Namna ya Kupakua
Bofya kwenye picha ya jalada la e-book unayotaka. Kisha utafunguka ukurasa wenye kitabu hicho. Humo utaona kwenye kona ya juu kulia, maneno "Download" au alama ya mshale inayotazama chini. Bofya hapo, na e-book itapakuliwa.
1. Jeshi la Mungu
Maandiko yanasema
kwamba, Mungu ameshatubariki kwa baraka zote za rohoni katika Kristo Yesu. Kwa nini
basi wengi wetu bado tunahangaika na maisha na kila kitu kinaonekana kuwa ni
kigumu?
Jipatie e-book hii iitwayo Jeshi la Mungu ili
uweze kuona ni nini kinatakiwa kufanywa nasi ili tuweze kumiliki baraka ambazo
Bwana mwenyewe alitununulia kwa kifo chake msalabani.
2. God's Worriors
Hiki ni kitabu kilekile cha namba 1, yaani Jeshi la Mungu, lakini kwa lugha ya Kiingereza. Ili kukipata, bofya HAPA.
Hiki ni kitabu kilekile cha namba 1, yaani Jeshi la Mungu, lakini kwa lugha ya Kiingereza. Ili kukipata, bofya HAPA.
3. Je,
sabato ni siku katika Juma?
Wengi wetu tumekuwa
tukichanganyikiwa na swali hili. Kama maandiko yanasema kuwa Kristo ni mwisho
wa sheria, je, sabato ambayo nayo ilikuwa ni sehemu ya sheria imeathiriwa vipi
na kuja kwa Bwana Yesu pamoja na Agano Jipya?
Unaweza kupata majibu
ya maswali haya pamoja na mengine yanayohusiana na sabato kwa kupakua e-book
hii iitwayo Je,
sabato ni siku katika Juma?.
4. Kuokoka
na Kuishi kwa Ushindi
Watu wengi wanasema
kwamba hakuna kuokoka duniani. Wanadai kwamba mtu ataokoka baada ya kufa. Je,
ukweli ni nini?
Jipatie e-book hii iitwayo Kuokoka
na Kuishi kwa Ushindi ili
uweze kujua ukweli wa jambo hili kutokana, si na maoni ya watu, bali na
maandiko, ili usije kuwa unashikilia mambo ambayo ni maagizo ya wanadamu badala
ya neno la Mungu aliye hai.
5. Kupata
Mwenzi Kibiblia
Je, umekuwa na shauku
ya kumpata mwenzi wa maisha yako? Bwana Yesu anasema kwamba kila mtu na awe na
mke wake; na mume wake. Kuwa na mwenzi ni jambo la kimungu na ni mapenzi ya
Mungu kila mwenye shauku hiyo apate hicho anachokitaka.
Unaweza kupata ushauri
na maelekezo ya kibiblia juu ya jambo hili kwa kupakua e-book hii iitwayo Kupata
Mwenzi Kibiblia.
6. Jiandae
Kukutana na Mungu Wako
Wako baadhi ya watu
ambao hawaamini kuwa kuna jehanamu ya moto au mbingu. Ushuhuda ufuatao ni wa
binti anayeitwa Angelica, ambaye Bwana Yesu alimpeleka jehanamu kisha mbinguni ili akajionee
mwenyewe kile ambacho Biblia inakisema.
Mbingu ni halisi na
jehanamu pia. Mbinguni ni kuzuri sana; lakini jehanamu ni kubaya mno. Pakua e-book
hii iitwayo Jiandae
Kukutana na Mungu Wako ili uweze kujua kile kinachoendelea katika ulimwengu wa roho; hatimaye
uweze kujiweka tayari kwa ujio wa nchi mpya na mbingu mpya.
7. Shetani Anavyozuia Maombi
Huu ni ushuhuda wenye nguvu sana wa kijana ambaye tangu tumboni mwa mama yake alikuwa ni ajenti wa ibilisi. Anaeleza jinsi ambavyo shetani anazuia maombi ya Wakristo kwenye anga ili yasimfkie Mungu. Pia, anaeleza jinsi ambavyo shetani anaiba yale majibu ya maombi ambayo Mungu amewatuma malaika wake wayapeleke kwa watu wanaoomba.
Kitabu hiki kinatufundisha nini cha kufanya ili kwamba tuweze kufanya vita vya kiroho kwa mafanikio, hivyo kupokea majibu ya maombi yetu kila wakati.
Kitabu hiki kinatufundisha nini cha kufanya ili kwamba tuweze kufanya vita vya kiroho kwa mafanikio, hivyo kupokea majibu ya maombi yetu kila wakati.
asante sana kwa vitabu hivi...mungu akubariki sana........
ReplyDeleteAmen. Ubarikiwe na wewe pia. Endelea kumtafuta Bwana Yesu kwa bidii.
ReplyDeleteUbarikiwe sana James John. Kwa kweli nimejifunza mengi sana. Mungu aendelee kukupa ufunuo zaidi. Amina!
DeleteYESU
ReplyDeleteHakuna blog iliyowahi kunibariki kama hii na hakika mtumishi ubarikiwe sana na MUNGU aendelee kukutumia zaidi na zaidi
ReplyDeleteAsante brother Michael. Ashukuriwe Mungu wetu na Jina lake lizidi kuinuliwa.
DeleteUbarikiwe sana mtumishi unayeendesha blog hii, imekuwa baraka sana kwangu. Mungu akuzidishie baraka mara nyingi
ReplyDeleteamen. ubarikiwe nawe pia
DeleteMungu akubariki mtumishi kwa kazi nzuri unayoifanya ya kutuwekea vitabu kwenye blog yako endelea hivyohivyo ili tuweze kujifunza mengi....
ReplyDeleteamen. Bwana Yesu akubariki nawe pia
DeleteHUDUMA YAKO NABARIKIWA SANA NAYO, MUNGU WA MBINGUNI AZIDI KUKUINUA MTUMISHI WAKE.
ReplyDeleteAmen. Na awewe pia ubarikiwe.
DeleteAmina sana...na barikiwa mno na kukua zaidi kiroho...endelea kutusaidia kwa vitabu vingine zaidi
ReplyDeleteAmen. Barikiwa pia
DeleteNdugu hata mimi nimebarikiwa na somo la sabato.
ReplyDelete