Sunday, December 15, 2013

Asili hasa ya Uislamu ni nini?




Je, wewe ni Mkristo? Je, wewe ni Mwislamu? Sote tuko kwenye safari ya kuelekea mbinguni huku tukiamini kuwa njia ile tuliyomo ndiyo sahihi; na njia ile waliyomo walio kinyume nasi haiko sahihi.

Ukristo na Uislamu ni dini kubwa ambazo zinadai kuwa zinaabudu Mungu mmoja aliyeumba mbingu na nchi tofauti na dini zingine ambazo zinaabudu miungu mingi. Hata hivyo, zipo tofauti za msingi sana kati ya Uislamu na Ukristo ambazo KATU haziwezi kufanya pande hizi mbili ziwe zote sahihi. Kwa mfano:
  • Ukristo unaamini kuwa Yesu ni Mungu na Uislamu unaamini kuwa Yesu si Mungu. Haiwezekani kamwe Ukristo ukawa sahihi katika hili na Uislamu ukawa sahihi katika hili. Ni lazima uwe ni upande mmoja TU ulio sahihi katika jambo hili.

Hali ni hiihii katika mambo mengine mengi. Kwa mfano:
  • Ukristo hauamini hata kidogo kwamba Muhammad ni mtume wa Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo; lakini Uislamu unaamini hivyo.
  • Ukristo unaamini kwamba Yesu alikufa na kufufuka; lakini Uislamu hauamini kwamba Yesu alikufa na kufufuka.
  • Ukristo hauamini kuwa kuna Mwislamu YEYOTE atakayekwenda mbinguni kwa kupitia imani ya Uislamu; lakini Uislamu unaamini hivyo; n.k., n.k.

Kwa kuwa haiwezekani pande zote mbili zikawa sahihi, lazima kuna upande uliodanganywa; na Biblia ilishaonya tangu karne nyingi kabla kwamba yuko Ibilisi audanganye ulimwengu wote. (Ufunuo 12:9).

Je, asili ya Uislamu ni nini? Hata kama wewe ni Mkristo, ni muhimu kuyajua haya maana tunao ndugu zetu wengi walio upande wa pili. Ndugu zetu hawa si kwamba hawataki kwenda mbinguni; la hasha! Mbingu wanaitaka sana. Tena wapo wengi walio na juhudi kubwa kuliko hata sisi tulio Wakristo. Lakini juhudi na nia njema huwa si jibu na suluhisho la shida yoyote. Ni lazima hizi zichanganywe na maarifa sahihi.

Hata Waswahili wanasema: Penye nia pana njia. Lakini kama una nia ya kwenda mji ulio kaskazini lakini ukapanda gari inayokwenda magharibi ni vigumu sana kufikia lengo. Nia ya kweli ni LAZIMA iungane na maarifa ya kweli!

Uislamu umetokea wapi? Tafadhali weka maarifa haya kwenye blog yako; kwenye facebook; kwenye tweeter; n.k.; huwezi kujua utasababisha wokovu kwa nani.

Bofya HAPA ili kufahamu zaidi.

No comments:

Post a Comment