Sunday, December 21, 2014

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 7




Bwana alizungumza waziwazi. Wakati huu, shughuli za kiroho za makanisa zinapingana na kile ambazo niliwakusudia. Viongozi na waumini wananiabudu kimazoea tu na wananijua kwa nadharia tu za vitabuni. Iweni na shauku kubwa kisha mnijie Mimi.


Bwana wetu ana shauku ya kutuonyesha uhalisia wa kuingia kwenye mapambano ya kiroho dhidi ya mapepo wabaya na kufungua macho yetu ya kiroho ili kwamba tuweze kuona moja kwa moja Mbinguni, kuzimu, malaika na shetani. 



==== SIKU YA 16 ====

Lee, Yoo-Kyung:
* Mabishano husababisha nyumba yako ya mbinguni ianguke.
Huko Mbinguni niliuliza, “Yesu, niliambiwa kuwa tuna nyumba Mbinguni. Ningependa kuona nyumba yangu. Alinipeleka hadi kwenye nyumba yangu. Tulitembea kwa kitambo, ndipo nilipoona nyumba ya dhahabu inayong’aa. Yesu alisema, “Hii ndiyo nyumba yako.Nilishangazwa sana na uzuri wake. Malaika walikuwa wakipita huku na kule katika harakati za kuijenga nyumba yangu.


Nilipouliza ni nyumba ya ghorofa ngapi, alisema kuwa ghorofa ya tano ilikuwa karibu kukamilika na nguzo zaidi zilikuwa zikijengwa ili kuongeza ghorofa zingine zaidi. Pia niliona nyumba ya ndugu Haak-Sung na ghorofa ya saba ilikuwa ndio imekamilika.


Nilipoomba kuonyeshwa nyumba ya Joseph na ya Joo-Eun, Yesu alionekana mwenye wasiwasi, akasema, Nifanye nini? Nini kinaweza kufanyika?” Nikamwuliza Yesu kama kulikuwa na tatizo. Alisema kuwa ghrofa ya tatu na ya nne zilikuwa karibu kumalizika, lakini walipoingia kwenye mabishano, nyumba zilianguka. Yesu alinifundisha kuwa mtu akiwa mchoyo, mbishani au mtukanaji, nyumba yake Mbinguni huanguka. Hii inawahusu watoto na watu wazima. Yesu aliniambia nikawaambie Joseph na Joo-Eun waache kabisa kugombana na kubishana kunapotokea kutoelewana.


Yesu alionekana mwenye uso wa huzuni sana alipoangalia nyumba iliyoanguka. Hakuficha huzuni yake. Oh, tufanye nini? Kwa nini Joseph na Joo-Eun hubishana kiasi hicho? Tafadhali, Yoo-Kyung, waambie Joseph na Joo-Eun waache kugombana. Wote huanza kutaniana na kuishia kupigana, na wakati wanapocheza mpira, huishia kwenye mabishano. Nyumba hii ilijengwa kwa ugumu sana na malaika kwa maagizo yangu. Tutaijengaje tena sasa?”


Mara nyingi huwa nagombana na kaka yangu, Haak-Sung, na sasa natambua kuwa natakiwa kuwa makini sana katika mabishano yetu.


Yesu alinivisha joho la dhahabu lenye mabawa akisema, Mpendwa wangu Yoo-Kyung, wewe unawashuhudia watu wengi sana nami nakupenda sana kutokana na hilo. Mara moja nilisema, “Bwana, hata kesho nitaenda kushuhudia pia.” Yesu akasema, Kweli? Endelea na moto huohuo. Nitaijenga nyumba yako kwa haraka.


Lee, Haak-Sung: 
*Kadiri tunavyokutana na ulimwengu wa roho kiundani zaidi, ndivyo unavyozidi kuwa wa kushangaza.


Takribani dakika 10 baada ya kuanza kuomba, mashetani watatu walitokea. Moja lilikuwa la kiume na halina kichwa. Pepo la kike limevaa gauni, huku kukiwa na mvumo wa upepo, lilijaribu kuniparua kwa makucha yake makali. Joka kubwa likiwa na vichwa pande zote lilitokea, huku kila kichwa kikitaka kutangulia. Nilipiga kelele,  “Yesu, niokoe! Tafadhali nisaidie!” Alikuja mara moja na kuyafukuza mashetani yale.


Yesu alituzunguka wakati tukiomba na alimgusa kila mmoja wetu. Yesu alimgusa Mchungaji Kim kichwani na mgongo uliokuwa ukiuma; aligusa mguu wa Joseph na mgongo wa Joo-Eun. Yesu akasema, Joseph, niambie shauku yako mojawapo. Akajibu, “Yesu, tafadhali msaidie kaka Oh, Jong-Suk asipoteze kazi yake na aendelee kuhudhuria kanisani kwa bidii.” Yesu alikubali na akanipongeza akisema, Haak-Sung, kuna baridi sana leo, lakini bado ulitoka kwenda kushuhudia na kuwahubiria watu Injili. Umenifurahisha sana.


Baada ya Yesu kuondoka, pepo la kike lililovaa gauni lilinisogelea. Lilionekana kama msichana mwanafunzi wa shule. Sikulitilia maanani nikaendelea tu kuomba kwa kunena kwa lugha. Alilazimisha uso wake uwe mbele yangu na kutekenya pua zangu kwa unyoya wakati nikiomba. Nikamwamuru aondoke. 


Kumeshakuwa na mapepo mengi tofautitofauti na mambo ya ajabu yameshatoa tangu nianze kuomba kwa bidii. Kadiri ninavyozama ndani, ndivyo ninavyozidi kukutana na vitu visivyokuwapo kwenye ulimwengu wa mwili.


Kim, Yong-Doo: 
*Adhabu ya kutoa siri


Jana mchungaji wa kanisa lililo karibu yetu pamoja na mke wake walikuja kwa ajili ya mazungumzo. Waliuliza kama wanaweza kujiunga na kikundi cha maombi. Nilijaribu kukwepa hayo mazungumzo kwa njia isiyo ya wazi sana. Lakini mke aliendelea kuuliza nami sikutaka nionekane nisiyekuwa na adabu. Hatimaye nilijikuta nimesema, sawa. Nilijua moyoni mwangu kuwa SIKUTAKIWA kufanya hivyo. Huzuni kubwa ilijaa moyoni mwangu, maana nilikumbuka jinsi ambavyo Yesu alituambia tusimweleze mtu yeyote nje ya kundi letu juu ya mkutano wetu wa maombi hadi kitabu kitakapotoka. Watu hawajui nini kinachoendelea na wakati wa maombi tunakuwa kwenye vita vya kufa na kupona dhidi ya mapepo.


Yesu alinitaka niwe thabiti na nikatae shauku ya yule mke wa mchungaji ya kujiunga na kikundi cha maombi. Nilishindwa na ndani kabisa ya moyo wangu nilikuwa naogopa kile ambacho kingeenda kutokea kutokana na kukosa kwangu utii. Ibada ya Jumapili usiku iliisha kiajabu kwa sababu ya kuhudhuria kwa huyo mke wa mchungaji ambako hakukutakiwa. Mapema alfajiri, kwenye saa 8, nilimaliza sehemu ya kwanza ya maombi na nilitaka kumwambia aende nyumbani, lakini alikaa kana kwamba alitaka kusema jambo. Nilihakikisha kuwa hakuna mtu kwenye kundi lile ambaye angesema chochote, lakini kwa namna fulani mimi na mke wangu ndio tulioishia kutoa siri.


Nilifichua siri kwamba tumekuwa tukitembelea Mbinguni na kuzimu tunapoomba iwe hivyo na wengi wamepokea vipawa vya macho ya kiroho, unabii, kupambanua kati ya roho za Mbinguni na za kuzimu, kunena kwa lugha, imani, hekima na maarifa. Nilifichua kuwa, nilikuwa kwenye harakati za kuandika matukio hayo kwenye kitabu ambacho kingechapishwa. Kwa hiyo, nilimtia moyo arudi kwenye kanisa lake na waombe kwa bidii.  


Mungu alishapanga kufunua macho yangu ya rohoni Jumapili ile usiku wakati wa maombi na alithibitisha hilo kwa kupitia washirika ambayo tayari macho yao yalishafunguka. Lakini Mungu alikasirishwa na tabia yangu ya kushindwa kuficha siri zake. Akili yangu ndogo ilidhani kuwa ilikuwa sawa tu kufichwa baadhi ya mambo, kumbe nilifanya kosa kubwa sana. Kwa sababu hiyo, mpango wa kufunguliwa macho yangu uliondolewa.


Yesu alihuzunika sana. Wakati wa maombi, Dada Baek, Bong-Nyo alilia, “Iweje kile tulichokisema kiwe ni jambo kubwa kiasi hicho?” Alilia sana. Kwa vile nilishindwa kutunza siri, nilijiona sifai na sikuweza kustahimili ile hatia. Je, Samsoni alijisikiaje alipotoa siri yake? Alisaliti uhusiano wake na Mungu. 


Sister Baek, Bong-Nyo:          
*Makemeo ya Bwana kwa Mchungaji Kim


Mpendwa wangu Bong-Nyo, kwa nini unalia kiasi hicho? Mchungaji wa kanisa lako, Kim, Yong-Doo amefanya kosa kubwa. Lakini kwa nini unalia? Yesu aliuliza kwa sauti ya ukali. Mchungaji Kim anatakiwa atubu. Matukio yanayoendelea kwenye kanisa lenu ni lazima yaandikwe kwenye kitabu na kufunuliwa kwa ulimwengu. Lakini kabla ya hapo, ni lazima iwe siri. Lakini kwa nini alifunua siri na kunitenda dhambi? Bwana alisikitishwa sana na hilo.


Siri hii inafunua uhalisia wa ibilisi. Kwa hiyo, kutakuwapo majaribu mengi njiani. Huna haja ya kulia. Kamweleze Mchungaji Kim haya niliyokwambia. Hasira ya kutisha ya Yesu iliendelea. Mchungaji Kim amefunua siri kwa mke wa mchungaji wa kanisa la karibu na sijui ni kwa nini amefanya dhambi hii. Kosa la Mchungaji Kim ni kubwa, lakini usilie. 


Yesu alitoa maelezo. Namna ambavyo kusanyiko linaomba kwa umoja na matukio yote yaliyotokea, yatapeleka mtikisiko mkubwa duniani kote. Ibilisi hataki uhalisia wake ujulikane kwa ulimwengu na anajaribu kwa nguvu kuuficha. Anaogopa kuwa mambo mliyoyaona yatamweka wazi yeye na malaika zake. Kama ukweli huu juu ya uwepo wake na namna alivyo utawekwa wazi kabla ya kitabu kutoka, mashambulizi ya shetani yataongezeka. Kwa hiyo, itabidi mvumilie matatizo zaidi. Hadi mambo yote kuhusu mikesha hii yawe yamerekodiwa ipasavyo, hii ni siri kabisa. nitawapa nafasi nyingine. Mchungaji Kim itabidi awe kwenye kuomba na kuandika kitabu. Pia, kila mmoja mwenye kipawa cha unabii ni lazima aache kwanza kuwaombea wengine.”


Yesu aliwakemea wachungaji na wake zao kwa ukali kutokana na kukosa kwao mwelekeo (focus). Kwa uthabiti, Yesu alisema, kuwa makanisa yote yaliyojengwa kwa Jina lake ni lazima yaweze kupata majibu ya tatizo lolote, hata kama ni kubwa kiasi gani, ndani yao wenyewe. “Kunapokuwa na tatizo, mchungaji na mke wake ni lazima waombe kwa kukubaliana na hakika jibu litatokea kutoka kwa Mungu. Wengi hawana uwezo wa kustahimili, wanaenda huku na kule, wakitafuta watu wenye vipawa vya unabii ili wawaombee. Kuwa wengi sana mlio namna hii na hilo linanisikitisha sana. Wake wa wachungaji wanaposaidia na kuomba pamoja na wachungaji wao, wakiwa wamepiga magoti madhabahuni mwa makanisa yao, Mungu atajibu maombi yao. Pia, kama umeomba na kumwachia Mungu mambo yako yako yote, basi ngoja, maana hiyo ndiyo imani ya kweli.”


Wakati wa ibada ya mchana, hata kama Mchungaji Kim angeendesha sifa kwa kumaanisha kiasi gani, au angehubiri kwa nguvu kiasi gani, Yesu alisimama pembeni ya madhabahu kimya huku akiwa amechukia. Mchungaji Kim aliendesha ibada huku jasho likimtoka usoni, lakini hasira ya Yesu haikuonekana kupungua. Mchungaji alionekana kama mtu aliyetelekezwa. Nilifanya maombi toka moyoni kabisa kwa Yesu, lakini alijibu kwa uthabiti kabisa kwamba, Njia pekee ni kwa Mchungaji Kim kuomba msamaha kwa moyo wa toba, na Baba yetu wa Mbinguni ataangalia na kuamua.”


Yesu alisema kwa mamlaka, “Kama mkifunua siri hii kwa watu, karama zote za rohoni mlizopewa zitaondolewa! Mchungaji Kim atatakiwa ajitenge na ndugu zake na marafiki zake na kujifungia kwa ajili ya maombi. Yesu aliomba kwamba Mchungaji ajihusishe zaidi na maombi na kurekodi kila kitu ambacho Bwana amemwonyesha, ili aweze kuchapisha kitabu hicho mapema.


Niliuliza, Yesu, vipi kama mke wa mchungaji toka kwenye lile kanisa jirani aliyekuja kwa Mchungaji Kim akirudi tena kwa Mchungaji Kim Jumapili mchana kwenye ibada na kwa ajili ya kuongea na kuomba? Mchungaji wetu ni mpole na hawezi kusema, hapana.” Bwana akasema kwa mamlaka, Mimi ni mganga wa kienyeji? Kwa nini unaniulizauliza kila mara kana kwamba mimi ni mbashiri? Kwa wachungaji na wake zao akasema, Ni lazima mjibidishe kuomba, kunitafuta na kunililia. Ndipo nitawajibu. Sijui kwa nini mnarukaruka toka sehemu moja kwenda nyingine mkitafuta majibu! Alikuwa hana furaha kabisa juu ya hili. 

No comments:

Post a Comment