Sunday, March 16, 2014

Mwanafunzi wa Mchawi - Sehemu ya 5


(Waebrania 11:35-40)


Hii ni sehemu ya mwisho ya ushuhuda wa Jim McCoy aliyekuwa mwanafunzi wa mwanamke mchawi kule Marekani, lakini akaokolewa na Bwana Yesu na kutolewa ndani ya vifungo vya mauti.



.........................................

Mojawapo ya mambo hayo ni kuhakikisha kuwa Wakristo lazima wakubaliane na imani ya New Age, watii mafundisho yake, vinginevyo ni lazima waharibiwe.  Kinachoongelewa hivi sasa ni juu ya kuwatowesha kabisa! Kama unadhani kuwa mipango hii ni maneno tu, basi umekosea sana. Haya ni mambo ya kweli kabisa! Mimi mwenyewe nimekuwa nikifanyia kazi mipango hii na nimeona jinsi inavyoenezwa. Leo, nilipoongea na ndugu mmoja, nilimwambia kuwa Mshauri wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya New Age kule Marekani alishaagiza nchini gilotini 100,000 (gilotini ni mtambo wa kukatia shingo za watu), kwa ajili ya kuwaua wale Wakristo wasiokuwa tayari kuonyesha ushirikiano. Vilevile, katika nchi nyingine mipango kama hiyo inaendelea kuandaliwa. Lakini kumbuka kuwa hizi si ndoto bali ni mambo halisi yanayotokea sasa hivi. Mshauri wa Umoja wa Mataifa ni taasisi muhimu katika kuwezesha sheria hizi zianze kufanya kazi.


Lakini hali halisi nyingine ni ukweli kwamba Bwana Yesu Kristo anakuja kwa ajili ya bibi harusi wake, ambaye naye ni lazima asiwe na waa wala kunyanzi lolote (Efe. 5:27).

Kumpokea Yesu kama Mwokozi wako binafsi kwenye maisha yako peke yake haitoshi kukuponya wewe. Ni lazima pia ufanye uamuzi wa kubadilika moyo wako chini ya uongozi wake, na kuwa kiumbe kipya. Kwa njia hii ndipo utaweza kusimama kinyume na wale manabii na hayo makundi ya uongo. Tuna watu duniani kote ambao wanahatarisha maisha yao ili kuharibu mafundisho hayo ya New Age na ninajua kuwa wengi katika jamhuri ya Cheki wanajitahidi kufanya vivyo hivyo. Unaweza kuuliza, “Nawezaje kufanya hivyo bila kufanya mapinduzi? Nawezaje kushiriki kibinafsi katika vita hii ya kiroho?” Sasa siongelei juu ya kumwaga damu au kupigana kimwili bali ninachosema ni kuwa, tumia zile zilaha ambazo Bwana Yesu ametupatia.

Yafuatayo ni mambo muhimu ili kuweza kupigana vita hivi:


1) Kwanza ni kubatizwa kwa Roho Mtakatifu, maana bila Roho Mtakatifu hutaweza kujua namna sahihi ya kuzitumia silaha hizo.

2) Silaha yenye nguvu zaidi na inayofaa zaidi dhidi ya New Age na mambo mengine ya uongo ni kuhubiri Injili kwa nguvu kwa mataifa yote kwa ajili ya Bwana Yesu Kristo, hivyo kuwa na nguvu kwenye jamii yako. Bwana Yesu anarudi hivi karibuni (Ufu. 22:20) na uombe kuwa akukute uko tayari, na uko nje kule ukiwahubiria watu Injili yake. Ni lazima kuwajulisha watu, na kuwaepusha watoto mashuleni na mambo haya. Ni lazima ufanye uinjilisti na kufanya kazi chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu ili kwamba jamii yenu isivunjike tena na watu kuibiwa. Nyie vijana ndio msingi wa kesho. Ni lazima mzuie mambo haya kwa kizazi hiki na vile vijavyo. Msipofanya hivyo, hali itakuwa mbaya sana. Msikubali uinjilisti uzimike kwenye nchi yenu. Ni lazima muwafundishe watoto  na kuwaonyesha kuwa Yesu Kristo kweli anajishughulisha na maisha ya watu. Ni lazima muwe na ushuhuda ulio hai juu ya Bwana.

Nilitembea usiku kucha kwenye mitaa ya Prague. Nimetembea usiku kucha kwenye mitaa ya Brno, na kile nilichoona ni kibaya sana. Watoto walikaa mitaani wakiwa wamelewa chakari, huku wakicheza muziki wa rock ambao unawaharibu ufahamu wao. Kuna makahaba wengi wa umri mdogo tu. Watoto hawa; vijana hawa wanaelekea kwa kasi shimoni, kwenye uangamivu. Kwa hiyo, ninyi walimu, wazazi na yeyote mwenye ushawishi, wafundisheni Injili ya Yesu Kristo. Hilo ndilo tumaini pekee kwa ajili yao na hata kwenu ili msije kutumbukia kwenye mafundisho ya New Age. Kama nilivyosema kabla, wanaharakati wa New Age na waabudu shetani wamelenga hasa kwa vijana. Ni lazima tuwe makini na tabia za vijana kwenye makanisa. Vijana ndio msingi wa jamii. Hao ndio taifa lenyewe.

Inasikitisha lakini ukweli ni kwamba New Age wako makanisani tayari miongoni mwa vijana. Pia kwenye sehemu mbalimbali za jamii wameshaingia. Vilevile kwenye nafasi za juu za kitabibu kupitia “holistic teaching”. Haya ni mafundisho yanayosema kuwa mwanadamu ni kiumbe ambaye tayari ameshakuwa mkamilifu.

Namna zote zile mbadala za utabibu ziko chini ya mafundisho haya. Wanasaikatria (psychiatrists) wote wanaotoa huduma zao kwa kutumia upigaji taswira kichwani (visualization) na kufikiria (imagination), wanaamsha nguvu za maono (psychic power) ndani ya mtu. Hii ina maana kuwa mtaalamu wa eneo hilo anakuwa anaingiza ndani yako mawazo fulani anayotaka uwe unayaona, hivyo kukuongoza katika welekeo fulani ambao anautaka yeye. Hii ni mbinu ambayo shetani ataitumia ili kukutoa nje ya mpango aliokuandalia Mungu.

Eneo la tiba mbadala linajumuisha njia kama tibavitobo na tibamgandamizo
(acupuncture and acupressure). Niliongea na baadhi ya madaktari nchini kwangu na pia na baadhi ya Wakristo ambao wamewahi kutumia aina hizi za uponyaji. Walikuwa na anwani inayoonyesha kampuni fulani ya kule Kalifonia, ambayo hujishughulisha na huduma hizi. Nilibaini kuwa kampuni hii ina malengo ya kuhakikisha kuwa sindano zote zinatoka mahali pamoja kisha zisambazwe duniani kote.

Niliwauliza kama jambo hili linafanyika kwa maslahi ya lile Baraza la Ulimwengu
nao wakanithibitishia kuwa hilo ni kweli. Pia nilitafuta ni wapi hizi sindano zinazotumika kwenye tibavitobo zinakotoka. Na sasa naweza hata kuwaonyesha nyaraka zinazothibitisha kuwa ni kweli kwamba kila sindano inatoka kwa makuhani wa kibudha. Kuna kiwanda kikubwa kinachozizalisha, kisha hao makuhani huzifanyia maombi yao kabla ya kusambazwa duniani kote. Kwa namna hiyo, ile laana yao inasambaa kote. Tangu wakati wa hizo sindano kutengenezwa hadi zinapotumiwa kwa mgonjwa, ile sala ya kuhani inakuwa inafuatana na hiyo sindano.

Nyuma ya matumizi ya hizi sindano ziko nguvu za kiroho ambazo huathiri aina fulani ya nguvu (energy) ndani ya mwanadamu na hatimaye kumharibu. Zinaweza kupoza maumivu kwa muda tu lakini watu wanakuwa chini ya hiyo nguvu. Kwa kifupi ni kuwa sindano hizi zina nguvu za kipepo na za imani za kipagani za mashariki nyuma yake. Hapa tena shetani anawadanganya watu na wakati huu anapitia kwenye mgongo wa sayansi. Wakristo wengi hutumia tiba mbadala, badala ya kukimbilia uponyaji wa Bwana Yesu. Yeye ni yuleyule, hajabadilika. Nilijua hilo pale nilipokabiliwa na kifo kutokana na kansa na nimonia nilipokuwa nikiishi kwenye kile kijumba chenye baridi kali. Nilipomwita Yesu, alikuja kwenye maisha yangu na kuniponya kabisa. Yesu Kristo ndiye tunayemuhitaji.

Jamhuri ya Cheki hivi sasa inayo fursa kubwa inayoweza kuitumia, nami ninaomba kuwa muitumie na kwamba New Age wasilete uovu wao kwenye nchi yenu. Naomba kwamba maisha yenu yawe mikononi mwa Yesu Kristo; ili muweze kupigana hii vita kubwa kabisa, ambayo si yenu tu bali ni ya mataifa yote na Wakristo wote. Hatari hiyo kubwa ni kundi la New Age. Soma ufunuo 21:7-8. Ndiyo, uongo huo upo hapa sasa hivi! New Age yote ni uchawi; kila kitu kinachohusiana na mambo haya ya giza – yaani imani yao. Wanataka kumleta Lusifa. Hatuko hapa kuwachukia wao, lakini ni lazima tuuchukie uongo na udanganyifu huo ambao umewanasa. Fanyeni kazi ya kueneza Injili ambayo ametuagiza Yesu; leteni wanafunzi kutoka mataifa yote. Asanteni.    


Malengo ya New Age
- Mpango wenye dondoo kumi na tatu -

Na 1) kuanzisha umoja kwa dunia yote, dini ya NEW AGE na mfumo wa kisiasa na kijamii unaofanana duniani kote.

Na 2) dini ya dunia, yaani NEW AGE itaimarishwa kwa kutekeleza ibada ya sanamu iliyokuwa ikifanyika katika Babeli ya zamani, ambako ndiko zilikoshamiri imani za siri (mystical cults), uchawi, uabudu shetani na ufisadi (immorality).

Na 3) kuukamilisha mpango pale atakapokuja masihi wa NEW AGE, Mpingakristo ambaye namba yake ni 666, ambaye atakuja katika mwili ili kuwaongoza wale wote walioungana katika dini moja ya kilimwengu ya NEW AGE na kuusimamia huo mpango mpya wa dunia.

Na 4) kuleta dini ya NEW AGE ili kuwasaidia viongozi wa kiroho (mapepo) kuja na kuandaa njia ya Mpingakristo. Huyu mtu, ambaye ni mungu wa NEW AGE, atatangazwa kuwa ni Mwalimu mkubwa katika dunia.

Na 5) kaulimbiu kuu ya hii dini ya kilimwengu itakuwa ni: “Amani ya dunia!” “Upendo!” na “Umoja!”

Na 6) Mafundisho ya NEW AGE yatafundishwa na kuenezwa kila mahali duniani kote.

Na 7) viongozi na waumini wa NEW AGE watakuwa wakisambaza uongo, kwamba Yesu si Mungu wala si Kristo.

Na 8) Ukristo na dini zingine zitakuwa ni sehemu ya dini ya kilimwengu ya NEW AGE.

Na 9) kanuni za Kikristo ni lazima zichafuliwe ili watu wazitilie mashaka na kuachana nazo.

Na 10) Watoto ni lazima wadanganywe na wakiwa mashuleni, wafundishwe mafundisho ya NEW AGE.

Na 11) wadanganyifu wataudanganya ulimwengu kwa kuuambia kuwa mwanadamu ni mungu.

Na 12) sayansi na dini ya kilimwengu ya NEW AGE zitaungana pamoja.

Na 13) Wakristo watakaokataa mpango wa NEW AGE watashughulikiwa. Ikibidi, wataharibiwa na dunia “itasafishwa” – yaani watauawa ili wasiwepo kabisa.

Hapa chini, nimechagua mafundisho ya aina kuu tatu ulimwenguni ili kukufanya uelewe zaidi mafundisho ya NEW AGE – Ukristo, uasili [naturalism – ambayo inajumuisha kutoamini mungu kabisa (atheism) na ubinadamu (humanism)], kisha New Age. Haya ni makundi matatu ya msingi – kile wanachoamini, misimamo yao na tofauti kati yao:

UKRISTO

Unaamini yafuatayo:

1) Mungu: anajua yote; ana nguvu zote; ni Muumbaji wa mwanadamu na ulimwengu.

2) Mwanadamu: aliumbwa na Mungu kwa sura ya Mungu. Anatakiwa kujikana na kumtukuza Muumba.

3) Kweli: ni thabiti, haibadili, inaweza kujulikana (yaani, inawezekana kujua jema na baya).

4) Mwongozo wa mwanadamu na kanuni za maisha: Neno la Mungu Muumba ambaye ameumba vyote. “Ee Bwana, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” (Yer. 10:23)

5) Kristo: ni Yesu, Mzaliwa wa kwanza wa Mungu, Mwokozi na Bwana wetu.

6) Tatizo la mwanadamu: Chanzo cha dhambi: kutomfuata Mungu.
Suluhisho: Imani na utii kwa Mungu – Yesu Kristo.

7) Familia: ilianzishwa na Mungu na inaongozwa na kanuni za kimaadili. Kwa njia hii, ndoa pamoja na watoto wanalindwa.

8) Kifo: ni kuingia katika ulimwengu mwingine, ambako roho inaendelea kuishi milele, ama mbinguni au jehanamu.

9) Malengo: kumfundisha kila mtu kuhusu Mungu na Yesu Kristo ili kwamba kuwepo na uzima tele sasa na milele. 

HITIMISHO:  Mwanzo, Mungu alimuumba mwanadamu kwa sura yake. Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu  (Ebr. 9:27)



UASILI (NATURALISM)

Unaamini yafuatayo:

Na 1) Mungu: hakuna muumba aliye na nguvu zisizo za kibinadamu. Mawazo kuhusu Mungu yalitokana tu na jamii za zamani ambazo hazikuwa na ustaarabu wala maendeleo, bali zilijaa ushirikina tu.

Na 2) Mwanadamu: alitokea kwa bahati tu kutokana na mabadiliko (evolution). Wanamkana Muumba na kujitukuza wao wenyewe.

Na 3)  Kweli: ni jambo linalotegemeana na hali ya mambo; inaweza kubadilika tena na tena (yaani, kilicho kweli sasa, kinaweza kisiwe kweli baadaye). Kila mtu kibinafsi ndiye mwenye kuamua kweli ni ipi kwake. Imani yao ni kuwa, “wewe fanya kile ambacho roho yako inapenda.”

Na 4) Mwongozo wa mwanadamu na kanuni za maisha: hakuna mamlaka iliyo nje ya mtu; kinachomwongoza mwanadamu ni sayansi na ufahamu wake binafsi. “Ninawaza. Nina hisia. Niko sawa tu.” Maadili yanategemeana na hali.

Na 5) Kristo: ni mwalimu, mwanamaadili, hana asili ya uungu.

Na 6) Matatizo ya mwanadamu: ni matokeo ya kukosa elimu. Pia ni matokeo ya kuwa na dini.

Suluhisho: maarifa, elimu, kumwelewa mwanadamu, sayansi na teknolojia.

Na 7) Familia: ni kundi la watu wanaoishi pamoja; kila mtu yuko huru kuamua juu ya kanuni za kufuata maishani.

Na 8) Kifo: ndio mwisho wa mwanadamu; hakuna mbingu wala jehanamu.

Na 9) Malengo: kutengeneza jamii timilifu duniani (utopian society) kupitia serikali ya kijamii ya kilimwengu.

HITIMISHO: mwanadamu ana wema ndani yake. Wazo la Mungu lilitokana na jamii za kale ambazo hazikuwa na elimu. Mwelimishe mwanadamu ili ajue kuwa Mungu hayupo.


NEW AGE MOVEMENT

Wanaamini yafuatayo:

Na 1) Mungu: kila mtu na kila kitu ni mungu.

Na 2) Mwanadamu: ameendelea kimwili, lakini bado anaendelea kupiga hatua kiroho. Wanamkana Muumba na kujitukuza wenyewe.

Na 3) Kweli: ufunuo unatoka kwa mtu mwenyewe au kutoka kwa “viongozi wa kiroho” (spiritual guides). Kwa hiyo, ni kutoka kwa mwanadamu hadi kwa mwanadamu mwingine.

Na 4) Mwongozo wa mwanadamu na kanuni za maisha: sayansi na “mungu aliye ndani ya mwanadamu” ndio wanaounda dini. Msingi wa maamuzi: upendo kwa jirani, umoja wa kilimwengu.

Na 5) Kristo: ni mmoja kati ya wengi, ambao walileta michango katika mpango wa kiroho.

Na 6) Matatizo ya mwanadamu: yanasababishwa na utengano kati ya umoja (the oneness) toka kwa kila mmoja na toka kwenye maumbile ya asili (nature).

SULUHISHO: mabadiliko juu ya ufahamu (consciousness) katika umoja na “mungu ndani ya moyo wa mwanadamu.”

Na 7) Familia: kutokana na kurudi tena duniani baada ya kufa (reincarnation), kila roho inachagua familia iitakayo kabla ya kuzaliwa; na kwa jinsi hii, mafungamano yanakuwa thabiti.  

Na 8) Kifo: ni kama kiinimacho tu; ni kubadilika na kuingia kwenye maisha mengine ya mwili kwa njia ya kuzaliwa kama kiumbe mwingine (reincarnation).

9) Malengo: kuunda jamii timilifu (utopian society) kupitia dini ya kilimwengu na serikali moja ya ulimwengu wote.  

HITIMISHO: Mungu ni hai kabisa kwa sababu MIMI MWENYEWE NI MUNGU na ataendelea kuwapo baadaye kupitia maisha ya wanadamu wengine.

Mpokee Yesu leo.
Kama unahubiri, fanya kazi kwa bidii.
Jungu la uovu linakaribia kumwaga duniani kile ambacho kimekuwa kinapikwa. Lakini kwa walio ndani ya Yesu, milango ya kuzimu haitaliweza Kanisa!

………………………………………

Neno la mwisho toka kwa blogger:
Duniani hivi sasa kuna uovu mwingi na mkubwa na wa kutisha unaoendelea kusukwa na shetani kupitia wanadamu wanaomtumikia. Lengo ni kushika madaraka ili maamuzi mbalimbali yaweze kufanywa yanayowanyima watu uhuru wa kumwabudu Kristo ili kwamba giza la kuzimu liweze ufunika kabisa ufahamu wa mwanadamu. Kristo ndiye NURU pekee kwetu.

Biblia inasema vizuri sana: Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza. (Yohana 1:4-5).

Lakini liko tatizo moja kubwa:
Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. (Yoh 1:10-11).

MARANATHA!

………………………………….

Kama ungependa kusoma ushuhuda huu kwa Kiingereza, bofya HAPA. Lakini kwa sasa uko kwenye Word Document ambayo itabidi u-dowload. Utaangalia upande wa chini na kubofya link ya Disciple of a Witch.

3 comments:

  1. Asante sana umenipaisha tena kiroho nitazidi kuhubiri.Ubarikiwe sana.

    ReplyDelete
  2. Amen. Ubarikiwe na Bwana na azidi kukupaisha hadi utimilifu wa Kristo kwenye eneo alilokuitia katika Jina la Yesu.

    ReplyDelete
  3. barikiwa sana mtumishi wa mungu ushuhuda huu umenigusa na umenikumbusha sana wakati mungu aliposema nami nikasomee psychology chuo kikuu.....mwanzo nilipata shida sababu kuna aina ya vitabu nilikuwa nikivisoma mungu anizuia kwa namna flani vinaitwa SELF HELP BOOKS....nilichogundua psychology baada kuanza kusoma psychology chuoni ni hivi.....psychology yenye misingi mizuri ni ile ambayo inamkubaliana na neno la mungu (school of thought) lakini kuna baadhi ya wasisi walidiriki hata kusema dini ni moja ya ugonjwa wa akili ambao utatibiwa na psychotherapist mfano Sigmund Freud.....hivyo psychology ipo parts ambayo inamkubali mungu na haina tatizo ila ipo nyingine part kama...Self help books, Telepathy,psychic na nyingine mtumishi wa mungu huyo alizozitaja....kanisa tuwe macho...Bwana Yesu atusaidie

    ReplyDelete