Wednesday, July 16, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 2





Huu ni ushuhuda unaotokana na kitabu kinachojulikana kama Baptized by Blazing Fire, Devine Expose of Heaven and Hell kilichoandikwa na Mchungaji Yong-Doo Kim wa Korea. Ni ushuhuda mrefu ambao utakupa mafundisho, maonyo, utakutia moyo na kukuimarisha katika safari yetu ya kuelekea kwa Baba, Mbinguni.



…………………………………………………………


 




KITABU CHA 1 – SEHEMU YA PILI

====  SIKU YA 6  ====

Baek, Bong-Nyo: 
Saa 4 zilishapita tangu mchungaji aanze mahubiri yake. Hakuna kati yetu ambaye hata alifunga macho. Hata Meena mwenye miaka 5 naye alikuwa akisikiliza kwa makini. Nilipokaza macho yangu kwa mchungaji, Yesu alitokea na kundi la malaika. Yesu alikuwa akiongoza kondoo tisa. Nikagundua kuwa idadi ya kondoo ilifanana na idadi ya mashujaa wa maombi waliokuwapo! Alisema, "Ninyi wote ni kondoo wangu. Ninawachunga wakati wote, kwa hiyo msiogope."

Mahubiri ya mchungaji Kim yalikuwa yanawaka, aliongea kwa moto wa Roho Mtakatifu. Yesu alihusika sana kwenye mahubiri hayo ya mchungaji, na alipaza sauti akisema,  "Safi sana Mchungaji Kim. Unafanya vizuri sana." Yesu alikuwa akitembeatembea pembeni ya Mchungaji Kim, huku akitabasamu kila wakati. Mchungaji akienda kushoto, Yesu naye anaenda kushoto; akienda kulia, Yesu naye anaenda kulia. Kisha walitokea malaika kumi. Mmoja alisimama akiwa na kitabu kilichofunguliwa huku akirekodi mambo fulani kwa haraka. Malaika wengine walimzunguka mchungaji huku wakiwa na vyombo, wakikusanya mahubiri yale. Chombo kimoja kikijaa, malaika mwingine anakuja na chombo kingine. Waliendelea hivi huku wakiondoka na mahubiri yale hadi Mbinguni. Yesu alifurahia na malaika nao walifurahia.  

Baada ya mahubiri, ulifika wakati wa kuomba kwa pamoja. Tukiwa tunaomba, washirika tisa wa ile timu ya maombi walionekana kama wanapigana vita. Tukiwa tunamlilia Bwana kwa toba, machozi na jasho vilikuwa vikitiririka.

Kisha Yesu alinisogelea, huku akiniita jina langu. Bwana aliongea kwa kulinganisha Makanisa kadhaa. "Bong-Nyo, makanisa mengi yamelala huku misalaba yao myekundu ikiwa inawaka usiku, lakini washirika wa  Kanisa la Bwana wanaomba kwa bidii. Nina furaha sana sasa." Kisha malaika walishuka wakiwa watatuwatatu. Moja, mbili, tatu, nne, tano... Nilihesabu kwa muda lakini sikuona mwisho wa mstari wao, kwa hiyo nikaacha kuhesabu. Waliendelea kushuka bila mwisho na kusimama mbele ya madhabahu ambako sisi tisa tulikuwa tukiomba. Walikusanya maombi yetu kwenye vyombo vya dhahabu na kwenda nayo Mbinguni na kurudi tena. Malaika hupelekea maombi yetu kwa Mungu. Lakini hivi karibuni, wakati washirika wa Kanisa la Bwana wakiabudu usiku kucha huku tukijitupa kwenye maombi, malaika walitushukuru kwa kuwapatia kazi ya kutosha ya kufanya. 

Yesu alisema, "Kwa juhudi yenu ya kumwita Bwana na kuabudu usiku na mchana, Baba wa Mbinguni, Mimi na Roho Mtakatifu tumeshangazwa na kujitoa kwenu. Ni nadra kuona Kanisa kama lenu duniani." Baba wa Mbinguni alituuliza sisi, "Je, niwape kitu gani?" Kisha Baba alimwuliza Yesu, "Mwanangu, unafikiri nifanye nini?" Yesu akajibu, "Baba, fanya kama upendavyo Wewe." Roho Mtakatifu alitupa upako wa moto mtakatifu, mafuta na vipawa vya Mbinguni.  Baba akasema, "Kwa mke wa mchungaji, Kang, Hyun-Ja, yeye hasa nataka kumpa upako wa moto uwakao wa Roho Mtakatifu na uwezo wa kuponya wagonjwa, na nataka aweze kucheza uchezaji wa kiroho kwa ujasiri."

Mke wa mchungaji alianza kucheza uchezaji wa kiroho, kila mmoja alitazama kwa heshima kubwa. Uso wake ulianza kuwa mwekundu kadiri alivyocheza kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.

Ghafla Mungu alinisukuma mahali ambapo palionekana kama vile niko ndani ya maji; na kana kwamba mwili na miguu yangu vilikuwa vikienda kwa akili zake vyenyewe. Baadaye kidogo nilisikia sauti ya Bwana ikisema,  "Nitawabatiza kwa moto uwakao." Nilihisi kama vile nimetupwa kwenye mafuta, na mwili wangu mara moja ulikuwa kama una moto.

Baadaye Yesu alianza kuongelea kuhusu makanisa ya Korea. Kwa sauti yenye ghadhabu, alisema, "Kuna faida gani kwa kanisa kuwa tu kubwa na tupu ndani huku likiwa na msalaba unaowaka? Niliwachagua viongozi wa kichungaji ili kuokoa roho zilizopotea, lakini hawana maombi, na moyo Wangu unaumia."

Baadaye, nikawa nacheza uchezaji mtakatifu huku nikiomba kwa lugha pale Yesu aliponishika mkono, huku akisema, "Bong-Nyo, twende Mbinguni." Mara niliposhika mkono wa Yesu, nikajikuta nimevaa vazi jeupe, na nilikuwa napaa na Yesu hewani. Nilipofika juu zaidi, dunia ikaendelea kuwa ndogo zaidi na zaidi. Ulimwengu ulikuwa mzuri sana. Tulipaa kwa muda, kisha tukafika kwenye galaksi. Tulipovuka galaksi, kukawa giza tena, nami niliona barabara mbili. Tulipita kwenye barabara ya kulia. Kwa hiyo, nikauliza,  "Bwana, hii barabara ya kushoto inaelekea wapi?" Aliniambia kuwa ilikuwa inaenda hadi jehanamu. Ilionekana kuwa tulikuwa kwenye barabara kwa muda mfupi, ndipo ulionekana mwanga ghafla ambao ulikuwa mkali sana, kiasi kwamba sikuweza kufungua macho yangu.

Mbingu ilikuwa imejaa nyota. Duniani mara nyingi watu hutumia neno paradiso, lakini kile nilichokiona hakiwezi kuelezwa kwa maneno ya kibinadamu. "Inawezekanaje? Inawezekanaje?" niliuliza. Wanadamu hawawezi kuelewa kikamilifu vile Mbingu ilivyo. Malaika wengi walinisalimia na kunikaribisha. Yesu akasema, "Umeamua na kujitoa mwenyewe kuhudhuria kanisani kwa bidii, kwa hiyo nataka nikuonyeshe nyumba yako ya Mbinguni. Twende nifuate.."  Niliona malaika wengi wakijenga kitu fulani. Yesu akaniambia, "Hii ni nyumba yako." Niliangalia lakini kulikuwa hakuna nyumba! Niliona tu msingi mrefu. Malaika walikuwa wakitumia dhahabu kufanya kazi yao. Yesu akasema, "Ndani ya siku chache, nyumba yako itainuka. Usikate tamaa, bali omba kwa bidii na ishi kwa uaminifu. Ulimwabudu shetani na umewapeleka watu wengi kwenye udanganyifu. Lakini ulifanya uamuzi wa kuniamini Mimi na kuhudhuria kanisani kwa bidii."  Yesu akasema, "Kuna mahali nataka nikuonyeshe, kwa hiyo nifuate," na akanipeleka mahali pengine.  "Mpendwa wangu Bong-Nyo, nitakuonyesha stoo ya hazina na nyumba ya watu wanaohusika na kuwaletea Injili ninyi, mchungaji wa kanisa lako, Kim, Yong-Doo, na mke wake, Kang, Hyun-Ja.  Angalia kwa makini. Nyumba ya ghorofa elfu moja duniani ni sawa na nyumba ya ghorofa moja Mbinguni, na kila kitu Mbinguni hakiwezi kuelezewa kwa msamiati wa kibinadamu maana haujitoshelezi.

Mbele ya macho yangu kulikuwa na jumba kubwa sana sana, na nuru liliyokuwa likiitoa ilikuwa kali sana kiasi kwamba sikuweza kuinua kichwa changu. "Hii ni nyumba ya Mchungaji Kim, Yong-Doo," Yesu alisema. Yesu aliinua mkono wake na ghafla niliweza kuona waziwazi nyumba mpya ya mchungaji kule Mbinguni. Kisha Bwana akasema, "Sasa hebu tuone stoo ya hazina ya Mchungaji Kim."  Umbali toka kwenye stoo ya hazina ulikuwa kama wa vituo vitatu hivi vya mabasi, kwa kulinganisha. Stoo ya hazina ya mchungaji ilikuwa ina ulinzi mkali sana wa mamia ya malaika, ili tusiweze kuingia. Yesu alipotokea, malaika walinzi walishusha mabawa yao na kusimama wima na kuinamisha vichwa mbele zake. Kila nyumba ya hazina Mbinguni ilihitaji ruhusa ya Yesu ili kuingia ndani. Rangi zinazong’aa toka ndani yake zilikuwa zinashangaza sana.   "Haa! Mchungaji Kim atafurahi sana," nilisema. Ndani ya stoo ya hazina kulikuwa na malaika wasio na idadi wakishughulika kukusanya vitu vya mchungaji kutoka duniani. Hazina ya mchungaji inaendelea kuongezeka. Nikamwuliza Yesu, "Kwa nini nyumba ya Mchungaji Kim ni kubwa kiasi hiki, na kwa nini ana hazina nyingi namna hii?" Bwana akanijibu, "Mchungaji Kim, Yong-Doo alianza kazi yake ya uaminifu mapema, na kila wakati amekuwa akiniomba na kunitumikia kwa bidii."  Hatimaye Yesu akasema, "Kwa leo hayo yanatosha. Tutaona mengi zaidi wakati mwingine utakapokuwa hapa." Akanirudisha kanisani. Yesu alisema jambo moja la mwisho kabla hajaniacha: "Nilipokufa msalabani, wengi waliamini kuwa sitaishi tena. Hao waliacha kuniamini; wakaacha kwenda kanisani, na sasa wanafanya mambo mengine ya kidunia."

====  SIKU YA 7  ====

Kim, Joo-Eun: 
Niliomba kwa lugha kwa takribani saa moja, ndipo ghafla mwanga mkali uliangaza. Kisha Yesu, akiwa amevaa vazi jeupe alitokea mbele yangu. Alikuwa na nywele za kahawia na alikuwa amevaa vazi kama mgolole jeupe linalometameta. Aliniita kwa jina. "Joo-Eun, mpendwa wangu Joo-Eun, nakupenda." Yesu alinisogelea na akawa anaongea nami. Nilishangaa na kusema, "Hivi wewe kweli ni Yesu? Haa! Hakika nakupenda. Wewe ni mwema sana." Nilijawa na msisimuko kwa sababu sikujua cha kufanya. Yesu alikaa mbele yangu huku akisema kuwa ananipenda. Nilisema kwa msisimuko, "Yesu, hakika nakupenda," naye akajibu, "Ndiyo, nakupenda nawe pia sana." Yesu akaniambia, "Omba kwa bidii, nami nitajionyesha kwako. Nitakupeleka Mbinguni na kukuonyesha jinsi kulivyo. Kwa hiyo, omba kwa bidii,"; baada ya hapo akatoweka.

Nilipoona haonekani, nilianza kwa kuomba kwa lugha kwa nguvu zangu zote. Ghafla, mbele yangu kulitokea kitu cha ajabu. Kilikuwa kinakimbia kunijia. Kona zote za macho yake zilikuwa kama zimechanika, na jicho la kulia lilikuwa na sura ya X. shetani hili lilikuwa limejaa makovu. Nikapaza sauti, "Kwa Jina la Yesu, ondoka kwangu!" Lile shetani likapotea. Nikaendelea kuomba, ndipo kitu chenye macho membamba kuliko ya paka kilitokea mbele yangu. Kilikuwa na mabawa kama ya popo, na meno makali yaliyotokeza nje. Kilikimbia kuja kwangu ili kunitisha, lakini nilikishinda kwa Jina la Yesu. 
 
Hatimaye pepo lenye sura isiyo ngeni lilitokea, na nikawa najiuliza  niliiona wapi. Niligundua kuwa nililiona kwenye michezo ya kompyuta (computer game Starcraft).  Pepo hili la kike lilinikimbilia. Lilijaribu kunitisha kwa kunikodolea macho. Tofauti na mapepo mengine maovu ambayo yalikimbia mara nilipoita Jina la Yesu, hili halikuondoka kirahisi. Hata baada ya kutaja Jina la Yesu mara kadhaa, halikushtuka, na nikaanza kuingiwa na hofu. Nilikimbia kwa Mchungaji Kim pembeni ya madhabahu na kuendelea kuomba. Mchungaji alishika mkono wangu na kuuinua, akaanza kuomba na mimi. Hapo ndipo pepo lile lilipoondoka.

ITAENDELEA ….

No comments:

Post a Comment