea kwa muda na yule dada alipoona amefanikiwa kuzima nuru ya Kristo ndani ya dada J, alibadili mbinu na kuanza kumtembelea dada J kiroho. Hapo dada J alipewa nguo nyekundu, jiwe la kwenye maji, pete kwa ajili ya kidole gumba cha mguu wa kulia na mkufu wa kuvaa mguuni. Kwa kuwa dada J alishakula sana nao na alishapokea zawadi zao nyingi sana, hakukuwa na njia ya kukataa. Aliingia agano nao na akaanza kuhudhuria mikutano yao. Alikuwa sasa anaweza kujigeuza nyoka, popo, n.k. Ndipo akawa ajenti wao kwa lengo la kuvuna roho kwa ajili yao kutoka Kanisani.

Mungu asifiwe kwa kuwa sasa ameshafunguliwa! Zawadi zote alizokuwa amepewa ziliharibiwa na sasa ana furaha tena katka Bwana. Mpendwa msomaji, hii yote ilianza na urafiki usio wa kawaida, na kwa kuwa dada J hakuwa na karama ya kupambanua roho, na hakuwa macho kama Bwana anavyotuagiza, yaani “Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, ” (Marko 14:38), dada huyu alipotoka na kuangukia mikononi kabisa mwa adui; na mbio zake zingeweza kuishia kuzimu kwa sababu ya uzembe.


Unaweza kuwatambua maajenti wa shetani kirahisi kutokana na mambo yafuatayo:

- wanavaa pete kwenye moja ya vidole vyao gumba, mkufu kwenye mguu, pete ya puani, bangili za ajabuajabu, n.k.

- wanaingia Kanisani au kwenye feloshipu na kuwa na bidii sana katika shughuli za kikundi au Kanisa, kwa ajili ya Mkristo mmoja tu ambaye wanamfuatilia. Baadhi huwa na tabia zisizo za kawaida na wengine ni waovu, n.k.

Ndiyo maana mwana wa Mungu anatakiwa kumwomba Mungu ampe karama ya kupambanua roho, ili aweze kuwatambua mara anapowaona. Mara wanapogundua kuwa umewajua, wanahakikisha hauji karibu yao. Sababu ni kuwa mkubwa wao atawaonya kuhusiana na wewe!

Masokoni

Maajenti hawa wanatenda kazi kwa njia mbalimbali masokoni. Sokoni ni eneo lao mojawapo kubwa la kufanyia kazi, kama ambavyo kwenye mahoteli ni eneo wanakosubiria wanaume. Sokoni, ndiko wanakonasia mawindo yao,  baadhi ya wanawake wajawazito ambao huwasababishia mimba zao kuharibika ili waweze kupata damu kwa ajili ya akiba zao za damu. Baadhi ya watu, maajenti hawa huwasindikiza hadi kwenye nyumba zao ili waweze kwenda huko usiku. Hii hutokea kwa wasio waamini! Baadhi ya vitu vya kuvutia vinavyouzwa sokoni, kama vile mikufu, rangi za midomo, marashi na vyakula kama dagaa aina ya “Queen of the Coast” n.k., vina asili za ajabu.

Kuna vitendo fulanifulani ambavyo Wakristo wanatakiwa kuwa makini navyo, maana unaweza kumwona mwanamke au mwanamume ambaye atakugusa ghafla tumboni au sehemu yoyote ya mwili wako, na jambo hilo likasababisha ugonjwa. Kwa hiyo, Mkristo anatakiwa, akiona hivi, akemee kwa mamlaka ya Jina la Yesu, huku akitawanya na kuharibu mipango ya ibilisi, n.k. Na hakika yake, kila utakachokitawanya au kukifunga hapa duniani, kitatendeka vivyo hivyo. (Mat 16:19, Mat 18:18).

Shughuli za kitamaduni

Ni muhimu pia kutambua kuwa watu wengi huingizwa kwenye shughuli za shetani au kuingiwa na mapepo kupitia shughuli nyingi za kitamaduni, kama vile sherehe na ngoma. Nyingi ya tamaduni zetu zina ushetani ndani yake. Wengine hupagawa kupitia marafiki, na wengine kupitia kusoma baadhi ya maandiko au vitabu vya hadithi. Mapepo huzungukazunguka karibu na kila sanamu. Hutenda kazi kupitia ibada ya sanamu (Zakaria 10:2). Kama sehemu muhimu ya dini, ibada ya sanamu ni kuvipa nguvu ya kiungu vitu vya kawaida na kutoa heshima ya kiungu kwa kiumbe (Rum 1:18-22). Maandiko yanaita ibada ya sanamu kuwa ni ukahaba wa kiroho (Yeremia 3:8-10). Kwa hiyo, mwana wa Mungu hatakiwi kuwa na uhusiano wowote, wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja, na ibada ya sanamu. Kile kinachoitwa maisha ya juu, juju na muziki wa disko vina uvuvio wa shetani na mapepo.

Nakumbuka, kabla Bwana hajaniokoa, kwenye mkutano mmojawapo tuliofanya na shetani, alisema, “Dunia hii ni yangu na naenda kuitawala kwa nguvu zangu, na nitawaharibu wote wanaomwamini Yule Mwenye Haki.” Shetani huwa hataji Jina la Yesu. Mtu yeyote akifanya hivyo mbele zake, anakuwa kwenye hatari ya kupoteza maisha yake. Aliahidi kutufanya sisi tuliokuwa maajenti wake, magavana, n.k. Shetani ni mwongo na hakika ni baba wa uongo. Kulikuwa pia na mipango ya kuwanyamazisha Wakristo wa Naijeria kwa kupiga marufuku uingizaji wa Biblia na maandiko mengine ya Kikristo.

Huwa anatenda kazi kupitia wasioamini walio kwenye nyadhifa za utawala, kwa kuanzisha sera na programu zilizo kinyume na Ukristo. Pia anaanzisha vituo vya uponyaji ambavyo vitaonekana ni vya kiroho kabisa; na kupitia hivyo, ananasa roho za watu. Hivi kwa kawaida hujulikana kama nyumba za uponyaji wa kiroho na zimetuzunguka kila upande. Hapa miujiza mingi ya uongo hutendeka ili kuwadanganya washiriki wake. Shetani anajua sana juu ya  kuja mara ya pili kwa Yesu Kristo na kila wakati huwahimiza maajenti wake kuharakisha na kuwa na bidii katika operesheni zao. Kila wakati husema, “Hatuna tena muda wa kutosha.” Wapendwa wana wa Mungu, shetani halali. Kwa nini wewe ulale?  

ITAENDELEA ....

2 comments: