Tuesday, October 23, 2012

Majibu ya Ndugu Hamudi - Sehemu ya II



Katika sehemu hii ya pili, ninaendelea na kujibu maswali aliyouliza ndugu Hamudi kutokana na makala yangu niliyotoa katika blog hii yenye kichwa: Ndugu Waislamu Nisaidieni.

Kwa kuwa Bwana Hamudi aliuliza maswali mengi, nimeona ni vema niwe nayajibu kwa mafungu kulingana na yeye alivyoyaweka katika mafungu. Leo tutaangalia fungu la pili la maswali hayo.

Sunday, October 21, 2012

Majibu ya Ndugu Hamudi – Sehemu ya I





Katika blog hii kuna makala yanayosema “Ndugu Waislamu Nisaidieni.” Nashukuru kwamba ndugu Hamudi amejitokeza kujibu maswali yangu kadhaa niliyokuwa nimeuliza. Lakini pia, baada ya kufanya hivyo, ndugu Hamudi ameuliza maswali si machache. Nami nimeona kuwa niyaweke hapa pamoja na kile nilichojibu, kama makala ili kwamba, hata mtu mwingine anayependa kuchangia, afanye hivyo.

Ndugu Hamudi, asante tena kwa maswali yako yenye kutikisa akili na fahamu za mtu. Ni lazima nikiri kuwa haya ni maswali ambayo, hakika, kama hujui sawasawa kile unachokiamini, ni lazima ama utachanganyikiwa au utakimbia.

Sunday, October 14, 2012

Nilihisi kama Mungu Amenisaliti!




Utangulizi kutoka kwa blogger

Je, unahisi kuwa una huzuni kubwa isiyoweza kuondoka, umekata tama, unajiona huna maana, unahisi kama vile Mungu amekudanganya au amekuacha; unahisi kama vile  Mungu si wa kuaminiwa au Neno lake si la kuaminiwa, unahisi kuwa Mungu hasikii maombi yako, hakupendi; unahisi kwamba umeshapoteza wokovu wako, au unahisi kuwa umetenda sana dhambi kiasi kwamba Mungu hawezi kukusamehe tena?

Napenda nikuletee habari njema kwamba, bado liko tumaini, tena kubwa sana kwa ajili yako. Karibu usome ushuhuda huu ambao, si tu ni ushuhuda wa mpendwa aliyepita kwenye mapito kama hayo, lakini pia ni somo zuri mno kiasi kwamba, kama kawaida, Mungu anayo mengi ya kutufundisha kupitia mambo ambayo wengine walipitia kama sisi na wakashinda kwa neema ya Mungu ambayo iko kwa ajili ya kila mwanadamu, ukiwamo na wewe. Pendo la Mungu ni zaidi ya maji ya bahari, hivyo hakika kabisa unayo sehemu yako humo ambayo inakungoja uingie na kupokea.

Tuesday, October 9, 2012

Imam wa Msikiti Aokolewa na Yesu





Zak Gariba ni mtoto wa pili kuzaliwa katika familia yao. Kwa sababu ya kulitaja jina la Yesu msikitini, Zak Gariba, ambaye alikuwa ni imam alitupwa si tu nje ya msikiti, bali pia nje ya familia yake. Alikataliwa na kujikuta hana tena ndugu; na akapoteza kila kitu. Matokeo yake alifika mahali ambapo aliamua kujiua. Lakini Yesu Kristo mwenyewe alienda kugonga mlango wa nyumba yake na akayabadili kabisa maisha yake kutoka mautini na kumwingiza uzimani.

Wednesday, October 3, 2012

Jinsi Ibilisi Anavyozuia Maombi Yako


Ndugu msomaji wa blog hii, kati ya makala au masomo ambayo nimeyaandika humu, hili ni somo na ushuhuda mmojawapo wenye nguvu sana ambao, kila mwana wa Mungu atakayeusoma, atapata msukumo wa rohoni usio wa kawaida. Haya ni mafunuo yenye nguvu mno ambayo, hakika yatakuinua kwa kiwango cha juu sana nawe utamshukuru Mungu. Nilipouona ushuhuda huu kwenye mtandao, moyo wangu ulianza kuwaka niweze kuutafsiri harakaharaka na kuuweka kwenye blog hii ili yamkini uweze kuwafikia wapendwa wengi iwezekanavyo.