Friday, December 21, 2012

Maswali kwa Maalim Moses na Ndugu Hamudi




Nawashukuru ndugu Hamudi na Maalim Moses kwa majibu na maswali yenu kuhusu makala yangu ya Ndugu Waislamu Nisaidieni. Mimi naamini lengo letu sote ni kumtafuta na kumtii Mungu wetu aliyetuumba, huku tukiwa na imani kuwa, mwisho wa safari ya maisha haya tutafika kwake mbinguni. Hata hivyo, leo ninayo maswali mengine kwao na kwa Waislamu wengine.




Mimi naamini kuwa njia pekee ya kufika mbinguni ni Yesu Kristo tu. Kwa msingi huo, ningependa kuona kuwa si Waislamu tu, bali hata wanadamu wote wanatambua kuwa Kristo ndiye Mwokozi wetu ambaye pia ni njia ya kufika mbinguni.


Katika kutekeleza kusudi hilo, ninakutana na changamoto mbalimbali kutoka kwa watu kama akina Hamudi na Maalim Moses. Na mimi ninafurahi kwa kuwa zinanifanya nifikirie kwa undani juu ya kile ninachokiamini – maana kuna maswali mengine ni mazito kwelikweli! Bila shaka Hamudi na Maalim Moses nao wangependa watu wote tuwe Waislamu kwa kuwa wao nao wanaamini kuwa Uislamu ndiyo njia pekee ya kufika mbinguni.


Hamudi na Maalim Moses hawako hapa kuhubiri Ukristo. Vivyo hivyo nami siko hapa kuhubiri Uislamu. Lakini kwa kuwa kila mmoja wetu anaamini kuwa mwenzake hayuko sawa, ndiyo maana tunajaribu kuitana ili sote tuende mbinguni. Maana mimi najiuliza, kwa nini Hamudi na Maalim Moses wapotee ilhali mimi niko hapa naujua ukweli? Naamini na wao nao wanafikiri hivyo hivyo.


Hoja tunazowekeana ndizo sasa zinazofungua ufahamu wetu, na zinamfanya mtu aone kibinafsi kuwa, “Ahaa, kumbe hii ndiyo kweli niliyokuwa naitafuta!!” Maana ukweli unapokuwa dhahiri, hata ukibisha kwa nje, moyo wako utasema tu, “Japo nabisha, lakini kwa kweli niko nje kabisa ya ukweli wenyewe.”


Kwa mantiki hiyo, katika makala haya ninayo maswali kadhaa ambayo si tu yanatupatia ufahamu juu ya imani zetu, lakini pia yanatuwezesha kutafuta majibu yanayohusu hatima zetu – si hatima za maisha ya duniani bali ni hatima za roho zetu, yaani yanatusaidia kujibu swali kuu: “Hivi ni kweli naenda mbinguni au naenda jehanamu MILELE?”


Yafuatayo ndiyo maswali yangu kwa Hamudi, kwa Maalim Moses na kwa Waislamu wote:

1.      Adamu na Hawa walifukuzwa kwenye Bustani ya Edeni kutokana na dhambi. Sisi pia tulio uzao wao ni wenye dhambi? Suluhisho la tatizo hili ni moja tu kulingana na Biblia – Yesu Kristo alikufa msalabani na kufanyika sadaka au dhabihu ili sisi tusiendelee kuchinja wanyama kila siku kwa ajili ya dhambi zetu kama torati inavyosema, badala yake tuamini TU katika sadaka ya Yesu na kupokea msamaha wa dhambi na wokovu wa Mungu bure.


Waislamu hamumwamini Yesu Kristo kama mwokozi aliyefia dhambi za wanadamu wote. Je, suluhisho la dhambi kwa mwanadamu ni nini? Kwa maana nyingine, ninyi Waislamu mtaponaje na jehanamu ya moto ilhali ni wazi kuwa ninyi, kama ilivyo kwa kila mwanadamu, mna dhambi ambazo ndizo hizohizo zilimtenga Adamu na Mungu?

2. Biblia inasema: Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. (1 Yohana 1:8-9). Kwa hiyo mimi Mkristo nikijikuta nimetenda dhambi nakwenda mwenyewe kwa Bwana Yesu na kumwambia, “Bwana wangu, nimesema uongo, nimeiba, nimetukana, nimetamani, … n.k. naomba unisamehe.” Sisubiri hadi mchungaji au mtu mwingine anikamate kwenye kosa kama polisi wanavyokamata wahalifu.


Ninyi Waislamu mnasema kuwa torati ndiyo njia sahihi ya maisha ya mwanadamu, kwamba mtu akifanya makosa ni lazima aadhibiwe kama vile kupigwa mawe, kuchapwa viboko, kukatwa mikono, n.k. 


Watalebani wakimchapa viboko mkosaji

Swali ni kuwa, kwa nini hatusikii Waislamu wakijipeleka wenyewe kupokea adhabu hizo baada ya kufanya dhambi? Hatujawahi kusikia Mwislamu ameenda kusema, “Jamani nimezini kwa hiyo nimekuja mnipige mawe; Nimeiba, hivyo nimekuja mnikate mkono.” Kwa nini wanaoadhibiwa ni wale TU wanaokamatwa? Mnataka kutuambia kuwa wakosaji ni hao tu? Kama unaamini kuwa mzinzi ni lazima apigwe mawe, si uende ukaombe wakupige mawe baada ya kuzini. Kwa nini hamfanyi hivyo?


3.      Huenda katika swali la hapo juu utajitetea kwa kusema huendi kwa sababu hujakamatwa (ingawaje Mungu tayari anakuwa ameshakukamata). Sasa, mbona hatusikii mkiwapiga viboko mia, au kuwakata mikono watoto wenu wenyewe kwenye familia zenu pale wanapoiba mboga au fedha nyumbani?


Bila shaka wizi ni wizi tu hata kama aliyeufanya ni mtoto. Ndiyo maana huwa tunawachapa viboko kwa namna ya kawaida isiyo ya kidini. Kwa nini basi sheria za kiislamu zinakuwa sahihi pale zinapohusu tu watoto wa wengine?


4.      Hivi ni mwanadamu gani anayeweza kusema kuwa anaweza akae japo siku moja bila kutenda dhambi? Au hata nusu siku? Au hata saa moja tu? Hivi kuna mtu anaweza kuoga mara moja kwa mwezi halafu akabaki safi kwa mwezi huo mzima? Mimi naamini hilo haliwezekani. Ukitaka kuwa safi ni lazima uoge kila siku. Sasa, kama ambavyo jasho, vumbi na harufu mbaya ni uchafu wa mwili, je, dhambi si ndiyo uchafu wa roho? Na kama dhambi ni uchafu wa roho, “logic” ya ninyi Waislamu kuwa na mwezi mmoja wa toba ni nini? Unawezaje kutubu kwa mwezi mmoja halafu eti uwe safi mwaka mzima?


5.  Bila shaka ninyi mnaamini kabisa kuwa Uislamu ni dini inayowapeleka mbinguni. Pili, mnaamini kuwa mtu akijitoa muhanga kuua makafiri (yaani akifa huku anatetea dini ya Mwenyezi Mungu), anakwenda peponi moja kwa moja.


Na bila shaka mnaamini kuwa wale makafiri wanaouawa na mwislamu kama huyo wanakwenda motoni, maana hata hivyo, wao si ni maadui wa Allah na dini yake?


Tuchukulie kuwa una watoto watatu – Amri, Hemedi na Sauda. Amri anakuja kwako na kusema, “Baba, Hemedi na Sauda wamekataa kufua nguo kama ulivyosema. Kwa hiyo nimewaua.”


Hivi, ni mwislamu gani atakayesema, “Safi sana mwanangu. Wewe ndiye unayefaa kabisa kuwa mwanangu.”


Mungu ameumba waislamu pamoja na makafiri ambao “hawataki kufua” – yaani hawataki kushika dini yake. Lakini kuna waislamu leo wanatarajia kuwa baada ya kufa, labda watamwendea Mungu huyu aliyewaumba wanadamu wote, na kusema, “Baba, nimeua makafiri mia moja kwa sababu walikuwa hawataki kufuata dini yako” – ambao maana yake ni kuwa hao mia moja wameenda jehanamu ya moto.


Kwa maneno mengine, mwislamu huyu anachomwambia Mungu hapo ni hiki: “Baba, nifungulie mlango wa pepo mimi kiumbe wako mmoja maana nimepeleka viumbe wako mia moja jehanamu.”


Swali ni kwamba: Inawezekanaje wewe ukaenda mbinguni kutokana na kupeleka wengine jehanamu? Tena wale mia moja ni watoto wa baba yuleyule unayemwomba akufungulie mlango wa mbingu!


6.      Kama Mungu aliumba mbingu na nchi na kila kitu kwa neno lake tu, iweje leo neno lake hilohilo lishindwe kubadili tabia tu za watu hadi Uislamu ulazimishe kwa nguvu ya upanga kuliingiza neno hilo ndani ya wanadamu? Kwa nini nchi za Kiislamu kama vile Iran, Saudi Arabia, n.k. zina polisi na mahakama kwa ajili ya kuzuia watu kutenda dhambi!!!!! Yaani polisi wanapita huku na kule kuhakikisha watu hawazini, hawalewi, n.k. Ajabu mno! Hivi ni kweli Allah anaweza kusema kwa ujasiri kwamba watu katika nchi hizo wanampenda? Si kwamba watu kama hao wanaogopa tu polisi na mahakama? 


   Hata hivyo, wanachofanya polisi ni kuzuia watu kutenda dhambi kwa nje. Je, moyoni inakuwaje? Au hamjui kwamba wizi, uzinzi n.k. haukai mwilini bali moyoni? Maskini wee! Mbona Mungu wenu kawaacha mnahangaika peke yenu? Mnahangaika kutafuta waumini kwa kutumia upanga! Mkishawapata mnahangaika kuwalinda kwa polisi na mahakama ili wasitoke! Mnahangaika kuzuia dini zingine kuhubiriwa kwenye nchi za Kiislamu ili watu wasijui ukweli utakaowafanya wauache Uislamu! Kweli ndugu zangu mnatia huruma kupita kiasi.


7.      Kama Uislamu ungekuwa na neno la kweli, kwa nini nchi za kiislamu zinaogopa na kupiga vita kabisa Ukristo kuhubiriwa humo? Je, hii si ishara kuwa mnafahamu kuwa watu watajua kweli ambazo zitawafanya waukimbie Uislamu?


Natumaini ndugu zangu Hamudi na Maalim Moses na Waislamu wengine mtanisaidia kupata majibu ya maswali haya. Nawaalika mpokee wokovu wa Yesu Kristo kungali mapema, maana mlango wa wokovu utafika mahali utafungwa na wale wote ambao watakuwa wako nje, kama ilivyokuwa wakati wa Nuhu, gharika itawakumba. Na gharika ya sasa si ya maji, bali ni ya moto. Bwana Yesu akubariki ndugu msomaji.

2 comments:

  1. rafiki yangu mzanzibari aliniambia mtume alisema vita vya kueneza uislam vimeisha, jihad iliyobaki ni mtu kupigana vita vya jihad ndani ya nafsi yake mwenyewe yaani mtu kupigana vita vya kuushinda mwili na nafsi yake dhidi ya matendo maovu.KAMA KWELI HAYO NI MANENO NA MAAGIZO YA MTUME MOHAMAD KIPENZI CHA WAISLAMU, HAKIKA MTUME HANA MFUASI HATA MMOJA! inasikitisha sana waislamu si wafuasi wa mtume wala si wafuasi wa YESU. kwa maneno mengine kulingana na maagizo hayo hapo juu ya mtume mohamad kipenzi cha waislamu,siku ya hukumu atawaambia ingawa niliwaagiza katika mafundisho yangu ya mwanzo kuwa mchukie adui zenu, mkate wezi mikono, wazinzi wapigwe mawe na mpigane jihad kwa ajili ya dini ya allah LAKINI MWISHO NILIWAAMBIA JIHAD IMEISHA JIHAD IMEBAKIA KWAKO MWENYEWE DHIDI YA NAFSI NA MWILI WAKO( yaani hakuna tena chuki dhidi ya wasiokuwa waislamu, hakuna kutetea dini ya allah, kukata watu mikono n.k) sasa ndugu zangu waislamu kwa muhamad kipenzi chenu hampo, kwa yesu hampo! mpo wapi? mmeamriwa kuwalinda na kuwahami wasiokuwa waislamu, kutokuharibu makanisa wala kuiba au kuchukua kwa nguvu mali ya kanisa na masinagogi. ni kwamba hamsomi QURAN au mnasoma QURAN nyingine tofauti na ile niliyoisoma? ( siku ya sabasaba ktk banda la wahamadiya), nilipowauliza kwa upole kwanini waislamu wanachoma makanisa kwa kigezo cha kuitetea dini ya allah, nao vijana wawili waliokuwepo wakanifungulia sura ( nimeisahau) niligutuka sana kwani niliyoyasoma ni kinyume 100% na imani na matendo ya waislamu. mwisho wakaniambia wao wahamadia wanafuata mafundisho ya muhamed ndio maana hawasapoti mambo yanayoshabikiwa na waislamu wengine na ndio maana waislamu wengine wanawakataa wahamadia .kwamba wao wanapigania ustawi wa jamii kama vile kufadhili na kujenga miradi ya maji, hospital, shule, misikiti n.k. kwa misingi hii huenda wahamadia ndio waislamu wengine hawa ni wafuasi wa dini iliyojificha ndani ya uislamu lakini si uislamu. --castor

    ReplyDelete
  2. 54 inasema siku kazaa lakini 69 inataja kwa idadi kabisa

    ReplyDelete