Wednesday, August 29, 2012

Ulinzi Kutoka kwa Waganga wa Kienyeji



Naamini umeshasikia mara kadhaa watu wakitaja kile kinachoitwa “sayansi ya kiafrika”. Kwa kifupi maneno haya yanaongelea kazi za waganga wa kienyeji. Ni wazi kuwa yanamaanisha upigaji ramli, uaguzi, usafishaji nyota, na hata ulozi na mengine kama hayo.

Siku hizi watu wengi wanakimbilia kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kupata “mafanikio”, wakiwamo wanasiasa, wafanyabiashara, wafanyakazi, wake, waume, wapenzi, wachumba, wanamuziki, na hata wale wanaotaka  kuwakomesha wabaya wao.

Tuesday, August 28, 2012

Jicho lako likiwa bovu



Bwana wetu Yesu alisema kwamba:
Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote unao mwanga; lakini likiwa bovu, mwili wako nao una giza. Angalia basi, mwanga ulio ndani yako usije ukawa giza.

Basi kama mwanga umeenea katika mwili wako wote, wala hauna sehemu iliyo na giza, mwili wako wote utakuwa na mwanga mtupu; kama vile taa ikumulikiapo kwa mwanga wake. (Luka 11:34-36).
Kati ya mambo ambayo adui yetu shetani anajaribu sana kuyafanya ni kuiba muda ambao tunatakiwa kuwa na Bwana – iwe ni katika kumwomba, kutafakari, kusoma Biblia, kusikiliza ibada, n.k. Adui anajua kuwa, kama akiweza kutufanya tutumie muda mwingi kwa ajili ya mambo mengine badala ya Bwana Yesu, basi mwisho wa safari atakuwa ametunasa, maana Biblia inasema wazi:

Sunday, August 26, 2012

Msalaba wa Kristo



Msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo ndilo jambo kubwa kabisa katika maisha yetu, maana unamaanisha wokovu. Na wokovu ni kila kitu - uponyaji, msamaha wa dhambi, uzima wa milele!

Mimi ninapenda 'country gospel songs'. Naamini nawe utafurahia. Bwana wetu Yesu akubariki.


Thursday, August 23, 2012

Ndugu Waislamu Nisaidieni



Allah katika sura Al-Nisa 4:82 anasema kwamba:

Then do they not reflect upon the Quran? If it had been from [any] other than Allah, they would have found within it much contradiction.

Yaani:

Je, hawaitafakari Quran? Kama isingekuwa imetoka kwa Allah, hakika wangekuta ndani yake sehemu nyingi zinazopingana.

Wednesday, August 22, 2012

Waislamu Wanamgeukia Yesu





Video hii inamwonyesha mtu ambaye ni mzaliwa wa ukoo wa Abu Bakr Saddiq, ambaye alikuwa ni rafiki mkubwa wa Mtume Mohammad. Abu Bakr Saddiq pia ndiye aliyekuwa Khalifa wa kwanza kwenye ulimwengu wote wa kiislamu baada ya kifo cha Mtume Mohammad.

Mzaliwa huyu anaitwa Dk. Nasir Siddiki. Yeye pia ametokea kwenye familia tajiri. Akiwa na umri wa miaka 35 alikuwa tayari ni milionea, huku akimiliki kila kitu cha kupendeza ambacho unaweza kukifikiria – iwe ni magari ya kifahari, majumba, nk.

Monday, August 20, 2012

Free E-Books

Je, umeiona sehemu mpya ya  
Free E-Books hapo juu? 

Fungua sehemu hiyo ujipatie 
E-Books 
za bure ili uweze kujiendeleza 
na kukua kiimani. 

Mungu akubariki.

Saturday, August 18, 2012

Chapa ya Mpinga Kristo - 666


 Kifaa cha kuwekwa kwenye mkono
chini ya ngozi

Makala haya niliyatoa kwenye blog nyingine, inawezekana umeshayasoma, lakini nimeona kuwa ni vema niyatoe tena hapa kwa ajili ya yeyote ambaye hakupata nafasi ya kuyasoma. Hii ni kwa sababu ni makala ya muhimu sana, yanayotuonyesha tuko wapi katika ratiba ya nyakati, majira na unabii.

Utakaposoma kilichoandikwa humu, itakuwa ni jambo jema kuwapatia hata wengine unaowafahamu, ama kwa kwa njia ya baruapepe au kwa kuwaambia wasome makala haya wao wenyewe katika blog hii. Mungu akubariki kwa hilo.

Tuesday, August 7, 2012

Je, Watakatifu Hutuombea Tulio Duniani?



Kanisa Katoliki limekuwa likifundisha kwa miaka na miaka kwamba tunaweza kuwaomba watakatifu walioko mbinguni watuombee kwa Mungu. Je, jambo hili lina ukweli kibiblia? Je, hili ni fundisho la Mungu au ni la wanadamu? Je, mtu anayefanya hivyo anampendeza Mungu au anamuudhi?

Hakuna mahali popote katika Biblia ambapo tumeagizwa kuwaomba watakatifu ili watuombee kwa Mungu. Sasa haya mafundisho yanatoka wapi? Unawezaje kuwafundisha watu kitu kisicho kwenye Biblia halafu usiwe na hatia ya kuongeza au kupunguza ujumbe wa Mungu; maana Bwana anasema kuwa atakayeongeza au kupunguza katika neno lake ana hatia. (Ufunuo 22:19).

Thursday, August 2, 2012

Wana wa Mungu


Nani ni "heroes" wa watoto wako. Je, ni wacheza mieleka? je, ni washika bunduki na wauaji wa kwenye sinema na video? Ukimnunulia zawadi mwanao, je, unamletea nini? Je, ni "toy" ya bunduki au ni nini?

Hatima ya mwanao iko mikononi mwako. Kile unachofanya au usichofanya angali bado mchanga ndicho kitakachoamua maisha yake ya baadaye; na hata uzima au mauti ya milele ijayo.


Contina

Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, ambayo baba zetu walituambia. Hayo hatutawaficha wana wao, huku tukiwaambia kizazi kingine, sifa za BWANA, na nguvu zake, na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya. Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu wawajulishe wana wao, ili kizazi kingine wawe na habari, ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao. (Zaburi 78:3-5).


Kanon Tipton

Wanao wakiyashika maagano yangu, na shuhuda nitakazowafundisha; watoto wao nao wataketi katika kiti chako cha enzi milele. (Zaburi 132:12).

Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, watoto wake watabarikiwa baada yake. (Mithali 20:7).

Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili. (Mithali 20:11).



Kanon Tipton

Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. (Mithali 22:6).