Wednesday, March 21, 2018

Kubatizwa kwa Moto Uwakao - 12


==== SIKU YA 21 ====
Kim, Joo-Eun:
Nilikuwa kwenye moto, nikiomba kwa kunena. Madragoni (mazimwi) matatu ya kutisha yakatokea. Dragoni la kwanza lilikuwa na michoro mingi na maumbo ya duara kwenye mwili wake wote mwekundu. Dragoni la pili lilikuwa na mistari myekundu na buluu ya wima iliyochanganywa pamoja kiasi kwamba ilinifanya kuchanganyikiwa nilipoitazama. Dragoni la tatu lilikuwa na mistari ya buluu na njano ya ulalo iliyochanganywa pamoja. Yalikuja kama vile yanataka kunimeza mzimamzima, lakini nilipaza sauti mara tatu kwa uthabiti, “Kwa Jina la Yesu, ondokeni kwangu!” Yakakimbia.


Nilipoangaza angaza macho, nikaona mapepo yaliyokuwa yamekaa kwenye duara yakijadiliana jambo. Kiongozi wao akaliambia pepo mojawapo lililokuwa kipara, “Wewe, safari hii utaenda kujaribu!” Kwa haraka lilikuja kwangu, lakini kama ilivyokua mwanzo, nilikamata kichwa chake na kukivuta huku na kule. Nikatoboa macho yake, likakimbia. Kisha pepo lenye vidole kama mkasi likanijia. Lilikuwa linakwaruza ubao. Sauti iliyokuwa inatoka sikuweza kuivumilia. Kwa hiyo nikalivunja vidole vyake na kuliparua usoni kwa vidole hivyo. Likasema, “Wewe, nirudishie vidole vyangu! Kwa nini unachukua vidole vyangu? We kisumbufu kidogo, usinichezee! Kwa nini imani yako imekua kiasi hiki?” Baada ya kusema hivyo, likatoweka.

Niliendelea kuomba kwa nguvu. Joka kubwa lilitambaa kuelekea kwangu huku lionyesha uso wa hasira. Magamba yake yalibadilika rangi mbalimbali na lilikuwa linaleta na kuondoa mkia wake karibu na mimi. Nililikamata na kulitupia ukutani. (Marko 16:17,19)

Kisha pepo jingine lilitokea ambalo lilikuwa limefungwa bandeji mwili mzima. Lilinifanya nikumbuke katuni ya kichina inayoonyesha pepo aitwaye ‘Kang-She.’ Likasema, “Tazama we mtoto, hii inafurahisha kwelikweli!” Likaanza kufungua zile bandeji. Chini ya bandeji kulikuwa na wadudu wengi, majongoo na matandu yalitambaa juu ya mwili wake wote. Huku nikiwa nimesikia kinyaa sana, kwa haraka nilimwita Yesu, na akatokea. Akalikamata lile pepo na kulitupa chini. “Yesu asante sana!” nilisema. Akatabasamu na kupapasa kichwa changu taratibu. “Mpendwa wangu Ufuta, imani yako imeongezeka sana! Omba kwa bidii.” Leo Yesu alikuwa amevaa vazi maalum la dhahabu lenye moyo mwekundu kifuani mwake unaotoa rangi mbalimbali.

Baada ya Yesu kuondoka, pepo lililojifanya kama bibi kizee, lilitokea. Lilikuwa limevaa nguo nyeusi na kushikilia shoka refu. “Acha kuomba! Utaomba wakati mwingine. Si lazima uombe leo, sawa? Kwa nini umeng’ang’ania kuomba leo? Omba kesho. Yesu atakutana na wewe ukiomba kesho. Fanya hivyo. Likarudia kusema hivyo kwa sauti zaidi. Kwa hiyo na mimi nikaliambia kwa sauti, “We kizee mwenye sura mbaya, kwa Jina la Yesu, ondoka kwangu!” Likatoweka.

Lee, Yoo-Kyung:
Wakati nikiomba, pepo moja lilinijia na kusema, “Wewe! Hivi hujui kuwa unatakiwa kuniomba msamaha?” Sikuamini kile nilichokisikia. Kwa hiyo, nikalikamata na kulizaba kibao usoni. Lakini na lenyewe likanizaba kibao usoni kwangu, huku likisema, “Unathubutu kunipiga kofi? Njoo hapa. Nitakuua!” Nilikuwa nimejawa na hasira. Kwa hiyo, nikayang’oa macho yake na kuyatupa chini. Shavu langu likaanza kuvimba na sikuweza kusahau jinsi kujisahau kidogo tu kulivyosababisha mimi nikazabwa kibao na yule pepo.


Muda mfupi baadaye, pepo la kike lililovaa vazi jeupe lilitokea. Lilikuwa linalia machozi. “Hii si sawa kabisa! Mwanaharamu yule, Haak-Sung, amenipiga na kile kijitu kisumbufu, Joo-Eun, nacho kimenipigapiga!” Nikalisubiri lifike karibu kisha nikang’oa macho yake kwa vidole vyangu. Likarukaruka kwa maumivu na likakimbia. Pepo jingine la kike likasema, “Wewe, unadhani utabaki salama kwa haya unayotufanyia?” Nikashika nywele zake, nikalizungusha kisha nikalitupilia mbali nami. Nikasema, “Yesu nipe shoka.” Kwa kutumia shoka, nikakata kichwa cha pepo yule na kukipasua. Huku kichwa chake kikiwa kimekatika, likanijia na kusema kwa sauti, “Wewe, hata husikii huruma kwangu?” Likawa linazunguka likitafuta kilipo kile kichwa chake, huku likisema, “Kichwa changu kiko wapi? Uso wangu uko wapi?”

Baadaye, nilitaka kumwona Yesu. Nikamwita kwa nguvu zangu zote, “Baba! Baba!” Yesu akanisalimia kwa tabasamu pana, “Mpendwa wangu Ufuta, umefanya vizuri sana. Yoo-Kyung wangu anaweza peke yake kuyashinda mapepo kikamilifu kabisa.” Pia akasema, “Yoo-Kyung, Mchungaji Kim atakapokuita, ‘Sesame’ (Ufuta) wakati wa ibada, uitike kwa nguvu kabisa. Kuitika kwa nguvu nayo ni imani. Umenielewa?” Nikasema, “Ndiyo, Bwana. Amen.”

Baada ya muda mfupi, baadhi ya malaika walikuja, wakasema, “Dada Yoo-Kyung, umeyashinda mapepo. Wewe si wa kawaida. Songa mbele! Na mapepo yakikushambulia tena, uyashinde tena kama ulivyofanya hadi sasa!” Wote wakanishangilia. Yesu alinichukua kwenda kutembelea Mbinguni. Nilipofika pale, Yae-Ji na mimi tulianza kucheza mbele za Bwana. Tukamwomba “Bwana, tafadhali mimina machozi ya toba kwa Shemasi Shin Sung-Kyun, na Joseph. Wote wawili wanatamani kuomba sala ya toba kwa machozi lakini hawawezi kulia.” Lakini Bwana akajibu, “Naweza tu kutoa machozi ya toba kama watu wanaomba kwa moyo kabisa kwa toba kwa mioyo yao.” Tulisindikizwa kurudi hadi Kanisani. Yesu aligusa shavu langu nilikokuwa nimezabwa kibao na yule pepo na akasema, “Mpendwa Yoo-Kyung, uwe imara. Umeelewa?” Kisha akapunga mkono na kutoweka.

Lee, Haak-Sung: * Pepo lenye msumeno wa mnyororo
Wakati nikiomba kwa kunena, mapepo matatu yalinivamia kwa mara moja. Moja lilikuwa na uso wa binadamu na mwili wa dragoni. Jingine lilikuwa ni mifupa tu. Na la tatu lilikuwa limevaa kinyago cha chuma. Cha ajabu, lilikuwa limebeba msumeno mkubwa wa mnyororo (chainsaw) na lilijaribu kukata mikono yangu. Ilinibidi niwe makini sana. Kama ningepoteza uzingativu wangu hata kwa sekunde moja, lile pepo lingenikata. Sikuwa tayari kupoteza. Kwa hiyo, nilikwepa na kukimbia mashambulizi. Kisha wakati wa kushambuliana, nililipokonya ule msumeno na nikalifyeka mikono yake. Likawa linapiga kelele huku yale mengine mawili yakanikimbia.

Baadaye, pepo jingine lilinijia. Nikalidanganya linisogelee kwa kuliambia, “Wewe, njoo hapa nikufundishe jambo la kufurahisha. Njoo huku! Fanya haraka!” Pepo lile likawa na wasiwasi na likagoma kuja. “Wewe! Kweli nina kitu kizuri cha kufurahisha kwa ajili yako. Njoo uone!” nikasema, lakini bado halikuniamini. Likaniuliza, “Unaahidi kuwa hautaniadhibu?” Nikajibu, “Kwa nini nikuadhibu? Nilitaka tu kukuonyesha jambo la kufurahisha. Kwa hiyo njoo hapa. Likaja karibu nami huku likiwa limechangamka. Lilipokuwa karibu, nikakamata mkono wake na kuanza kulizungusha hewani, kisha nikalitupa likajibamiza ukutani.

Baadaye kidogo, nikasikia sauti kubwa za miguu inayotembea kama ya kikosi cha askari. Ilikuwa kama mamia ya miguu ikitembea kwa pamoja. Mara nikaona kundi kubwa la mapepo likinijia, yote yakiwa yamevalia sare za kijeshi. Nilijua kuwa mapepo yanayokuja kunishambulia yalikuwa yakiendelea kuwa yenye nguvu zaidi kuliko yaliyotangulia. Lakini nilipotaja Jina la Yesu, yote yakatoweka.


Kim, Yong-Doo: * Mikono yote iligeuzwa kama keki iliyopinda (pretzel)
Nilikuwa nikimlilia Bwana huku mikono yangu ikiwa imeinuliwa juu kwa takribani dakika 30. Mikono yangu ilianza kuzunguka tena na tena. Mkono wangu wa kushoto ulianza kujisogeza kutokea ndani kwenda nje, ukifuatiwa na mkono wangu wa kulia, nao ukifanya kama wa kushoto. Ghafla, mikono yote ikaanza kujinyonga kuelekea nje kama keki iliyopinda na ikabakia kwenye mkao huo. Ulikuwa ni mkao mbaya na wenye mateso na mgumu kustahimili. Kisha mikono yangu kila mmoja ukaanza kujinyonga kuelekea upande tofauti na mwingine, kutokea nje kuja ndani; ndani ya dakika moja tena. Kwanza mkono wangu wa kushoto, kisha wa kulia. Halafu nikabakia kwenye mkao huo nao kwa dakika 30 zingine.  Kwa sababu jambo hilo lilikuwa linatendeka polepole, nilikosa uvumilivu na nikaanza kuingiwa na hasira.

Nikalalamika, “Bwana, kwa nini unanifanya niteseke kiasi hiki? Kama utanigeuza ndani nje, basi bora ufanye haraka. Mbona kama unacheza nami? Unanifanyia nini hiki sasa? Nimechoka. Si itakuwa bora kwetu sote kama utanipa mara moja hicho ninachotaka?” Nikaanza kumshambulia Bwana kwa malalamiko yangu, “Bwana, kama ungenipiga tu kwa moto wako Mtakatifu na kufungua macho yangu ya kiroho, si itakuwa bora kwa upande wako na wangu?  Nani ataweza kupokea vipawa vya rohoni kama utafanya mambo kuwa magumu kiasi hiki?”

Niliomba na kudai vipawa vya rohoni.  Nililia, nilipiga kelele kwa nguvu zangu zote. Lakini Bwana aliendelea kurudia kazi za Roho Mtakatifu kupitia kunyonga mikono yangu. Alifanya hivi mara nyingi. Nikawaza, “Hivi anataka kunipa vipawa gani hasa vya rohoni? Hii ni aina gani ya vipawa jamani?” Nilikuwa nimekereka sana na nilitamani jambo lile lingefanyika kwa haraka. Lakini Bwana wala hakuwa na haraka kama mimi. Badala yake, nilikerwa na mwendo wake wa polepole.


Ilikuwa ni takribani saa nne baadaye, ndipo kunyonga kwa mikono yangu kulipokoma na ikaanza kusogea kuanzia mbele kwenda nyuma. Nilijaribu kwa kila njia kuituliza mikono yangu, lakini kule kutetemeka kwake kuliendelea.  Kwa kweli, ilikuwa inachekesha. Niliambiwa kupitia unabii kuwa nilikuwa kwenye mchakato wa kupokea kipawa cha uponyaji na nguvu ya miujiza.

Dada Baek Bong-Nyo: * Ziara nyingine Kuzimu
Nilikuwa nafurahia uchezaji wa kiroho na kuomba kwa kunena. Malaika kumi walishuka kutoka Mbinguni ili kunichukua hadi kwa Yesu. Nilipofikishwa kwa Yesu, alisema, “Mpendwa wangu Bong-Nyo, kama unavyojua, mchungaji wako Kim anaandika kitabu juu ya Mbinguni na Kuzimu. Ningependa kumchukua Mchungaji Kim pamoja nami hadi Kuzimu na kumwonyesha kile anachotakiwa kuandika kuhusina na Kuzimu, lakini macho yake ya rohoni hayajafunguka bado. Sina namna ila kukuchukua wewe, ili kuwezesha kuandikwa kwa usahihi mambo ya Kuzimu. Wewe peke yako ndio ninaweza kukupeleka kule. Kwa hiyo nakuomba uvumilie kwa muda kidogo. Haya twende tukatembelee Kuzimu pamoja.”

Mara tulikuwa tunatembea kwenye barabara ya Kuzimu. Harufu mbaya ya nyama zilizooza ilifanya tumbo langu livurugike na kulikuwa na giza lisilo na mwisho. Nilishikilia kwa nguvu mkono wa Bwana. Kule Kuzimu, kuna mateso tu milele. Tulifika mahali ambapo watu waliokuwa kwenye shimo lenye moto walikuwa wakilia na kuomba msaada. Moto ulikuwa mkali sana. Kulikuwa na watu wengi wasio na idadi, wote wakiwa uchi, wakirukaruka na kupiga kelele ndani ya pipa kubwa sana. Nikamwona baba yangu tena. Alianza kulia, “Bong-Nyo, unafanya nini hapa? Siwezi kuvumilia maumivu ya moyo kila wakati ninapokuona. Nisamehe sana kwa yote niliyokutendea. Nadhani hiyo ndiyo sababu niko hapa nikilipia yale niliyotenda.” Sikuweza kusema neno lolote, lakini nililia tu mfululizo. Maumivu yaliyoko Kuzimu ni makubwa mno kuliko mateso ambayo baba yangu alinisababishia duniani. Kile kilichonipata duniani kilikuwa si lolote si chochote.

Pepo moja kubwa lilikuwa linafurahia kuwakatakata watu kwa fyekeo kubwa (scythe). Lilikuwa linaimba na kuimba. Lilimnyakua baba yangu na kuanza kumkatakata, kama ambavyo tunakatakata chakula cha tambi nyumbani. “Ahhhh! Tafadhali niokoe! Naomba! Tafadhali niueni tu!” Vilio vya maumivu na mateso vya baba yangu vilinifanya nizimie. Bila ya kuwapo Bwana karibu yangu, ningezimia mara nyingi tu. Hakuna mwisho wa mateso kule Kuzimu. Unakuwa umelaaniwa kwa majuto ya milele. Hakuna tena matumaini. Njia pekee ya kuepuka kwenda Kuzimu ni kumpokea Yesu kama Mwokozi wako na kuishi kwa uaminifu.

Tuliendelea mbele, huku tukiacha nyuma vilio vya maumivu makali vya baba yangu. Baada ya kutembea kwa muda, niliona mti mbele yangu. Nilipofika karibu, nikamwona mama yangu, mdogo wangu wa kiume, shemeji yangu na mpwa wangu, wote wakiwa uchi, huku wakiwa wamening’inizwa mtini kwa vifundo vya miguu yao. Pembeni yao kulikuwa na pepo lililokuwa refu kuliko mlima. Nilimtazama mama yangu na yeye akaniona, huku akiwa kaning’inia mtini. Wengine nao waliniona na kuanza kunililia. “Bong-Nyo, kwa nini uko hapa kama huwezi kutusaidia? Kwa nini umekuja tena? Je, unapenda kuniona nikiwa kwenye mateso kiasi hiki?”

Yesu akaniambia kuwa pepo lile lilikuwa ni la pili kwa ukubwa kule Kuzimu. Lilikuwa linapenda kuwapiga watu na kubandua nyama za miili yao. Kisha linawatupa bila huruma motoni. Nilitamani nilichanechane! Lilimwamuru mmoja wa walio chini yake kuweka chombo kikubwa kilichojaa wadudu chini ya watu wa familia yangu. Wadudu hawa walikuwa kama funza, wakiwa na meno makali na macho yaliyong’aa sana. Walipanda hadi kwa wale ndugu zangu na kuanza kuwatafuna nyama za miili yao bila huruma. Walichimba kote kwenye miili yao, hata macho na pua zao. Nikawasikia wote wakilia, “Ahhhh! Tafadhali niokoe! Bong-Nyo! Dada mkubwa! Aaaa! Shemeji! Tafadhali niokoe! Shangazi! Tafadhali nisaidie!” Mara nyama yote ikawa imekwisha na wale wadudu wakaendelea kuchimba hata ndani ya mifupa yao. Moyo wangu uliumia sana kujua kwamba hali hii ingeendelea milele. Pamoja na kumwomba sana Yesu asaidie, alichoweza tu kusema ni, “Siwezi kufanya hivyo. Muda huo ulishapita!”

Yesu alinipeleka hadi kwenye mlima mkubwa sana. Niliona watu wamesimama kuuzunguka huku wakiwa wamekata tamaa. Walionekana wamechoka na wamevimba kutokana na kupigwa sana. Pembeni yao kulikuwa na pepo linalotisha, ambalo lilianza kunidhihaki, likisema, “Nakuona hapa mara kwa mara. Umefuata nini tena leo?” Nilijawa na hasira, nikaanza kulilaani, “Wewe, we ni mwanaharamu! Natamani nikuchane vipandevipande kama ulivyofanya kwa familia yangu, kisha nikutupe kwenye shimo la moto! Nitakupata tu!” Pepo lile likadhihaki kwa sauti hata zaidi, “Unalia kwa sababu unaniogopa. Hiyo inanifanya nifurahi! Utafanya nini sasa?” Nikasema, “Yesu, nataka kuliua pepo hilo. Nalichukia pepo hilo! Bwana, kwa nini umesimama tu na haufanyi lolote? Nionyeshe chochote!” Yesu alinyanyua mkono wake wa kulia na kuuzungusha. Mara moja mwili wa pepo lile ukapooza na halikuweza kusogea, kama nguzo ya jiwe. Mara watu wote walifunikwa na wadudu mbalimbali, ambao walikuwa wanakula nyama za miili yao. Vilio vya watu wale vilirindima kwenye anga lote la Kuzimu.

* Kukutana na Rais aliyepita wa Korea
Tuliendelea mbele, na Yesu akasema, “Roho utakazokutana nazo sasa ni zile unazozifahamu sana, kwa hiyo tazama kwa makini.” Nikamwona rais aliyepita wa Korea. Kulikuwa na joka kubwa jeupe limemviringa mwili wake na nyoka wengine kadhaa wa rangi mbalimbali walikuwa juu yake.  Alisema, “Ahhh! Acheni kunikosesha pumzi! Tafadhali acheni! Niokoe tafadhali!” Lakini licha ya maumivu yale makali, alianza kuongea na mimi akisema, “Wewe ni nani? Kwa nini uko hapa? Mimi nilikuwa rais wa Korea, nikiwa na hadhi zote, lakini sasa ninateseka hapa Kuzimu. Wachungaji wengi walijaribu kunishauri niende kanisani, lakini niliwapuuza wote. Nilipuuza kile walichonieleza kuhusu Kuzimu na sikuwahi kudhania kuwa kuna sehemu kama hiyo. Mwanangu bado hamjui Yesu na nina wasiwasi sana juu ya hilo. Mwanangu anatakiwa amkubali Yesu akiwa bado yuko hai na apokee wokovu ili aje aishi Mbinguni. Natamani ningeweza kwenda sasa na kumweleza mwanangu ukweli huu.    Lakini siwezi. Sasa nifanyeje? Ahhh! Moyo wangu unauma sana. Alimwomba Yesu, lakini Yesu alimsikiliza tu bila kusema neno lolote.

No comments:

Post a Comment